Saturday, January 24, 2015

HIKI NDICHO ALICHOKISEMA PROF. MUHONGO ALIPOTANGAZA KUJIUZULU LEO...!!!

Aliyekuwa Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhuongo akizungumza na waandishi wa habari ofisini kwake leo.
Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhuongo, amejiuzulu wadhifa huo kutokana na kuchoshwa na sakata la Akauti ya Tegeta Escrow.

Akizungumza na waandishi wa habari Ofisini kwake jijini Dar es Salaam leo, Barabara ya Samora, Profesa Sospeter Muhongo amesema ameamua kujiuzulu ili kuwa sehemu ya suluhisho la suala la akaunti ya Tegeta Escrow.

Aidha Muhongo alisema kuwa suala la ankauti ya Tegeta Escrow limekuwa likizungumzwa na kufanya mambo mengine yasiendelee na huku watanzania walio wengi ni masikini wakihitaji umeme na sio kuuliza tegeta Escrow. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Friday, January 23, 2015

HATIMA YA MUHONGO NDANI YA SAA 48 ZIJAZO...!!!

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo.

Zikiwa zimebaki siku tatu kabla ya Bunge la Jamhuri ya Muungano kuanza mjini Dodoma, sasa hakuna shaka kwamba Rais Jakaya Kikwete atafanya mabadiliko katika Baraza la Mawaziri wakati wowote kuanzia leo na kabla ya Jumapili (saa 48) kutokana na kukabiliwa na safari ya nje.
Rais anatarajiwa kufanya mabadiliko hayo baada ya kumwondoa Anna Tibaijuka, ambaye alikuwa Waziri wa Ardhi, Nyumba na Maendeleo ya Makazi kwa kuhusishwa na kashfa ya uchotwaji fedha kwenye Akaunti ya Tegeta Escrow baada ya kuingiziwa Sh1.6 bilioni kwenye akaunti yake.
Mwingine ni Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo, ambaye anatuhumiwa kutoshughulikia kwa makini sakata hilo na kusababisha Serikali kupoteza fedha hivyo kuwapo kwa uwezekano mkubwa wa kumvua uwaziri utakaomlazimu Rais kufanya mabadiliko madogo kwenye baraza lake, ikiwa ni miezi isiyozidi mitano kabla ya kuvunja Bunge kupisha Uchaguzi Mkuu wa Oktoba.
Habari ambazo Mwananchi imezipata zinaeleza kuwa Rais Kikwete anaweza kutangaza mabadiliko hayo wakati wowote kuanzia leo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

HUYU NDO MTANZANIA TAJIRI ANAYE ENDESHA MAGARI YA KIFAHARI NA YA BEI KULIKO MTANZANIA MWINGINE...!!!

Kama ndo machine aliyo nunua safari hii basi katisha aisee maana hii ni one of the most expensive and luxury cars around na hela yake ni ndefu sana. It's confirmed gari kanuna na soon mtaiona mitaa ya kati. Davis yaelekea ni mpenzi sana wa magari mazuri na of course uwezo wa kuyanunua anao cause he works so damn hard. Hongera sana Davis can't wait to see this new toy in Bongo.  Hii ndo inaitwa "Tumia Pesa Ikuzoeee"
Hi ni gari nyingine aina ya Lamborghini anayo miliki mfanyabiashara Davis Mosha huko Bongo.  "Heshima Pesa Shikamoo Makelele"
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

EMIRATES KUMWAGA AJIRA KWA WATANZANIA

Simba Yahya
 Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Simba Yahya

KATIKA kutekeleza moja ya malengo ya Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa hususan kuwatafutia ajira Watanzania nje ya nchi, Wizara hiyo kupitia Ubalozi Mdogo wa Tanzania uliopo Dubai, Umoja wa Falme za Kiarabu umefanikisha kulishawishi Shirika la Ndege la Emirates kuajiri Watanzania wengi zaidi kuanzia mwaka 2015.
Emirates, moja ya mashirika ya ndege tajiri zaidi duniani, linamiliki zaidi ya ndege za kisasa 280, huku likiwa na safari za uhakika duniani kote.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Mkurugenzi wa Idara ya Mashariki ya Kati katika Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Simba Yahya alisema shirika hilo litaajiri Watanzania katika kada mbalimbali.
“Wamekubali kuajiri Watanzania katika kada mbalimbali, ambapo maofisa wake wanaosimamia ajira watakuja nchini (Tanzania) Machi 2015 kwa ajili ya kuwafanyia usaili Watanzania watakaoomba kazi hizo na kupata uteuzi wa awali,” alisema.
Aliwataka Watanzania kuchangamkia ajira hizo, ambazo awali zilitangazwa Julai 2014, lakini ni Watanzania wachache tu walioomba na hivyo kutofikia lengo lililokusudiwa.
“Baada ya mazungumzo ya kina, uongozi wa Emirates umekubali kuongeza muda wa kuzitangaza ajira hizo kwa mara nyingine na kupanga kufanya usaili kama ilivyoelekezwa hapo awali,” alisema.
Aliwasisitiza Watanzania wenye sifa na vigezo stahiki, kutumia fursa hiyo kuomba nafasi hizo na pia kujiandaa vyema katika usaili ili wajihakikishe ajira katika soko la ajira la kimataifa.
Kaimu Mtendaji Mkuu kutoka Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA), Boniface Chandaruba aliwataka waombaji wote kuhakikisha wanapata barua kutoka wakala huo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 23, 2015


.
.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KAMATI TATU ZA BUNGE ZAMGOMEA MAKINDA


Spika wa Bunge, Anne Makinda (kulia) akiongoza kikao cha Kamati ya Uongozi kinachojumuisha wenyeviti wote wa Kamati za Bunge kilichokutana jana kupanga ratiba ya mkutano wa Bunge unaotarajiwa kuanza vikao vyake Jumanne ijayo. Kikao hicho kilifanyika katika Ofisi Ndogo ya Bunge.

Danadana zimeendelea juu ya utekelezaji wa azimio la tatu la Bunge kuhusu kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow linaloagiza kuwajibika kwa wenyeviti wa kamati zake tatu za kudumu, baada ya juzi Spika wa Bunge, Anne Makinda kukaririwa akisema wameshajiuzulu, lakini wajumbe wake wameibuka jana na kusema hawatafanya uchaguzi hadi watakapopata maelekezo kutoka Ofisi ya Spika.

Azimio hilo ambalo ni moja ya manane ya Bunge hilo linasema: “Kamati husika za Kudumu za Bunge zichukue hatua za haraka na kwa vyovyote vile kabla ya Mkutano wa 18 wa Bunge, kuwavua nyadhifa zao wenyeviti tajwa wa kamati husika za kudumu za Bunge.”

Wenyeviti hao na kamati zao katika mabano ni Victor Mwabalaswa (Nishati na Madini), Andrew Chenge (Bajeti) na William Ngeleja (Katiba, Sheria na Utawala).

Juzi, Spika Makinda aliwaeleza waandishi wa habari kwamba wenyeviti waliotakiwa kuvuliwa nyadhifa zao tayari wamejiuzulu na kamati husika zinatakiwa kufanya uchaguzi kupata wengine wapya. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

CCM YAREJESHA AMANI SUDAN KUSINI

Rais Jakaya Kikwete akiwa na Rais Salva Kiir wa Sudan ya Kusini (kushoto), Makamu wa Rais wa zamani wa Sudan, Dk Riek Machar (wa pili kulia) na Deng Alor Kuol wakitia saini mkataba wa makubaliano ya kukiunganisha upya chama cha SPLM cha Sudan Kusini katika Hoteli ya Ngurdoto jijini Arusha juzi usiku. Nyuma yao ni mjane wa marehemu, John Garang aliyekuwa Mwenyekiti wa SPLM, Rebecca Nyandeng de Mabior na Ofisa wa Wizara ya Mambo ya Nje na Ushirikiano wa Kimataifa, Thobias Makoba. Nyuma yao wakishuhudia utiaji saini huo ni Makamu wa Rais, Dk Mohamed Ghalib Bilal, Rais Uhuru Kenyatta wa Kenya na Rais Yoweri Museveni wa Uganda. (Picha na Ikulu).
BAADA ya miezi mitano ya mazungumzo ya kurejesha amani Sudan Kusini yaliyoratibiwa na chama tawala, CCM, hatimaye Rais wa nchi hiyo, Salva Kiir na hasimu wake, Riek Machar wamesaini makubaliano ya kusitisha mapigano, yaliyoibuka tangu mwaka 2011.
Kutokana na machafuko hayo, zaidi ya raia 20,000 wa Sudan Kusini, wamepoteza maisha huku wengine zaidi ya milioni moja wakikosa makazi.
Walisaini makubaliano hayo juzi usiku jijini hapa, huku marais wa ndani na nje ya nchi wanachama wa Jumuiya ya Afrika Mashariki (EAC), wakiongozwa na Rais Jakaya Kikwete, wakishuhudia.
Wengine walioshuhudia makubaliano hayo ni Rais wa Kenya, Uhuru Kenyatta, Naibu Rais wa Afrika ya Kusini, Cyril Ramaphosa , Rais wa Uganda, Yoweri Museveni, Salva Kiir, Riek Machar na Makamu wa Rais wa Tanzania, Dk Mohammed Gharib Bilal. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

CHANJO DHIDI YA EBOLA KUWASILI LIBERIA

 Chanjo ya majaribio dhidi ya ugonjwa wa Ebola iko njiani kuelekea nchini Liberia.
Hii ni mara ya kwanza kwa chanjo hii kupelekwa kwenye nchi iliyoathiriwa zaidi na Ebola.
Lakini Wataalamu wanasema, wakati huu maambukizi ya Ebola yakiwa yanapungua, itakuwa vigumu kubaini kama chanjo hii inatoa kinga dhidi ya Virusi vya ugonjwa huo.

Chanjo hii ilitengenezwa na Kampuni moja ya Uingereza, GlaxoSmithKline (GSK )na Taasisi ya kitaifa ya afya nchini Marekani. GSK imesema ndege iliyo na dozi za awali takriban 300 za chanjo inatarajiwa kufika Monrovia siku ya ijumaa.
Kampuni ina matumaini mtu wa kwanza kujitolea atapata chanjo hiyo wiki chache zijazo.
Wanasayansi wanalenga kuwahusisha watu watakaojitolea takriban 30,000 katika majaribio hayo wakiwemo wafanyakazi wa afya. Ikiwa taratibu zote zitafuatwa, Watu 10,000 watapatiwa chanjo ya GSK.

Wataalamu wanaona itakuwa vigumu kubaini kama chanjo hiyo itafanya kazi 
 
Idadi hiyohiyo ya watu watapata chanjo aina ya Placedo ,na wengine 10,000 chanjo nyingine ya majaribio. Matokeo yatalinganishwa ili kubaini kama kuna chanjo yeyote kati ya hizo imefanya kazi dhidi ya Virusi vya Ebola.
Majaribio kama hayo tayari yalifanyika kwa wafanyakazi wa afya 200 waliojitolea nchini Uingereza, Marekani, Switerland na Mali.
Shirika la GSK limesema chanjo hizo zimeleta matokeo chanya. Lakini ni kwa nchi zilizoathirika pekee ambapo wataalamu watasema kama inatoa kinga thabiti.
Kampuni inasisitiza kuwa Chanjo bado iko katika uboreshwaji na Shirika la Afya duniani, WHO na wakaguzi wengine wanakazi ya kuhakikisha kuwa wanajiridhisha kuhusu ubora na usalama wake kabla ya kampeni za matumizi ya kinga hiyo .
Chanjo hizo pia zimepangwa pia Guinea, Liberia,na Sierra Leone miezi kadhaa ijayo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

MFALME ABDULLAH WA SAUDIA AFARIKI DUNIA

Hayyat Mfalme Abdullah 
 
Taarifa zilizotufikia hivi punde zinaeleza kuwa mfalme wa Saudia Abdullah bin Abdulaziz amefariki dunia akiwa hospitalini .
Tamko la kifo cha mfalme huyo zilitolewa na kaka wa mfalme huyo aitwaye , Salman,ambaye naye aliwahi kuwa mfalme.
Kabla ya tamko hilo television ya taifa la Saudi lilikatiza matangazo yake na kuweka nyimbo za quraan ,kama ishara ya kifo cha kiongozi wa juu wa ufalme.
King Abdullah, amefariki dunia akiwa na miaka 90, alilazwa hospitalini kwa wiki kadhaa tangu December mwaka wa jana kutokana na maambukizi kwenye njia ya hewa.
Mfalme huyo aliingia madarakani mwaka 2005 lakini alikuwa ni dhaifu mwenye kushambuliwa na maradhi mara kwa mara. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

MWAMUZI YANGA, RUVU AFUNGIWA

Mshambuliaji wa Yanga, Amis Tambwe 
SIKU moja baada ya Klabu ya Yanga kulalamika kudhalilishwa kwa mchezaji wake, Amisi Tambwe katika mchezo wao dhidi ya Ruvu Shooting, Kamati ya Waamuzi ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), imemwondoa kuchezesha mechi za Ligi Kuu mwamuzi wa pambano hilo kwa kushindwa kulimudu.
Kwa mujibu wa Mwenyekiti wa Kamati ya Waamuzi ya TFF, Salum Chama, mwamuzi huyo Mohammed Theofil ameondolewa kuchezesha ligi hiyo ya Tanzania Bara kwa kipindi kilichobaki.
Katika mchezo huo uliochezwa mwishoni mwa wiki kwenye Uwanja wa Taifa Dar es Salaam na kusimamiwa na mwamuzi huyo wa kati, timu ya Ruvu Shooting ilionesha mchezo wa kibabe ambapo baadhi ya wachezaji wake walifanya vitendo vya utovu wa nidhamu pasipo kuadhibiwa.
Mchezo huo ulisababisha mshambuliaji wa Yanga, Tambwe ambaye ni raia wa Burundi, kulalamika kwamba alidhalilishwa, huku akidai kuumizwa baadhi ya maeneo ya mwili wake na akidai kuwa aliitwa mkimbizi.
Lakini akizungumza jana akiwa jijini Mwanza, Chama ambaye pia ni Mjumbe wa Kamati ya Utendaji ya TFF na Katibu wa Chama cha Soka Kagera, alithibitisha kuondolewa kwa mwamuzi Theofil. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

ARSENE WENGER "VIBALI VYA KAZI VIFUTWE"

Kocha wa Arsenal, Arsene Wenger
Meneja wa Arsenal Arsene Wenger ametaka kanuni za kutoa kibali cha kufanya kazi kwa ajili ya wachezaji ambao hawamo kwenye umoja wa ulaya zifutwe.
Wenger anaejaribu kumsajili Gabriel Paulista kutoka Villarreal ambae anahitaji kibali cha uidhinisho toka nchini kwake sababu hajawahi kulitumikia taifa lake.
Bosi huyo amekosoa mpango wa mapendekezo ya kupunguza idadi ya wachezajitoka mashirikisho yasiyo ya Umoja wa Ulaya wenye pasipoti katika michezo ya ligi ya England msimu ujao.
Akasema "Kusema ukweli inapaswa funguliwa kabisa, na kila mtu anaweza kungia"
Kwasasa kibali cha kufanyia kazi kwa nchi zisizo umoja wa Ulaya kunahitajika kuwa katika nafasi 70 za juu katika ubora wa viwango vya Fifa na awe amecheza kwa asilimia 75 katika timu ya taifa ndani ya miaka miwili.
"Ili kumsajili Paulista tungeweza kuwashawishi maofisa wa kwao kuwa ni beki wa kipekee mwenye kipaji."
Chama cha Soka cha Englan kinataka kupunguza idadi ya wachezaji wasiokua wenyeji wa jumuiya ya ulaya kufikia asilimia 50 kwenye ligi. Lakini Wenger anadhani kuondoa kanuni itakuwa bora kwa ajili vijana wachezaji Kiingereza.
"kufunga mipaka ya nchi na kuruhusu kucheza wachezaji wa Kiingereza tu Nini kitatokea? Ni kuua mvuto wa ligi dunia kote. Wenger alisema Arsenal walitaka kumsajili winga wa kimataifa wa Ajentina Angel Di Maria lakini kibali cha kazi kikaleta shida.
Wenger aliongeza "Tulimtambua Di Maria alipokuwa 17.Tulimuona akiwa katika mashindano ya kimataifa na tulitaka aje hapa.
"Lakini alikwenda Ureno, na kutoka Ureno alikwenda Hispania. Kwa nini? Kwa sababu hakuweza kupata kibali cha kufanya kazi England. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TETESI ZA USAJILI: DE GEA KUUZWA?

 De Gea
Mustakabali wa kipa David de Gea kusalia Manchester United upo shakani baada ya wakala wake Jorge Mendes kushindwa kuwakatalia Real Madrid mpango wa kumsajili.
Manchester United inajianda kutoa ofa kwa timu ya Villarreal ili kumpata kumpata beki Gabriel Paulista, raia wa Brazil ambae yuko kwenye mazungumzo na Arsenal.
Klabu ya Chelsea iko katika mipango ya kumsajili kiungo wa Shakhtar Donetsk Douglas Costa.
Bosi wa West Brom Tony Pulis imethibitisha kuhitaji kuwasajili winga wa Wigan Callum McManaman na kiungo Darren Fletcher toka Man United katika dirisha hili la usajili.
Timu ya QPR imetoa ofa ya kumsajili mshambuliji wa zamani Ac Milan Alexandre Pato,anayechezea timu ya Sao paul kwa mkopo.
Meneja wa Swansea City Garry Monk anavutiwa na mpango wa kumsajilibeki wa kushoto wa Norwich Martin Olsson, mwenye miaka 26,pamoja na kiungo Alexandru Maxim toka Stuttgart
Kipa wa Manchester United David da Gea
Meneja wa Liverpool Brendan Rodgers anatarajia winga wake Raheem Sterling, atasaini mkataba wa muda mrefu kusalia klabu hapo siku chache zijazo. Manchester City wameulizia uwezekano wa kumpata mshambuliaji Jay Rodriguez wa timu ya Southampton.
Hull City wanamfuatilia winga wa Tottenham timu Taifa ya England Aaron Lennon,ambae anataka kuondoka White Hart Lane kwa kukosa namba kikosi cha kwanza.
Kiungo wa zamani wa Chelsea Kevin de Bruyne,amekata kurejea katika ligi ya England kwa kusema havutiwi kurudi katika ligi pamoja na kwepo taarifa za kuwaniwa na Arsenal na Manchester United.
Klabu ya Roma inajaribu kiwashawishi Chelsea kukubali pauni 380,000 ili kumchukua winga Mohamed Salah kwa mkopo mpaka mwisho wa msimu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Thursday, January 22, 2015

MAFURIKO MTWARA, NYUMBA 200 ZAZINGIRWA NA MAJI

Wakazi wa Mtaa wa Kiangu Manispaa ya Mtwara Mikindani wakipita kwenye maji  kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha mkoani humo.

Zaidi ya nyumba 200 zimezingirwa na maji katika Manispaa ya Mtwara Mikindani kufuatia mvua zinazoendelea kunyesha na kusababisha hasara kubwa ambayo thamani yake bado  haijajulikana.
Kufuatia  hali hiyo Mkuu wa Mkoa wa Mtwara, Halima Dendegu ametoa saa 24 kwa wataalam kuhakikisha wanayaondoa maji ndani ya makazi ya watu.
Mkuu wa Wilaya ya Mtwara, Wilaman Ndile amemwambia mkuu huyo wa mkoa alipotembelea maeneo yaliyoathiriwa na mafuriko hayo kuwa zaidi ya nyumba 200 zimezingirwa na maji katika mitaa mbalimbali ya manispaa hiyo.
Alisema kuwa hakuna mtu aliyeripotiwa kupoteza maisha kutokana na mafuriko hayo lakini kumetokea uharibifu mkubwa wa mali na vyakula.
 “Mvua kubwa zilizonyesha jana usiku zimeshababisha mafuriko haya…tatizo kubwa mji wetu hauna mifereji ya kupeleka maji baharini…athari ni kubwa sana,” alisema Ndile.
Aliongeza kuwa “Mitaa ya Magomeni, Chuno, Kiangu, Skoya,Kisutu Nabwada ndiyo yaliyoathiriwa zaidi na tatizo hili”
Alia Mussa ni mmoja wa waathirika wa mafuriko hayo kutoka Mtaa wa Kisutu eneo la Nabwada alisema kuwa amepoteza fedha kiasi cha Sh300,000, nguo, chakula na vyombo vya ndani.
“Tunaomba msaada kwa viongozi kunusuru hali hii, tunaona serikali yetu kama imetutupa, hatuna chakula, wala fedha za kununua chakula, kila kitu kimeloa,” alisema Mussa.
Dendegu amewaagiza wataalam wa mipango miji, zimamoto na manispaa kuhakikisha ndani ya saa 24 wanayaondoa maji hayo katika ya makazi ya watu. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MWIGULU ATII AGIZO LA KINANA, ASITISHA ZIARA ZAKE MIKOANI

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba 

Naibu Waziri wa Fedha, Mwigulu Nchemba amesitisha ziara zake za mikoani ili kutii agizo alilopewa na Katibu Mkuu wa Chama cha Mapinduzi (CCM), Abdulrahman Kinana.
Nchemba ambaye ni Naibu Katibu Mkuu wa CCM Bara, alisema jana kuwa anawajibika kutekeleza amri hiyo kutoka ndani ya chama.
Alisema agizo hilo halina lengo baya zaidi ya kukijenga chama ili kufikia malengo ikiwa ni pamoja na kuimarisha nidhamu miongoni mwa wanachama.
“Huwa ananituma, anaweza akaniambia nifanye au nisifanye jambo ambalo halina masilahi ya chama,” alisema Nchemba.
Utekelezaji huo umekuja baada ya Nchemba kuandikiwa barua na Kinana ambayo pia imezagaa katika mitandao ya kijamii ikimtaka kusitisha ziara anazozifanya maeneo mbalimbali kwa kuwa hazina baraka za chama hicho.
Katika barua hiyo iliyoandikwa Januari 18, ilieleza Nchemba amekuwa akifanya ziara nyingi katika mikoa na wilaya bila ya ushirikishwaji wa makao makuu, mikoa na wilaya na hasa kamati za siasa.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TTCL YAFILISIKA

Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk Kamugisha Kazaura
 Ofisa Mtendaji Mkuu wa TTCL, Dk Kamugisha Kazaura

KAMPUNI ya Simu Tanzania (TTCL) imetangazwa kufilisika, kutokana na kutokuwa na mtaji baada ya mwekezaji, Kampuni ya simu za mkononi ya Bharti Airtel, kushindwa kuwekeza kwa miaka 14.
Kutokana na hatua hiyo, Kamati ya Bunge ya Kudumu ya Hesabu za Serikali (PAC) imeamua kupeleka suala hilo bungeni ili kuweka mipango ya kimkakati kuifufua kampuni hiyo. Kwa kuanzia, Msajili wa Hazina amepewa kazi ya kufanya tathmini ya kina.
Hayo yalibainika jana katika kikao cha uongozi wa kampuni hiyo na kamati hiyo, inayoongozwa na Kabwe Zitto, iliyotaka kufahamu maendeleo ya kampuni hiyo, ambayo kwa miaka mingi imekuwa ikikabiliwa na changamoto kadhaa katika ushindani wa huduma za simu hususani katika siku za mkononi.
Umekuwepo pia mvutano mkali baina ya Serikali na Kampuni ya simu za mkononi ya Bharti Airtel kuhusu hatima ya asilimia 35 ya hisa, ambazo kampuni hiyo inamiliki ndani ya Kampuni ya TTCL. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

JANGA LA TATU JESHI LA POLISI


 
Jeshi la Polisi Tanzania, limekumbwa na janga la tatu katika kipindi kisichozidi miezi saba baada ya watu wanaosadikiwa kuwa majambazi kuvamia na kuua askari wake wawili katika Kituo cha Ikwiriri wilayani Rufiji juzi na kisha kupora bunduki saba na risasi 60.
Tukio hilo limefanya jumla ya askari waliouawa kufikia watano huku bunduki 22 na risasi zaidi ya 120 zikiwa zimeporwa baada ya kuvamiwa kwa vituo vitatu vya polisi tangu Juni 11 mwaka jana.
Mbali na Ikwiriri, vituo vingine vilivyovamiwa ni Mkamba Kimanzichana, Mkoa wa Pwani na Bukombe mkoani Geita.
Matukio hayo yametokea ikiwa ni mwaka mmoja na wiki tatu tangu Ernest Mangu alipoanza kazi ya Inspekta Jenerali wa Polisi (IGP) akimrithi mtangulizi wake, Said Mwema. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MAKINDA: SIWATAMBUI CHENGE NA NGELEJA...!!!


 
Spika wa Bunge, Anne Makinda akipokea kutoka kwa Balozi wa China hapa Nchini,  Dk LU Youquing baadhi ya vifaa vya Tehama vilivyotolewa na serikali ya China kwa ajili ya kusaidia shughuli za Bunge, katika hafla iliyofanyika kwenye ofisi ya spika Dar es Salaam jana. Kulia ni Kamishna wa Bunge, Dk Maua Daftari.

Spika wa Bunge, Anne Makinda amesema hawatambui wenyeviti wa kamati tatu za kudumu za Bunge ambao Bunge liliazimia wavuliwe nyadhifa zao kutokana na kutajwa katika kashfa ya Akaunti ya Tegeta Escrow.
Pamoja na kuwapo kwa maagizo ya Bunge, baadhi yao wanaendelea kujinasibu kuwa bado ni wenyeviti huku mmoja wao akiongoza vikao vya kamati.
Akizungumza Dar es Salaam jana, Makinda alisema anachofahamu ni kuwa wenyeviti hao tayari wamaeshajiuzulu na kamati zao zinatakiwa kufanya uchaguzi wa wenyeviti wengine.
Wanaotakiwa kuachia nyadhifa zao ni Victor Mwabalaswa (Nishati na Madini), Andrew Chenge (Bajeti) na William Ngeleja (Katiba, Sheria na Utawala), ambaye hadi jana mchana alikuwa akiongoza kikao cha kamati hiyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

SOMA MAGAZETI YA LEO JANUARI 22, 2015

.

.
Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WHATSAPP YAWABANA WATUMIAJI

Mtandao wa WjhatsApp 
 
Mtandao wa kijamii wa WhatsApp unawabana watu wanaotumia huduma hiyo kupitia programu bandia na ambayo haijaidhinishwa ya Android kwa muda wa saa 24.
WhatsApp ambayo inamilikiwa na Facebook, ilisema kuwa imechukua hatua dhidi ya watumiaji wa huduma ya WhatsApp Plus kwa sababu ya wasiwasi kwamba programu hiiyo huenda iksababisha kuvuja kwa taarifa za siri za watumiaji wa WhatsApp.
Programu hio bandia na isio rasmi ya Android inawezesha watumiaji wa WhatsApp Plus kupamba mawasiliano yao wanavyotaka.
Wataalamu wanasema kwamba watumiaji wa Android wanapaswa kuwa makini na kutahadhari kuhusu wanavyodownload programu flani au 'Apps'. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

WATOTO WA HOSNI MUBARAK KUACHIWA

 Aliyekuwa rais wa Misri Hosni Mubarak na wanawe Alaa na Gamal wakiwa kizimbani
 
Mahakama nchini Misri imeamrisha kuachiliwa kwa watoto wa kiume wa rais wa zamani Hosni mubarak wakati wanaposubiri kesi yao pamoja na baba yao inayohusu ufisadi.
Wakili wa Alaa na Gamal Mubarak anasema kwa anatarajia wawili hao kuachiliwa leo.
Hasira kutokana na kile kilichoonekana kama jitihada za kumuandaa Gamal Mubarak kuweza kumrithi babake kama rais ni moja ya sababu zilizosababisha maandamano makubwa yaliyomundoa madarakani rais Hosni Mubarak. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

UJUMBE WA UTURUKI SOMALIA WASHAMBULIWA

Hoteli ilioshambuliwa 
 
Kumekuwa na shambulizi la mlipuaji wa kujitolea muhanga katika hoteli moja mjini Mogadishu nchini Somali ambapo maafisa wa Uturuki walikuwa wakijiandaa kumlaki rais Recep Teyyip Erdogan.
Takriban raia watatu wa Somali waliuawa wawili kati yao wakiwa maafisa wa usalama wakati gari lililojaa vilipuzi lilipogonga lango la hoteli.
Uturuki hatahivyo imesema kuwa hakuna mjumbe wake aliyejeruhiwa na kwamba ziara ya rais Erdogan itaendelea kama ilivyopangwa siku ya ijumaa.
Kundi la wapiganaji wa Alshabaa limesema kuwa lilitekeleza shambulizi hilo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TUNISIA KUTOANA JASHO NA ZAMBIA

Afcon
 
Zambia italazimika kuimarisha safu ya kati katika mechi didi ya Tunisia kufuatia jeraha la mchezaji Nathan Sinkala ambalo limemuweka nje ya michuano yote ya mataifa ya Afrika.
Hatahivyo kikosi hicho cha Chipolopolo hakina tatizo kubwa juu wachezaji wake.
Mkufunzi wa Tunisia ana wachezaji wa kutosha wa kujumuisha katika timu yake,ijapokuwa wamekuwa na tatizo katika hoteli yao.
Kunako mwendo wa saa nane leo alfajiri ,kulikuwa na maji chungu nzima katika vyumba vya hoteli wanaolala wachezaji wa kikosi hicho.
Inadaiwa kuwa wachezaji hao walilazimika kubadili vyumba huku wachezaji wengine wakilazimika kulala wanne katika chumba kimoja. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Wednesday, January 21, 2015

KANISA KATOLIKI LAUNGA MKONO MAANDAMANO DRC

maandamanoDRC
 
Mkuu wa kanisa katoliki nchini Jamhuri ya kidemokrasi ya Congo ameunga mkono maandamano ya kupinga mabadiliko katika ya sheria ya uchaguzi ambayo imezua siku tatu za maandamano.
Kadinali laurent Monsengwo ameitaka mamlaka kwa maneno yake mwenyewe kusitisha mauaji ya raia wake. Amewataka waandamanaji kuweka amani.

Makundi ya haki za kibinaadamu yamesema kuwa zaidi ya watu 40 wamefariki katika ghasia hizo.
Vyama vya upinzani vinasema kuwa sheria hiyo iliyopendekezwa ililenga kuchelewesha uchaguzi ili rais Joseph Kabila aendelee kuwa mamlakani baada ya kipindi chake cha utawala kuisha mwaka ujao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

MWANAJESHI WA UK HATIANI KWA KUMBAKA MTOTO

Ikiwa atapatikana na hatia mwanajeshi huyo atafungwa jela miaka 10 
 
Mwanajeshi mwingereza ameshtakiwa kwa kosa la kumbaka na kumdhalilisha mtoto mwenye umri wa miaka 6 nchini Austria.
Viongozi wa mashitaka wanasema kuwa mwanajeshi huyo ambaye hajatajwa alikamatwa mwezi Novemba katika eneo la Tyrol ambako alikuwa anafanya mazoezi yake ya kijeshi.
Anatarajiwa kufikishwa mahakamani tarehe 10 mwezi Machi.
Msemaji wa kiongozi wa mashtaka alisema kua wendeshja mashtaka wanaamini kwamba mwanajeshi huyo aliingia nyumbani kwa familia ya msichana huyo akiwa mlevi nyakati za asubuhi na kufanya kitendo hicho.
Mwanajeshi huyo alipatikana katika chumba cha mtoto huyo baada ya babake kusikia kelele.
Alikamatwa mjini Neustift na ikiwa atapatikana na hatia huenda akafungwa jela miaka 10.
Msemaji wa kiongozi wa mashtaka aliambia BBC kuwa mtoto huyo alihojiwa na kiongozi wa mashitaka. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Na BBC

TAZAMA PICHA ZA SAMATTA KATIKA MAJARIBIO CSKA MOSCOW

15922_870694186307442_880608052995095050_n 
Hatimaye nyota ya mshambuliaji wa kimataifa wa Tanzania anayekipiga katika klabu ya TP Mazembe Mbwana Samatta imeanza kung’ara katika anga ya kimataifa ya soka.
Taarifa zilizothibitishwa ni kwamba mshambuliaji huyo yupo kwenye majaribio katika klabu ya CSKA Moscow – moja ya klabu kubwa kabisa nchini Urusi ambayo kwa miaka kadhaa imekuwa ikitawala soka la nchi hiyo na kucheza katika michuano ya mabingwa wa ulaya.
10690055_930864356931841_364362052221467735_n
Samatta alipewa nafasi ya kufanya majaribio ya siku 3 na klabu hiyo kwenye kambi yao ya mazoezi iliyopo Spain, lakini sasa ameongezewa wiki moja ya ziada ili maofisa ya jopo ya ufundi la timu hiyo wapate muda wa kumuangalia vizuri.
10689498_930864360265174_71847191900962169_n
Pamoja na CSKA Moscow – timu nyingine ambazo zinatajwa kumtaka mshambuliaji huyo ni Inter Milan na Udinese za Italia, Atletico Madrid ya Spain, FC Basel ya Uswis na Kaiserslauten ya Ujerumani. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

TAMBWE ASIMULIA ANAVYOTESWA, YANGA YASHITAKI

muro 2
Klabu ya Yanga imepanga leo kuwasilisha malalamiko yao juu ya tukio la kunyanyaswa kwa mshambuliaji wake Amissi Tambwe kwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) lakini pia mchezaji husika amefafanua kwa kina juu ya manyanyaso anayoyapata.
 
Akizungumza mchana wa leo katika makao makuu wa klabu hiyo Mkuu wa Kitengo cha Habari Jerry Muro amesema uongozi wao unakusudia kuwasilisha malalamiko yao hayo ambayo mengi yametokana na vitendo alivyofanyiwa Tambwe wikiendi iliyopita katika mchezo dhidi ya Ruvu Shooting ambapo wanataka mapendekezo yao manne yafanyiwe kazi.
Muro amesema kwanza Yanga ingwetaka kuona TFF inawachukulia hatua kali wahusika wote waliomdhalilisha Tambwe huku pili wakilitaka shirikisho hilo kutoa hadharani taarifa ya tathimini ya waamuzi wa mchezo huo lengo likiwa ni kujua umakini wa waamuzi hao. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
muro
“Tatu tungewaomba wenzetu wa TFF kwa kuwa wao wapo kimya pia kuwachukulia hatua wahusika wote waliosimamia mchezo huo kwa kushindwa kubaini haya ambayo vyombo vya habari imeyafichua lakini ikiwezekana wafungiwe na Yanga hatuwataki kuwaona wanachezesha mechi zetu vinginevyo tutagoma na hata Ruvu nao tungependa kuona wanapewa adhabu kwa viongozi wao kushabikia maovu haya.
Aidha Tambwe mwenyewe amechukizwa na matukio hayo akisema ameshangazwa kuona anafanyiwa vitendo vya kinyama ambapo mengine hawezi kuyaweka hadharani.
“Mpira ni starehe mimi sikatai mchezaji anikabe lakini ni jinsi gani unanikaba hapo ndiyo tatizo, naambiwa mimi mkimbizi hivi hawa wenzangu wanajua maana na haya maneno yapo mengi ambayo nimedhalilishwa nayo kiungwana siwezi kuyaweka wazi hapa lakini viongozi nitawaeleza,”alisema Tambwe. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

KLABU KUJIGHARAMIA HOTELI MICHUANO YA CAF

NGASA 
Shirikisho la Mpira wa Miguu Afrika (CAF) limefanyia marekebisho kanuni zake za michuano ya ngazi ya klabu kwa upande wa malazi ambapo sasa timu zitachagua na kujilipia zenyewe hoteli zinapokuwa kwenye mechi za ugenini. Kabla ya marekebisho ya kanuni hiyo, timu ngeni ilikuwa ikilipiwa hoteli na timu mwenyeji kwa msafara usiozidi watu 25. CAF ilikuwa imepitisha hoteli maalumu katika kila nchi ambapo mwenyeji alitakiwa kuziweka timu ngeni.
Kwa marekebisho hayo, Chama cha Mpira wa Miguu cha nchi mwenyeji kitakuwa na wajibu wa kuitafutia hoteli timu ngeni iwapo tu kitaombwa kufanya hivyo, lakini jukumu la kulipia malazi litakuwa la timu yenyewe.
Mwaka huu Tanzania inawakilishwa na timu mbili za Azam na Yanga katika michuano ya CAF. Azam inacheza Ligi ya Mabingwa (CL) ambapo itaanzia nyumbani Februari 15 mwaka huu kwa kuikaribisha El Merreikh ya Sudan kwenye Uwanja wa Azam Complex jijini Dar es Salaam.
Nayo Yanga itacheza michuano ya Kombe la Shirikisho (CC), na imepangiwa kucheza mechi ya kwanza nyumbani dhidi ya BDF IX ya Botswana. Mechi hiyo itafanyika Februari 14 mwaka huu Uwanja wa Taifa, Dar es Salaam. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.
IMETOLEWA NA SHIRIKISHO LA MPIRA WA MIGUU TANZANIA (TFF)

GERVINHO AOMBA MSAMAHA KWA KADI NYEKUNDU

Gervinho
 
Mchezaji wa Ivory Coast Gervinho ameomba msamaha baada ya kupewa kadi nyekundu kwa kumpiga mlinzi wa timu ya Guinea Naby Keita katika mechi ya timu hizo mbili ilioisha 1-1.
''Nataka kuomba msamaha kwa taifa la Ivory Coast,wachezaji wenzangu na waandalizi wa michuano ya mataifa ya Afrika kwa kitendo hiki cha hasira'',aliandika katika mtandao wake wa Twitter.
''Haikuwa mimi na vitendo kama hivyo havina nafasi katika viwanja vya soka'',,aliongezea.
Kulingana na sheria za FIFA, mchezaji hukosa mechi moja anapopewa kadi nyekundu ,lakini shirikisho la Soka barani Afrika huenda likaongeza adhabu hiyo.
Kawaida mtu hupewa marufuku ya mechi mbili katika michuano ya Afrika,lakini adhabu hiyo inaweza kuongezwa na kufikia mechi nne iwapo kamati ya nidhamu itahisi mchezaji huyo anahitaji kupewa adhabu kali. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

BUKINA FASO YAAPA KUWASHINDA WENYEJI

Afcon 
 
Nahodha wa timu ya taifa ya Burkina Fasso Charles Kabore amesisitiza kuwa wataimarisha mchezo wao baada ya kushindwa na Gabon katika mechi yao ya kwanza.
''Mashindano haya hayajakamilika kwetu sisi.''Iwapo tutashinda dhidi ya wenyeji wa maandalizi haya basi kila kitu kitakuwa shwari''.
Mkufunzi wa timu ya Equitorial Guinea Esteban Becker anajua kwamba timu yake ni sharti ishinde mchuano huo dhidi ya Burkina Fasso ilio na washambuliaji mahiri.
Hatahivyo Equitorial Guinea ni sharti iimarishe safu yake ya Ulinzi,baada ya kushindwa kuweka rekodi ya kutofungwa katika mechi zake nne katika michuano hiyo. Tangaza biashara yako hapa kwa bei nafuu zaidi, pia usisahau ku-Like Ukurasa Wetu Wa Facebook Kwa Kubofya/ Click Neno Jambo Tz.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...