Friday, January 22, 2016

UCHAGUZI ZANZIBAR KURUDIWA MACHI 20

Tume ya Uchaguzi Zanzibar (ZEC) imetangaza tarehe ya marudio ya uchaguzi visiwani humo baada ya matokeo ya uchaguzi uliopita kufutwa.

Uchaguzi huo sasa utafanyika Jumapili tarehe 20 Machi. Tangazo hilo limefanywa na mwenyekiti wa ZEC Jecha Salim Jecha. Bw Jecha amesema tarehe hiyo iliamuliwa na tume baada ya mkutano hapo jana.

"Uchaguzi huo utahusisha uchaguzi wa Rais, wajumbe wa Baraza la Wawakilishi na Madiwani na hakutakuwa na uteuzi mpya wa wagombea wala mikutano ya kampeni," amesema Bw Jecha.

"Wagombea wote walioteuliwa hapo awali wataendelea kuwa wagombea katika uchaguzi huu."

Chama cha Wananchi (CUF) kimekuwa kikipinga kurudiwa kwa uchaguzi. Chama hicho mapema mwezi huu kilionya kwamba hatua hiyo inaweza kusababisha vurugu. Viongozi wa chama hicho walisusia maadhimisho ya Siku ya Mapinduzi wiki iliyopita.

Chama tawala, Chama Cha Mapinduzi (CCM) kilikuwa tayari kimewashauri wanachama wake visiwani wajiandae kwa marudio ya uchaguzi, tangazo lililoshutumiwa vikali na viongozi wa CUF.

ANGALIA PICHA ZA RAIS DR. MAGUFULI AKIWA KATIKA VAZI LA JESHI...!!!

http://jambotz8.blogspot.com/

http://jambotz8.blogspot.com/
Amiri Jeshi Mkuu, Rais Dr. Magufuli akiwasikiliza wananchi kwa makini alipopita maeneno ya Sanawali kuwasalimia wakati akielekea Wilayani Monduli.

Thursday, January 21, 2016

MAGUFULI AMTEUA KIKWETE KUWA MKUU WA CHUO KIKUU CHA DAR ES SALAAM

Rais wa Tanzania Dkt John Magufuli amemteua Rais mstaafu Dkt Jakaya Kikwete kuwa mkuu wa chuo kikuu cha Dar es Salaam.

Tangazo la uteuzi huo limetolewa na katibu mkuu kiongozi Balozi Ombeni Sefue.

Uteuzi huo umeanza kutekelezwa tarehe 17 Januari.

Balozi Nicholas Kuhanga amekuwa akishikilia wadhifa huo kama kaimu, kwa mujibu wa tovuti ya chuo kikuu hicho.

ANGALIA PICHA ZA RAIS DR. MAGUFULI AKISHONA NGUO KWA CHEREHANI...!!!


 Rais Dr. John Pombe Joseph Magufuli akionesha umahiri wake wa kutumia Cherehani na kushona nguo za wafanyakazi wakati alipofanya ziara ya kutembelea na kuvifahamu vitengo mbalimbali na watumishi wake wa  Ikulu jijini Dar es salaam jana Januari 20, 2016.

Saturday, January 16, 2016

UKAWA YASHINDA KITI CHA UMEYA KINONDONI

Diwani wa Kata ya Ubungo kupitia chama cha demokrasia na Maendeleo (CHADEMA) Boniface Jacob ameshinda kiti cha Umeya wa Manispaa ya kinondoni kwa jumla ya kura 38 kati ya 58 zilizo pigwa.

Boniface alikuwa akichuana na mgombea mwenzake ambaye ni mtoto wa kada wa Chama cha Mapinduzi Benjamin Sitta ambaye alikuwa mgombea udiwani katika jimbo la Kawe na hqkufanikiwa kushinda.

Friday, January 08, 2016

WAZIRI ACHUKIZWA NA MADARAJA YA UFAULU

VITA ya kupambana na utendaji kazi usiokuwa na tija kwa Taifa kwa watendaji wengi wa taasisi za Serikali imezidi kushika kasi baada ya Waziri wa Elimu, Sayansi, Teknolojia na Ufundi, Profesa Joyce Ndalichako, kumtaka Katibu wa Baraza la Mitihani la Taifa (NECTA), Dk. Charles Msonde kumwandikia maelezo ya kitaalamu yaliyosababisha kubadilishwa kwa mfumo wa upangaji viwango vya ufaulu kutoka wa madaraja (Division) hadi wastani wa pointi (GPA).

Pia amemtaka kumweleza sababu zilizowafanya kuongeza mtihani (Continuous Assesment) kwa wanafunzi wa kujitegemea ili ajiridhishe pamoja na viongozi wengine wa wizara iwapo mabadiliko hayo yana tija kwa Taifa au la.

Profesa Ndalichako alitoa agizo hilo jana wakati akizungumza kwenye kikao cha menejimenti ya baraza hilo.

MKAPA AJITOSA KUMSAIDIA MAGUFULI

Rais Dk John Magufuli akizungumza na Rais Mstaafu wa Awamu ya tatu Benjamin William Mkapa Ikulu jijini Dar. Picha na Ikulu

Rais mstaafu Benjamin Mkapa amesema yuko tayari kufanya kazi yoyote na kutoa ushirikiano wake kwa serikali ya Rais John Magufuli endapo atahitajika.

Mkapa aliyeambatana na Waziri Mkuu Mstaafu Joseph Warioba ametoa kauli hiyo jana punde baada ya kukutana na Rais John Magufuli Ikulu, Dar es Salaam.

“Rais Mstaafu Mkapa pia amemhakikishia Rais Magufuli kuwa yuko tayari kutoa ushirikiano wakati wote ama kufanya kazi yoyote endapo atahitajika kufanya hivyo,” taarifa iliyotolewa na Ikulu jana mchana imeeleza.

SAMATTA, AUBAMEYANG WATISHA TUZO ZA AFRIKA

Mwanasoka raia wa Tanzania anayechezea TP Mazembe ya Jamuhuri ya Kidemokrasia ya Kongo Mmbwana Ally Samatta amenyakua tuzo ya mwanasoka bora wa Afrika anachezea ndani ya bara la Afrika. Huku tuzo ya mwanasoka bora barani Afrika ikienda kwa Pierre-Emerick raia wa Gabon anayesakata kabumbumbu katika klabu ya Borusia Dotmund nchini Ujerumani.

Tuzo hizo za kila mwaka zinazotolewa na Shirikisho la soka barani Afrika almaarufu kama CAF zimetolewa usiku kuamkia Ijumaa mjini Abuja nchini Nigeria.

Kwa upande wa timu ya wanawake ya mwaka tuzo imekwenda kwa timu ya Cameroon

YANGA YATINGA NUSU FAINALI MAPINDUZI CUP

Mabingwa wa Tanzania Bara Timu ya Yanga, imefanikiwa kutinga hatua ya Nusu fainali kufuatia ushindi wa Bao 2-1 dhidi ya Mtibwa mabao ambayo yamefungwa na wachezaji Aboubakar na Malimi Busungu na kuwa kinara wa kundi B la michuano ya kombe la Mapinduzi baada ya kujikusanyia jumla ya pointi 7.

Katika mchezo mwingine wa mapema kutinga hatua ya nu Nusu Fainali Timu ya Mafunzo imeichapa Azam FC 2-1 kwa ushindi usio na faida kwa timu hiyo baada ya kutupwa nje ya mashindano hayo kwa uchache wa pointi.

Yanga sasa watacheza Nusu Fainali na Mshindi wa Pili wa Kundi A na Mtibwa Sugar kukutana na Mshindi wa Kundi hilo.

Kundi A linamaliza Mechi zake leo Ijumaa kwa Timu ya Jamhuri kuchuana na URA na Simba ikicheza na JKU huku kila Timu ikiwa ina nafasi kutinga Nusu Fainali ikipata matokeo mazuri ingawa Sare kwa Simba itawafikisha Nusu Fainali wakati URA na Jamhuri zikihitaji ushindi.

Thursday, January 07, 2016

MTOTO WA KARUME ASHAURI SHEIN KUKAA PEMBENI

Mwanasheria wa kujitegemea nchini, Fatma ofisinakizungumzaini Dar es Salaam jana. Picha na Florence Majani

Dar es Salaam: Mwanasheria wa kujitegemea nchini, Fatma Karume amemshauri Rais wa Zanzibar, Ali Mohamed Shein kuachia madaraka.

“Dk Shein lazima aondoke kwa sababu kuendelea kubaki madarakani ni kuwanyang’anya Wazanzibari haki yao ya msingi,” alisema Fatma ambaye ni mtoto wa aliyekuwa Rais wa Zanzibar, Amani Abeid Karume.

Akizungumza katika mahojiano maalumu na mwandishi wa habari hizi ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana, Fatma alisema kuwa mzozo wa Zanzibar umesababishwa na Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi ya Zanzibar (ZEC), Jecha Salum Jecha kutangaza kufutwa matokeo yote ya Uchaguzi Mkuu visiwani humo wakati hana mamlaka kisheria kufanya hivyo.

JANUZAJ KUREJEA MAN U

Manchester United imemwita nyumbani Adnan Januzaj kutoka Borussia Dortmund ambako amekuwa kwa mkopo wa msimu mmoja.

United wamemtaka mshambuliaji huyo wa kimataifa wa Ubelgiji arejee Old Trafford kwa sababu ya kukosa kuchezeshwa Ujerumani.

Januzaj, mwenye umri wa miaka 20, amecheza mechi 12 pekee katika klabu hiyo ya Bundesliga, sana akiingia kama nguvu mpya.

Tuesday, January 05, 2016

PROF. JAY KUHAMISHIA STUDIO YAKE MIKUMI

MSANII na Mbunge wa Jimbo la Mikumi, Joseph Haule ‘Profesa Jay’, amesema ana mpango wa kuihamishia studio ya Mwanalizombe kwenye jimbo lake ili aweze kutekeleza ahadi ya kuinua sanaa. Profesa Jay alisema kuwa moja ya ahadi alizowaahidi

wakazi wa Mikumi kwenye kampeni zake ni kuibua vipaji vipya ndiyo maana ameamua kuihamishia studio hiyo huko ili aweze kutekeleza ahadi hiyo.

“Mikumi kuna vipaji vingi vya muziki lakini hakuna aliyeweza kuviibua kwa miaka mingi, ila mimi nikiwa kama Mbunge wao nitatekeleza ahadi hii kwa kuihamishia studio yangu Mikumi ili wasanii chipukizi waweze kufanya kazi zao,” alisema Profesa Jay.

Mwanalizombe ni studio inayomilikiwa na msanii huyo ipo maeneo ya Mbezi Luis, jijini Dar es salaam na imeshatoa nyimbo kali kama Makamanda wimbo wa Sugu, Tatu Chafu na Kipi Sijasikia chini ya mtayarishaji Villy.

BENITEZ ATUPWA NJE REAL MADRID, ZIDANE ACHUKUA NAFASI

Uongozi wa klabu ya Real Madrid umemtimua kocha wake Rafael Benitez ambaye ana Miezi 7 tu katika Mkataba wake wa Miaka Mitatu.

Sasa nafasi yake imechukuliwa na mchezaji mkongwe mfaransa Zinedine Zidane ambaye awali alikuwa Kocha wa Kikosi B cha Real Madrid .

Hii inatokana na matokeo mabaya kwa timu hiyo, ambapo ilitoka Sare 2-2 na Valencia, katika Mechi ya La Liga, Sare ambayo imewaacha Vigogo hao nafasi ya 3 wakiwa nyuma ya Atletico Madrid kwa pointi 4.

Tangu atue Madrid, Benitez amekuwa si kipenzi cha Mashabiki wa Klabu hiyo, baada ya kufungwa bao 4-0 kwenye mechi ya El Clasico Mwezi Novemba na Mahasimu wao Barcelona, pia kutupwa nje ya michuano ya Copa del Rey.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...