Thursday, April 30, 2015

MWANAFUNZI AUAWA BAADA YA KUKUTWA NA BARUA YA MAPENZI

        Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Jacob Mwaruanda
Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa, Jacob Mwaruanda

MWANAFUNZI wa Kidato cha Pili, Jofrey Robert Mwakatenya (15) anatuhumiwa kuuawa kikatili na baba yake mzazi, Robert Mwakatenya (35) baada ya kumkuta akiwa na barua ya mapenzi, inayodaiwa aliandikiwa na rafiki wake wa kike.

Mzazi huyo ambaye ni mfanyabiashara na mkazi wa eneo la Majengo ‘D’ Manispaa ya Sumbawanga, anadaiwa kumwadhibu mwanafunzi huyo, ambaye ni mtoto wake wa kwanza kwa kupiga ngumi na mateke mfululizo kwa zaidi ya saa tatu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Rukwa , Jacob Mwaruanda alithibitisha tukio hilo, lilitokea usiku wa kuamkia Jumapili iliyopita. Alisema bado wanamtafuta mtuhumiwa huyo kwani baada ya kufanya kitendo hicho alitokomea. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SARAFU YA SH. 500 YATENGENEZEWA MIKUFU

miatano
Sarafu mpya ya shilingi 500


SARAFU mpya ya shilingi 500 inadaiwa kuhujumiwa na baadhi ya watu ambao huinunua kwa Sh 2,500 na baadaye kuiyeyusha kwa ajili ya kutengenezea mikufu ya fedha (silver).

Taarifa ambazo MTANZANIA imezipata kutoka vyanzo mbalimbali zinaeleza tangu sarafu hizo zilipotolewa kwa mara ya kwanza Oktoba mwaka jana, baadhi ya watu wamekuwa wakizikusanya na kuzifanya kuadimika mtaani.


Imeelezwa kuwa tangu kutolewa kwa sarafu hiyo imekuwa adimu mitaani jambo ambalo si kawaida kwa fedha mpya zinazoingizwa kwenye mzunguko kuadimika kwa kiwango hicho. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

'TUTAWAREJESHEA WANANCHI MAJIMBO TATA' DL SLAA

http://jambotz8.blogspot.com/
Katibu Mkuu wa CHADEMA, Dk Willibrod Slaa

Katibu Mkuu wa Chadema, Dk Willibrod Slaa amesema endapo vyama vinavyounda Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) vitashindwa kuafikiana katika kuachiana baadhi ya majimbo kabla ya Uchaguzi Mkuu, watawaeleza wananchi kwa kuwa ndiyo kiini cha kuanzishwa kwa umoja huo.

Dk Slaa alisema hayo jana kabla ya kumalizika kwa vikao vya wakuu wa Ukawa ambao wamekubaliana kusimamisha mgombea mmoja kuanzia ngazi ya urais, ubunge na udiwani na kwa siku mbili kuanzia juzi, walikuwa wakijadili ufanikishwaji wa azimio hilo.
Dk Slaa alisema hadi sasa wameshakubaliana kuachiana asilimia 95 ya majimbo yote na kwamba ana matumaini watafanikisha, lakini akaonya kuwa ikishindikana, hawatasita kuwaeleza wananchi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ALI KIBA, DIAMOND, JUX WAPETA TUZO ZA KILI

alikiba1
Ali Kiba


WASANII wa muziki wa bongo fleva, Ali Kiba, Nasibu Abdul ‘Diamond’ na Juma Jux, wameingia katika vinyang’anyiro sita vinavyogombewa katika tuzo za muziki ‘Kili Music Award’.
Ali Kiba ameingia kwenye kipengele cha mtumbuizaji bora wa muziki wa kiume, wimbo bora wa mwaka, mwimbaji bora wa kiume, mtunzi bora, video bora ya mwaka na mwimbaji bora wa Afro-Pop.

jux
Juma Jux

 
Naye Diamond ameingia kwenye kipengele cha mtumbuizaji bora, mwimbaji bora, mtunzi bora, wimbo bora wa Zouk, wimbo bora wa Afro Pop na Video Bora ya mwaka kupitia wimbo wa ‘Nitampata Wapi’ na ‘Mdogo Mdogo’.
Diamond
Nasibu Abdul ‘Diamond’

Pia Juma Jux naye ameingia kwenye kipengele cha mwimbaji bora wa kiume, wimbo bora wa mwaka, mtunzi bora wa mwaka, mwimbaji bora wa kiume na wimbo bora wa R&B kupitia nyimbo zake mbili za ‘Sisikii’ na ‘Nitasubiri’.


Mkuu wa matukio wa Baraza la Sanaa Tanzania Basata, Kurwijira Maregesi, alisema zoezi rasmi la upigwaji wa kura litaanza Mei 4 na kufungwa Juni 5 mwaka huu kwa udhamini mkubwa wa Kampuni ya TBL, kupitia bia yake ya Kilimanjaro. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

'SITAVAA NGUO ZA UTUPU TENA' SNURA MAJANGA

snura
Snura Mushi ‘Majanga’


MWIGIZAJI na mwimbaji wa muziki wa Bongo Fleva, Snura Mushi ‘Majanga’, amesema hatavaa tena nguo za nusu uchi kwa kuwa ameshagundua makosa hayo.

Snura alisema awali alikuwa akivaa mavazi ya nusu uchi au nguo za kumbana, lakini kwa sasa amejirekebisha na anatambua nguo zinazompendeza ili kutokuleta sintofahamu kwa mashabiki wake.


“Kiukweli nashukuru ushauri wa watu katika suala la mavazi, nimeshajirekebisha kwa sasa sivai kama zamani mavazi yasiyofaa katika jamii,” alieleza Snura. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UGAIDI GARISSA, VYOMBO VYA USALAMA VILIZEMBEA

Watu 150 walipoteza maisha kwenye shambulio la Garissa
Waziri wa usalama wa ndani nchini Kenya Generali Joseph Nkaiserry amekiri kwamba vyanzo na duru za kijasusi zilitahadharisha lakini zilipuuzwa kabla ya shambulizi la Al Shabaab katika chuo kikuu cha Garrissa.

Karibu watu 150 walikufa wakati wa shambulio hilo. Waziri Nkaissery ameongeza kusema shughuli za wokozi zilizofuata pia zilifanywa kiholela.

Baadhi ya Maafisa wakuu wa polisi wamesimamishwa kazi kufuatia shambulia hilo la Chuo Kikuu cha Garrissa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC Swahili

KIJANA MDOGO AOKOLEWA AKIWA HAI SIKU BAADA YA KUFUKIWA NA KIFUSI...!!!

Kijana aokolewa siku tano baada ya kufunikwa na kifusi
Watoa huduma za uokoaji huko mji mkuu wa Nepal Kathmandu, wamefanikiwa kumuokoa kijana mmoja mwenye umri wa miaka 15 aliyepatikana hai baada ya funikwa na vifusi vya jengo alilokuwemo wakati wa tetemeko la ardhi kukumba taifa hilo siku tano zilizopita.

Licha ya kuwa chini ya maporomoko hayo kwa siku hizo tano isaidiwa na mwanya uliokuwa ukipenyeza hewa iliyomwezesha kupumua japo kwa shida. Makundi ya watu walimshangilia alipotolewa huku akionekana akijitahidi kufungua macho yake.Alikimbizwa hospitali mara moja kupata matibabu zaidi.

Zaidi ya watu 5,500 wamethibitishwa kufariki kutokana na janga hilo. Wengi wa wanavijiji wangali wanasubiri misaada ya chakula na maji safi ya kunywa huku mashirika ya kutoa misaada ya kisema huenda ikachukua siku nyengine 5 kabla ya kuwafikia baadhi yao kutokana na kuharibiwa kabisa kwa miundo mbinu.

Umoja wa mataifa umetoa wito kwa jumuiya ya kimataifa kuendelea kutoa misaada wakikadiria michango inayohitajika kuwa zaidi ya dolla millioni 415 kuisaidia Nepal katika kipindi cha miezi 3 ijayo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Thursday, April 23, 2015

AJARI ZARUDI TENA, BASI LAUA 10 SHINYANGA

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga.

Kamanda wa kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga
SIKU sita tangu ajali ya basi dogo aina ya Toyota Hiace kuua watu 19 mkoani Mbeya, nchi imeendelea kukumbwa na ajali za barabarani. Safari hii watu kumi wamekatishwa uhai, kutokana na ajali ya basi na lori, iliyotokea mkoani Shinyanga jana.


Katika ajali hiyo, watu tisa walikufa papo hapo na mmoja aliaga dunia akipatiwa matibabu katika Hospitali ya Mkoa wa Shinyanga. Abiria 51 walijeruhiwa na wanatibiwa hospitali hapo, wakati tisa, akiwemo dereva wa basi, wako katika hali mbaya.

Ajali hiyo ilitokea katika kijiji cha Ibingo Kata ya Samuye wilayani Shinyanga Vijijini na ilithibitishwa na Kamanda wa Polisi Mkoa wa Shinyanga, Justus Kamugisha.

Alisema ajali ilitokea majira ya saa 9:30 alasiri baada ya basi la kampuni ya Unique, lililokuwa linatoka Mwanza kwenda Tabora kugongana na lori la kampuni ya Coca Cola, lililokuwa linatoka Kahama. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ORODHA VYAMA VYA KIJAMII VITAKAVYOFUTWA KUANZA KUTOLEWA

Msemaji wa Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nch, Isaac Nantanga.
 
WIZARA ya Mambo ya Ndani ya Nchi, wakati wowote wiki hii itaanza kutoa orodha ya vyama vya kijamii vitakavyofutwa kwa kuanzia na mkoa wa Dar es Salaam.

Imesema vyama hivyo vitafutwa kutokana na kutotekeleza matakwa ya kisheria ya kuwasilisha taarifa za mwaka za ukaguzi wa hesabu za vyama na vile ambavyo havilipi ada ya mwaka kama sheria inavyoelekeza.

Msemaji wa wizara hiyo, Isaac Nantanga alisema hayo jana katika taarifa yake kwa vyombo vya habari kufafanua suala la uhakiki wa vyama vya kijamii nchini.

Alisema vyama vitakavyobainika vitafutwa katika Daftari la msajili wa vyama vya kijamii na wala siyo Taasisi zisizo za kiserikali (NGO,s) kwani haihusiki nazo.

“Orodha ya vyama vitakavyofutwa itaanza kutolewa kwa awamu kuanzia wiki hii na kwa kuanzia orodha hiyo itahusu vyama vilivyosajiliwa mkoa wa Dar es Salaam”Alisema 

Alisema kufuatana na orodha iliyopo vyama 10,000 vya kijamii na Taasisi za Dini vimesajiliwa na wizara hiyo na vitakavyofutwa ni vile tu ambavyo haviwasilishi taarifa za kila mwaka za ukaguzi wa hesabu zao na pia kama havilipi ada ya kila mwaka kama sheria inavyotaka.

Juzi, gazeti moja la kila siku liliandika kuwa Waziri wa Mambo ya Ndani Mathias Chikawe anaanza kuhakiki NGOs jambo ambalo siyo la kweli kinachofanyika ni kwa taasisi za kijamii. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO ALHAMIS APRILI 23, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01667
DSC01668
DSC01669 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

VOLCANO YALIPUKA CHILE

Mlipuko wa Volcano 
 
Volcano aina ya Calbuco imelipuka kwa muda mfupi huko ikiwa ni mara ya kwanza ndani ya zaidi ya miaka 40. Watu waliokuwa wakiishi maeneo jirani na ulikotokea mlipuko wa Volcano hiyo wamelazimika kuyahama makazi yao.

Picha za televisheni zilionyesha wingu zito na majivu vikipanda hewani umbali kilomita kadhaa angani katika jimbo la Los Lagos kusini mwa Chile.

Mamlaka nchini humo zimetoa tangazo la hali ya hatari kwa wakazi wote ambao wapo umbali wa kilomita la mlipuko wa Volcano hiyo huku safari za ndege kuelekea eneo hilo zikiwa zimeahirishwa. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

HALI MBAYA YEMEN...!!!

Wapiganaji wa Houthi nchini Yemen 
 
Shirika la kimataifa la msalaba mwekundu limesema kuwa hali inazidi kuwa mbaya nchini Yemen, huku Mji mkuu Sanaa ukikosa umeme na maji kwa kipindi cha siku tisa zilizopita.

Afisa wa ngazi ya juu wa Shirika hilo nchini humo Robert Mardini amesema ameshuhudia miili kadhaa kwenye mitaa alipotembelea mji wa Aden, na kueleza kuwa changamoto iliyopo ni upelekaji wa huduma za kitabibu.

Awali Saudi Arabia ilisema itaendelea kutumia jeshi kuzuia waasi wa kihudhi kudhibiti Yemen, waasi nao wametaka kumalizwa kwa mashambulizi ya anga dhidi yao na kuanza mazungumzo.
Mpiganaji anayemuunga mkono Rais Abdrabbuh Mansour Hadi amesema ni mapema mno kuanza kuzungumzia makubaliano kati ya pande mbili. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TIMU 4 ZATINGA NUSU FAINALI ULAYA


Javier Hernandez akishangilia goli mbele ya mashabiki wa Real Madrid
Timu nne zimetinga hatua ya nusu fainali katika ligi ya mabingwa barani Ulaya iliyokamilika hapo jana, baada ya Real Madrid ya Hispania na Juventus ya Uitaliano kufanikiwa kuingia nusu fainali.
Timu ya Juventus
Wakicheza katika uwanja wao wa nyumbani wa Santiago Bernabeu, Madrid walilazimika kusubiri hadi dakika ya 88, walipopata bao lao la pekee lililotiwa kimia Javier Hernandez almaarufu kama Chicharito,na hivyo kuhitimisha safari ya Atletico Madrid.
Katika msimu uliopita, huko Lisbon Ureno, Atletico walitolewa na Real Madrid katika hatua ya fainali.
Nayo Juventus imezima matumaini ya Monaco ya Ufaransa kwa kulinda bao lake lililofungwa katika mechi ya awali na hapo matokeo ikawa sare ya bila kutofungana. Hata hivyo nyota ni njema kwa Spain ambao sasa wanawakilishwa na timu mbili ambazo ni Real Madrid na Barcelona. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Monday, April 20, 2015

CHADEMA: ZITTO NI ADUI YETU NAMBA MOJA...!!!

MNYIKA
Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, John Mnyika

CHAMA cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema) kimetangaza kuwa adui yake namba moja ni Kiongozi Mkuu wa Chama cha Alliance for Change and Transparance (ACT-wazalendo), Zitto Kabwe.

Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Bara, John Mnyika akihutubia mkutano wa hadhara uliofanyika Uwanja wa Furahisha Mwanza juzi, alisema Chadema haiko tayari kuikaribisha ACT-Wazalendo ndani ya Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) kutokana na kile alichosema ‘ni adui kwao’.

“Mtume Muhamad (S.A.W) alikuwa anazungumzia unafiki ambao una sura mbili na sifa zake, leo (ACT) wanasema wapo upinzani, wanasema msiunge mkono Ukawa halafu mnawakaribisha?

“Nendeni kila mahali waambieni wananchi adui yetu mkuu ni Zitto. Sikilizeni niwaambie Taifa hili kama ni ufisadi tumeshazungumzia sana kuanzia EPA mpaka Richmond. Dk. Slaa (Willbrod) alipoingia bungeni aliyasema haya kwa sasa si mapya. Adui yetu ni Zitto na hatumtaki Ukawa,” alisema Mnyika.

Alisema Chadema haiko tayari kuikaribisha ACT-Wazalendo Ukawa kwa sababu adui kwao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ANGALIA PICHA ZA MAMIA YA WATU WALIOHUDHURIA MKUTANO WA ACT-WAZALENDO MKOANI MWANZA

Kiongozi wa Chama cha ACT-Wazalendo, Zitto Kabwe, akiwahutubia wakazi wa mji wa Mwanza kwenye viwanja vya Furahisha jijini humo.

 Umati wa watu ukiwa katika mkutano wa ACT-Wazalendo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
(Picha na Said Powa)

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMATATU APRILI 20, 2015 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01536

DSC01535 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

LOWASSA ATHIBITISHA UBORA WA AFYA YAKE

lowassa 1

Waziri Mkuu wa zamani, Edward Lowasa akiwa katika matembezi ya kupinga mauaji ya albino.

WAZIRI Mkuu wa zamani, Edward Lowasa, jana alithibitisha kwa vitendo kuwa afya yake iko safi baada ya kutembea umbali wa kilomita tano kwa miguu kwenye matembezi ya kupinga mauaji ya albino nchini.

Kwa muda mrefu, Lowassa ambaye ni mmoja wa makada wa Chama Cha Mapinduzi (CCM) wanaotajwa kuwania nafasi ya urais katika uchaguzi mkuu wa Oktoba mwaka huu, amekuwa akidaiwa kuwa na matatizo ya afya na kuwa hawezi kuhimili mikimiki ya kampeni na shughuli nyingine zinazohitaji nguvu.

Lakini matembezi ya jana yaliyoongozwa na Lowassa kuanzia Uwanja wa Taifa wilayani Temeke mpaka viwanja vya TCC Chan’gombe na kutumia dakika 25, yamedhihirisha vinginevyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

UCHINA KUWEKEZA MABILIONI PAKISTAN

Bango la kumkaribisha rais Xi nchini Pakistan.
Rais wa China Xi Jinping ameanza ziara ya siku mbili nchini Pakistan hii leo.
Bwana Xi atazindua mpango wa uwekezaji wa kichina wa gharama ya dola bilioni 50 ambao Pakistan ina matumaini kuwa utasuluhisha tatizo lake ya nishati.

Mpango huo unaofahamika kama barabara ya uchumi ya China na Pakistan ni pamoja na barabara , reli na mabomba ya jumla ya umbali wa kilomita 3000 kutoka mji wa bandari wa Gwadar nchini Pakistan hadi mji wa ulio mashariki mwa China wa Kashgar.

Waandishi wa habari wanasema kuwa lengo la China ni kuongeza ushawishi wake wa kiuchumi kwa Pakistan ili kulegeza ule wa Marekani na India. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SULUHU YATAKIWA KUHUSU WAHAMIAJI

Boti ya Italia iliyokuwa katika Operesheni ya kuokoa wahamiaji ikiwa imebeba wahamiaji walikuwa wakisafiri kwenda Ulaya.
 
Waziri mkuu wa Italia Matteo Renzi ametoa wito wa kufanyika kikao cha dharura cha viongozi wa umoja wa ulaya kujadili swala la wahamiaji wanaoangamia kwenye bahari ya Meditarenean wakijaribu kuingia ulaya. Inafuatia ajali ya hivi punde ambao karibu watu 700 wanahofiwa kufa maji baada ya boti kuzama baharini kaskazini mwa Libya, kilomita 200 kutoka kisiwa cha Lampedusa, nchini Italia.

Manusura 28 wa janga la hivi punde kwenye bahari ya Meditaranean walitarajiwa kufikishwa kisiwani Sicily alfajiri ya Jumatatu. Hadi kufikia usiku, ni miili 24 iliyokuwa imeopolewa, na maafisa wa usalama kwenye pwani ya Italia, wakaipeleka kisiwani Malta.

Ni vigumu kuhakikisha idadi ya watu walioanza safari kwenye boti hiyo kutoka pwani ya Libya. Lakini walionusurika wanasema walikuwa kati ya watu 500 na 700 kabla ya kupinduka kilomita mia mbili kutoka Lampedusa, kwenye maji ya Libya. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MSIMAMO WA LIGI KUU TANZANIA BARA

IMG_4798

Rnk
Team MP W D L GF GA +/- Pts

1
Young Africans 21 14 4 3 39 12 27 46

2
Azam 22 11 9 2 29 15 14 42

3
Simba SC 22 9 8 5 27 17 10 35

4
Kagera Sugar 23 8 7 8 22 22 0 31

5
Ruvu Shooting 23 7 8 8 16 21 -5 29

6
Mtibwa Sugar 23 6 10 7 22 23 -1 28

7
Mbeya City 23 6 10 7 19 21 -2 28

8
Mgambo JKT 22 8 4 10 18 21 -3 28

9
Stand United 22 7 7 8 19 24 -5 28

10
Coastal Union 23 6 9 8 16 23 -7 27

11
JKT Ruvu 23 6 7 10 17 23 -6 25

12
Ndanda 23 6 7 10 18 26 -8 25

13
Polisi Morogoro 23 5 9 9 15 22 -7 24

14
Tanzania Prisons 23 3 13 7 15 22 -7 22
 Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

LOOO...!!! SIMBA NOMA "INA WAGANGA WENGI WA KIENYEJI KULIKO WATAALAMU WA BENCHI LA UFUNDI"

IMG_9433
Simba waligoma kuingia kwenye vyumba vya kubadilishia nguo walipocheza na Mbeya City jumamosi iliyopita uwanja wa Sokoine

MTANDAO wa SHAFFIH DAUDA kwa muda mrefu sasa umekuwa ukifanya tafiti na kufuatilia mwenendo wa klabu ya Simba katika mechi za ligi kuu soka Tanzania bara msimu huu.
Mwishoni mwa juma lililopita, Simba ilifungwa magoli 2-0 na Mbeya City fc katika uwanja wa Sokoine, Mbeya na kuifanya klabu hiyo kongwe nchini kuendelea kukaa nafasi ya tatu kwa pointi 35 walizokusanya baada ya kushuka dimbani mara 22.
Machi 18 mwaka huu walifungwa magoli 2-0 na Mgambo JKT katika uwanja wa CCM Mkwakwani Tanga, lakini wakashinda 2-1 ugenini dhidi ya Kagera Sugar uwanja wa CCM Kambarage, Shinyanga na ilikuwa aprili 6 mwaka huu (jumatatu ya pasaka).
Katika mechi hizo tatu, mtandao huu ulikuwa unachunguza mwenendo wa Simba na namna wanavyoiandaa timu kwa ajili ya mechi. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MBWANA AWATAKA MASHABIKI WA PRISONS KUISAPOTI HADI MWISHO

makata-march6-2015
Mbwana Makata, kocha mkuu wa Tanzania Prisons.
 
MBWANA Makata, kocha mwenye uzoefu wa kufundisha timu za majeshi safari hii amepewa jukumu la kuibakisha Tanzania Prisons ligi kuu Tanzania bara msimu ujao.

Makata, kocha wa zamani wa JKT Ruvu na JKT Oljoro jana ameiongoza Prisons kupata sare nyumbani ya goli 1-1 dhidi ya Wakata miwa wa Mtibwa Sugar katika mechi ya ligi kuu iliyopigwa uwanja wa CCM Kumbukumbu ya Sokoine, Mbeya.

Baada ya sare hiyo, Makata amesema: “Mechi ilikuwa ni muhimu kwetu kuweza kupata matokeo ya ushindi, lakini mechi ilikuwa ngumu na tumeweza kutapa sare ya goli 1-1. Kikubwa niwapongeze vijana wangu kwasababu ratiba kwetu ilibana wiki hii, tulicheza jumatano, tukawa safarini na kucheza tena leo (jana), muda wa maandalizi haukuwepo."

"Cha msingi niwaombe wakazi wa Mbeya, mashabiki wa Prisons waisapoti timu yao, tupambane mpaka dakika za mwisho tuone nini kitatokea” Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Sunday, April 19, 2015

ALIYENUSURIKA AJALI MBEYA ASIMULIA..!!!

Mmoja wa manusura  wa ajali iliyotokea eneo la Mto Kiwira, Rungwe mkoani Mbeya, Mariam Manfredy akiwa amelazwa kwa matibabu katika  Hospitali ya Rufaa Mbeya. 

Mmoja wa majeruhi wa ajali iliyoua watu 19, Mariam Manfredy (28) aliyevunjika mguu wa kushoto, anasimulia ajali hiyo na kusema chanzo ni mwendo kasi na kuungua kwa breki.

Gari hilo lilikuwa ‘limeshona’ abiria, lilikuwa likitoka jijini Mbeya  kwenda Kiwira wilayani Rungwe kabla ya kuanguka eneo la Mto Kiwira na kuua watu 18 palepale na mmoja alifia Hospitali ya Igogwe huku wengine watatu wakijeruhiwa.

Mariam aliyelazwa katika Hospitali ya Rufaa Mbeya (MRH), alisema alipanda basi hilo katika Kijiji cha Simambwe akienda Kiwira kununua bidhaa za biashara. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MADEREVA WA MABASI KAMA WA BODABODA...!!!

Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, akitoa takwimu za vifo vilivyotokana na ajali za barabarani kati ya Januari Mosi mwaka huu hadi Aprili 12, sawa na siku 102 vifo 969.
Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, akitoa takwimu za vifo vilivyotokana na ajali za barabarani kati ya January Mosi hadi Aprili 12 mwaka huu, sawa na siku 102 vifo 969.

WAKATI ajali za barabarani zikiendelea kumaliza nguvu kazi ya Taifa na kuumiza vichwa vya Watanzania kuhusu suluhisho la ajali hizo, imefahamika moja ya tatizo sugu ni kukosekana kwa madereva wenye taaluma stahiki, ingawa wana leseni.

Wiki hii peke yake, ajali tatu za mabasi zilizotokea Mbeya, Morogoro na maeneo ya Mwanza, zimesababisha vifo vya watu 40 ndani ya siku sita.

Tayari Kamanda wa Kikosi cha Usalama Barabarani, Mohamed Mpinga, ametoa takwimu za vifo vilivyotokana na ajali za barabarani kati ya Januari Mosi mwaka huu hadi Aprili 12, sawa na siku 102 vifo 969. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMAPILI APRILI 19, 2015 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01499
DSC01500
DSC01501 
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...