Sunday, November 30, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI NOVEMBA 30, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


DSC06297

DSC06285
DSC06286 
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HONGERA DIAMOND: ATWAA TUZO 3 ZA CHANNEL O AFRIKA KUSINI

Diamond akiwa na tuzo.
MSANII Naseeb Abdul 'Diamond Platumz' ametwaa tuzo tatu za Channel O usiku wa kuamlia leo nchini Afrika Kusini. Tuzo hizo ni; Most Gifted new comer, Most Gifted Afropop na Most Gifted East kupitia wimbo wake wa Number One! Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

TAZAMA PICHA ZA AJALI YA HELIKOPTA ILIYOANGUKA JANA JIJINI DAR



Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Suleiman Kova akifafanua jambo mbele ya Vyombo vya habari katika eneo la ajali, kufuatia kutokea kwa ajali hiyo iliyopelekea vifo vya watu wanne.
 Mkuu wa Mkoa wa Dar Es Salaa,Mh.Sadick Meck Sadick akizungumza mbele ya Vyombo vya habari katika eneo la ajali, kufuatia kutokea kwa ajali hiyo iliyopelekea vifo vya watu wanne.


Baadhi ya Watu wakishuhudia mabaki ya helikopta hiyo iliyopata ajali maeneo ya Kipunguni B Moshi Bar, Ilala jijini Dar es Salaam.  Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZIARA YA KINANA MTWARA MJINI

Vijana wa Bodaboda wakiongoza msafara wa Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana wakati akiwasili Mtwara mjini ambapo alishiriki shughuli mbali mbali za kujenga na kuimarisha chama pamoja na kukagua utekelezaji wa ilani ya uchaguzi ya CCM 2010.
 Msafara wa Katibu Mkuu ukielekea Mtwara mjini.
 Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana akihutubia wakazi wa Mikindani mara baada ya kukabidhi leseni kwa madereva 70 wa boda boda waliohitimu mafunzo chini ya udhamini wa Mbunge wa Mtwara mjini Hasnain Murji.
 Wananchi wa Mikindani mkoani Mtwara wakimsikiliza Katibu Mkuu wa CCM Ndugu Abdulrahman Kinana . Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAIS KIKWETE ' NIMEPONA SARATANI'

Rais kikwete akitoa hotuba yake kwa taifa .Amesema kuwa amepona saratai ya kibofu.
  Rais Jakaya Kikwete amesema amepona saratani baada ya kufanyiwa upasuaji mapema mwezi huu nchini Marekani. Rais Kikwetemwenye umri wa miaka 64 ametoa hotuba kwa taifa kuelezea afya yake..
"Niligundulika kuwa na hatua ya pili ya saratani ya kibofu, ambayo baadaye ikaonekana kuwa ni hatua ya kwanza," alisema Kikwete katika hotuba iliyotangazwa moja kwa moja kupitia televisheni akiwa uwanja wa ndege wa Dar Es Salaam baada ya kurejea kutoka Marekani.
Aliongeza kuwa madaktari wamesema sasa hali yake shwari: "Madaktari walisema saratani haikuenea katika sehemu nyingine za mwili na baada ya upasuaji sasa wamesema nimepona saratani."
Alisema aligundulika kuwa na saratani ya kibofu zaid ya mwaka mmoja uliopita na alifanyiwa upasuaji katika hospitali ya Johns Hopkins Hospital tarehe nane Novemba.
Kikwete ambaye anamaliza muhula wake wa pili mwakani amesema wananchi wajenge tabia ya kupima afya zao ili wagundue maradhi mapema. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WALIOKUFA KWA EBOLA WATIMIA 7,000



Takwimu mpya zilizotolewa na Shirika la Afya Duniani, WHO, zinaonesha kuwa watu karibu 7,000 wamefariki hadi sasa kutokana na Ebola, karibu wote Afrika Magharibi.
Hao ni watu zaidi ya elfu moja kuliko idadi iliyotangazwa na WHO Jumatano tu.
Vifo vingi zaidi vimesajiliwa Liberia.
WHO inasema watu zaidi ya 16,000 wameugua Ebola hadi sasa.
Waandishi wa habari wanasema kuongezeka kwa idadi ya waliokufa siyo lazima inamaanisha ugonjwa unazidi kutapakaa kwa kasi kwa sababu takwimu nyengine ni za zamani. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, November 29, 2014

SWAPO YAELEKEA KUSHINDA TENA NAMIBIA

Matokeo ya mwanzo ya uchaguzi mkuu wa Namibia yanaonesha kuwa chama tawala cha SWAPO kimeshinda kwa kura nyingi.
SWAPO imetawala Namibia tangu nchi hiyo kupata uhuru mwaka wa 1990.
Lakini wanasaiasa wa upinzani kwa mara nyengine tena wanataka kura ibatilishwe, wakidai kuwa kanuni zilikiukwa na wapigaji kura waliendelea kupiga kura hata baada ya muda uliowekwa.
Mahakama makuu katika mji mkuu, Windhoek, yalitupilia mbali madai ya kuahirisha uchaguzi uliofanywa Ijumaa.
Wanasiasa wa upinzani wanasema upigaji kura wa digitali, bila ya kutumia karatasi, unatoa fursa ya kufanya udanganyifu.
Tume ya uchaguzi imekiri kuwa kulitokea matatizo kwenye mashini wakati wa kupiga kura, hata hivyo inasema matokeo yatakuwa ya kuaminika. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KESI DHIDI YA MUBARAK YATUPILIWA MBALI

Aliyekuwa rais wa Misri Hosni Mubarak. Kesi ya mauaji dhidi yake imetupiliwa mbali na mahakama moja nchini humo.
Mahakama moja nchini Misri imetupilia mbali kesi dhidi ya aliyekuwa rais wa taifa hilo Hosni Mubarak kutokana na mauaji ya mamia ya waandamanaji wakati wa maandamano ya kumng'atua mamlakani.
Aliyekuwa waziri wa maswala ya ndani wakati wa uongozi wa Mubarak ,Babib al Adly pamoja na maafisa kadhaa pia wameondolewa mashtaka.
Mubarak alihukumiwa miaka miwili iliopita lakini mahakama ya rufaa ikamuondela kifungo cha maisha gerezani.
Mahakama hiyo pia ilimuondolea rais huyo wa zamani mashtaka ya ufisadi.
Bwana Mubarak tayari anahudumia kifungo cha miaka mitatu kutokana na mashtaka ufujaji wa mali ya uma. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KOCHA WA LIVERPOOL AHOFIA HATMA YAKE

Mkufunzi wa Liverpool Brenda Rodgers asema kuwa anahofia kufutwa katika timu hiyo kutokana na matokeo mabaya 
 
Mkufunzi wa timu ya liverpool Brendan Rodgers amesema kuwa anakabiliwa na tishio la kufutwa kutokana na msururu wa matokeo mabaya ya timu hiyo.
Baada ya Liverpool kupata alama moja pekee katika mechi nne za mwisho ilizocheza,Liverpool iko katika nafasi ya 12 katika ligi ya Uingereza ,ikiwa na alama 18 nyuma ya viongozi wa ligi hiyo Chelsea.
Miezi kadhaa iliopita ,nilikuwa mkufunzi mzuri msimu huu , na sasa mimi ninakabiliwa na tishio la kufutwa'',alisema Rodgers ambaye ameorodheshwa katika nafasi ya tatu miongoni mwa wakufunzi wanaotarajiwa kushinda ligi msimu huu.
''Ni mambo ambayo makocha hukumbana nayo katika maisha ya soka'',aliongezea koch huyo.Liverpool tayari imepoteza mechi sita katika ligi msimu huu ,ikiwa ni nyingi ikilinganishwa na alama zote walizopoteza msimu uliopita.
wachezaji wa Liverpool
Lakini siku ya Jumatano waliweza kupata sare ya 2-2 dhidi ya kilabu ya Ludogorets Razgad na hivyobaisi kuimarisha matumaini ya kilabu hiyo kufuzu iwapo itaichapa Fc Basel katika michuano ya muondoano ya taji la kilabu bingwa barani Ulaya.
''Kitu ambacho mtu hutakiwa kufanya ni kuendelea kujaribu kutafuta matokjeo mazuri''.,alisema Rodgers.
Kocha huyo wa zamani wa kilabu ya Swansea pia amemtetea kipa Simon Mignolet aliyeshtumiwa na mlinda lango wa zamani wa kilabu hiyo Bruce Grobbelaar. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HENRY ATAKA KUISAIDIA ARSENAL

Thiery Henry
Uwezekano wa Thiery Henry kujiunga na Arsenal kama mkufunzi umeongezeka baada ya mchezaji huyo wa Ufaransa kufichua kwamba bado ana ndoto ya kuisadia Arsenal kushinda taji la kilabu bingwa barani Ulaya.
Henry huenda akaweka viatu vyake vya soka chini jumamosi wakati ambapo kilabu yake ya New York Red Bulls itajaribu kulipiza kichapo cha mabao 2-1 ugenini katika fainal ya raundi ya pili dhidi ya New England Revolution.
Mchezaji huyo mwenye miaka 37 amekamilisha kandarasi yake na kilabu hiyo na ijapokuwa anasema kuwa hakuna kilichoafikiwa kuhusu hatma yake ameanza kutoa maoni yake kuhusu maisha yake baada ya kusakata soka.
Arsene Wenger
Na baada ya kocha Arsene Wenger kumfungulia milango mchezaji huyo ,Henry amesema kuwa angependelea kuisaidia kilabu yake ya zamani.
''hakuna kilicho wazi''Henry aliliambia gazeti la L'Equipe.''Sijafanya uamuzi wowote na mimi sipendelei uvumi'',.
''Kitu kimoja kilicho wazi ni kwamba nitasalia katika soka kama mkufunzi ama afisa mkuu ,lakini tutaona'',alisema Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Friday, November 28, 2014

ASKOFU KILAINI, NZIGIRWA WAZUNGUMZIA TUHUMA YA ESCROW

Baba Askofu Methodius Kilaini  

Askofu Msaidizi wa Jimbo la Bukoba, Methodius Kilaini amekiri kupokea Sh80.5 milioni kutoka kwa Mkurugenzi wa VIP Engeering, James Rugemalira akisema si mara yake kwa kwanza kupokea fedha kutoka kwa mfanyabiashara huyo kwa kuwa mara nyingi huwa anachangia kwa uwazi miradi ya jamii.
Askofu huyo alikuwa akizungumzia Ripoti ya Kamati ya Bunge ya Hesabu za Serikali (PAC), iliyosomwa bungeni juzi ikimtaja kuwa ni miongoni mwa viongozi wa dini na watu wengine waliopokea mabilioni kutoka katika akaunti ya escrow.
Katika ripoti hiyo, Zitto aliwataja viongozi wengine wa dini walioingiziwa fedha katika Benki ya Mkombozi inayomilikiwa na Kanisa Katoliki kuwa ni Askofu Eusebius Nzigirwa (Sh40.4 milioni) na Padri Alphonce Twimanye Simon (Sh40.4 milioni). Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ESCROW NJIAPANDA, WABUNGE WAGAWANYIKA...!!!




Mbunge wa Viti Maalumu, Mariam Msangi (katikati)  akiwasihi Mbunge wa Kasulu Mjini, Moses Machali (kushoto) na Mbunge wa  Nkasi, Ali Kessy wasigombane kwenye Viwanja vya Bunge, mjini Dodoma jana.

Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo jana alipangua hoja zilizotolewa na Kamati ya Hesabu za Serikali (PAC), kuhusu ufisadi uliofanyika katika Akaunti ya Tegeta Escrow na kuacha wananchi njia panda kwa kutokuelewa nani anasema ukweli kati yake na kamati hiyo, inayoongozwa na Zitto Kabwe.

Juzi, kamati hiyo ya Zitto iliwasilisha ripoti yake kuwa imethibitisha kuwa Profesa Muhongo amekuwa mara kwa mara akilipotosha Bunge na Taifa kwa ujumla kwamba ndani ya fedha hizo hakukuwa na fedha za umma.

Kamati hiyo ilieleza kuwa imebaini kuwa Profesa Muhongo ndiye aliyekuwa dalali mkuu aliyewakutanisha Singh Sethi na James Rugemalira tena katika ofisi ya umma na pengine hilo ndilo lilikuwa sababu ya upotoshaji.

Akiwasilisha taarifa ya Serikali kuhusu hoja hiyo, Profesa Muhongo alianza kupangua hoja moja baada ya nyingine ingawa katika mjadala wa baadaye, zilihojiwa na wachangiaji wengine waliohoji uhalali wa vielelezo alivyotoa. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO IJUMAA NOVEMBA 28, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
;
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

IKULU YAHUSISHWA NA ESCROW

Ikulu ya rais nchini Tanzania 
 
Bunge la Tanzania hapo jana liliambiwa kwamba afisa mmoja wa ikulu ya rais bwana Prosper Mbena aliandika barua ili kushinikiza hatua ya kutolewa kwa billioni 306 fedha za Escrow kutoka banki kuu ya Tanzania.
Bwana Mbena ambaye anafanya kazi kama katibu katika afisi ya rais aliandika barua mwaka uliopita akiiagiza wizara ya fedha kuzitoa fedha hizo kama ilivyoamrishwa na mwanasheria mkuu.
Kushirikishwa kwa ikulu ya ya rais kulizuka baada ya wabunge kujadili ripoti kuhusu kashfa hiyo ambayo imeikumba serikali ya Tanzania katika miezi kadhaa iliopita.
Kiongozi wa upinzani katika bunge,Bwana Freeman Mbowe pamoja na kinara wa bunge upande wa upinzani bwana Tandu Lissu alifichua jukumu lililochukuliwa na afisa huyo wa ikulu kushinikiza madai kwamba baadhi ya maafisa wakuu serikalini walihusika katika utoaji wa mabilioni hayo ya fedha.
Ripoti hiyo imesema kuwa fedha hizo za Escrow ni za walipa ushuru wa Tanzania na kwamba zilitolewa kwa njia ya ufisadi na kugawanywa miongoni mwa watu maarufu.

WANAUME 13 WASHTAKIWA KWA UDHALILISHAJI

Genge la Wanaume waliotekeleza vitendo vya udhalilishaji dhidi ya Wasichana 
 
Wanaume kumi na watatu wameshtakiwa kwa kujihusisha na vitendo vya udhalilishaji kwa Watoto mjini Bristol, ikiwemo vitendo vya ubakaji na kuwalazimisha watoto wa kike kujiingiza kwenye vitendo vya biashara ya ngono.
Mahakama ya mjini Bristol ilimsikiliza binti wa miaka 16 aliyebakwa na Wanaume watano raia wa kisomali.
Halikadhalika mdogo wake mwenye umri wa miaka 14 alibakwa na mmoja wa wanaume hao, Msichana huyo alipofika kumtembelea Dada yake.
Uchunguzi uliofanywa na Polisi ulibaini kuwa genge jingine la wanaume wenye asili ya kisomali liliwadhalilisha kijinsia wasichana wengine wanne.
Wasichana hao walilipwa pauni 30,au kupewa dawa za kulevya, vilevi na zawadi kwa ajili ya kushiriki vitendo vya ngono na wanaume wenye umri mkubwa wa jamii ya kisomali.
Miongoni mwa walioshtakiwa ,Watu sita walihukumiwa kifungo,wengine saba walitiwa hatiani siku ya jumatano. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Na BBC

WAFANYABIASHARA WA UGANDA WAIONYA KENYA

Wafanyibiashara wa Uganda wameonya kuihama bandari ya Mombasa kutokana na ada mpya za mara kwa mara. 
 
Wafanyibiashara wa Uganda chini ya muungano wa Wanabiashara wa mji wa Kampala Uganda KACITA wamelipa Shirika la ukusanyaji Ushuru nchini kenya KRA wiki mbili kuitoa mizingo yote inayoelekea Uganda la sivyo waigomee bandari ya Mombasa.
Ilani hiyo iliafikiwa siku ya Alhamisi baada ya saa kadhaa za majadiliano kuhusu athari za hatua ya KRA ya kutoza kodi bidhaa zote zinazoingia katika badari hiyo.
Awali ,wafanyibiashara walikuwa wakilipa ada wanayotozwa wakati wanapochukua mizigo yao pamoja na ada nyenginezo.
Hatua hiyo kulingana na KACITA si kinyume na matarajio ya jumuiya ya Afrika mashariki pekee bali pia inawaumiza wafanyibiashara wa Uganda pamoja na uchumi.
Mwenyekiti wa KACITA Everest kayondo amesema kuwa kufikia jumatano kulikuwa na makasha 4,000 yanayozuiliwa katika Bandari ya Mombasa kutokana na ada za mara kwa mara zinazotolewa na KRA.
''Kwa hivyo tunaipa KRA wiki mbili kutoa mizigo yote ya Uganda la sivyo tuhame hadi katika bandari ya Dar es Salaam'',.aliongezea
Wafanyibiashara hao pia walikubaliana kwamba iwapo mahitaji yao hayataafikiwa ,wataishinikiza serikali ya Uganda kuzuia bidhaa za kenya zinazoingia katika soko la Uganda. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PHILIP HUGHES AFARIKI DUNIA

Philip Hughes
Bendera zinapepea nusu mlingoti katika viwanja vya cricket nchini Australia katika kuomboleza kifo cha mcheza crickte Philip Hughes aliyefariki hapo jana baada ya kupigwa na mpira. Salaam za rambi rambi zimeendelea kutolewa kutoka sehemu mbali mbali duniani. Baadhi ya wachazaji wa cricket wamekuwa wakiacha magongo ya mchezo huo katika mlangoni mwa nyumba zao kama ishara ya kuomboleza kifo hicho. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Wednesday, November 26, 2014

UKAWA WASAMBARATIKA SERENGETI


Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) Wilaya ya Serengeti, Mkoa wa Mara, umesambaratika baada ya Chadema kuamua kusimamisha wagombea vitongoji na vijiji vyote ikiwa ni kinyume na makubaliano ya vyama hivyo.

Novemba 4, viongozi wakuu wa vyama vya Nation League for Democracy (NLD), NCCR Mageuzi, CUF na Chadema walitiliana saini ushirikiano wa kusimamisha mgombea mmoja kila ngazi ya uchaguzi kuanzia serikali za mitaa, vijiji na vitongoji. Kusambaratika kwa umoja huo kulitokana na viongozi wa vyama vya CUF, NCCR Mageuzi na Chadema kukaa vikao vitatu kupanga jinsi ya kuachiana vijiji, vitongoji na mitaa kushindikana kufuatia viongozi wa Chadema kuvitaka vyama vingine kuwaachia vitongoji 24 vya Mamlaka ya Mji Mdogo Mugumu. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

HALIMA MDEE AMKANA MKONO


Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee. PICHA|MAKTABA 

Siku moja baada ya Mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono kusema amelishwa sumu akiwa London, Uingereza, Mbunge wa Kawe (Chadema), Halima Mdee amemtaka kusema ukweli na si kulihadaa Taifa kwa uongo.

Mkono akizungumza na waandishi wa habari juzi kuelezea mwenendo wa afya yake, alisema lengo la kulishwa sumu ilikuwa ni kutaka kuharibu figo zake ndani ya saa 72 kitendo kilichoshindikana.

Mdee aliyekuwa na Mkono katika ziara hiyo alisema: “Hakuna ukweli wowote kwamba alilishwa sumu, nilikuwa naye kule na mazingira aliyoanza kuumwa hadi kupona kwake ni utata... awaeleze Watanzania anaumwa nini na si kusema alilishwa sumu.

“Nilikaa kimya baada ya kuripotiwa na gazeti moja (The Citizen) kwamba Mkono kalishwa sumu, sasa amezungumza tena nikaona si busara kukaa kimya wakati alilidanganya Taifa. Mkono waeleze ukweli watu mbona unawadanganya.” Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATANO NOVEMBA 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MKOSAMALI APANDISHWA KIZIMBANI

Mbunge wa Jimbo la Muhambwe mkoani Kigoma, Felix Mkosamali. PICHA|MAKTABA 

Mbunge wa Jimbo la Muhambwe mkoani Kigoma, Felix Mkosamali amefikishwa katika Mahakama ya Wilaya ya Kibondo akikabiliwa na shtaka la kumzuia karani mwandikishaji kufanya kazi yake.
Mwendesha Mashtaka wa Polisi, Peter Makala alidai jana mahakamani hapo kuwa mbunge huyo alitenda kosa hilo juzi, baada ya kufika Kituo cha Kitongoji cha Nduta, Kijiji cha Kumhasha, Kata ya Murungu, wilayani Kibondo na kumzuia karani kuendelea kuandikisha wakazi kwa ajili ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Makala alidai kuwa kitendo cha kumzuia karani huyo kuendelea kufanya kazi yake ni kinyume na ukiukwaji wa Sheria ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.
Pia, alidai kuwa kitendo cha kuwazuia wakazi hao kujiandikisha ni kuwanyima haki yao ya msingi, kwani baada ya kuzuiwa waliendelea kudai kutaka kujiandikisha lakini mshtakiwa hakusikiliza kilio chao.
Mshtakiwa alikana shtaka na Hakimu Erick Marley alisema dhamana iko wazi kwa mdhamini kusaini bondi ya Sh4 milioni. Mbunge huyo alitimiza masharti na kesi hiyo imeahirishwa hadi Desemba 29.
Mkosamali alikamatwa juzi jioni baada ya kudaiwa kumnyang’nya karani vitabu na madodoso na kuyapeleka ofisi ya Mkurugenzi wa Halmashauri ya Wilaya ya Kibondo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BOKO HARAM WAFANYA MAUAJI TENA

Shambulio la bomu lililofanywa kariibu na soko.
 
Watu 78 wameuawa katika mashambulio mawili ya kujitoa mhanga yaliyofanywa sokoni, katika mji wa Maiduguri kaskazini mwa Nigeria.
Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema mlipuko wa kwanza ulitokea wakati washambuliaji hao walipomuwekea mlipuko mwanamke mmoja mwenye matatizo ya akili.
Wakati umati wa watu wakienda kutoa msaada, mwanamke mwingine alijitoa mhanga.
Kundi la kiislamu la wapiganaji la Boko Haram ambalo linadhibiti maeneo mengine ya miji ya kaskazini mwa nchi hiyo na vijiji, linadhaniwa kuhusika na shambulio hilo.
Mwandishi wa BBC anasema Wanaigeria wamekosa Imani na jaribio la serikali ya nchi yao kufanya mazungumzo na Boko Haram, kutokana an kuongezeka kwa ghasia hizo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ZAIDI YA WATU 60 WAUAWA SYRIA

Majeshi ya Syria yafanya mashambulizi.
 
Zaidi ya watu 60 wameuwawa, katika mashambulio kadhaa ya angani yaliyofanywa na Jeshi la serikali ya Syria.
Raia wengi waliuwawa katika mashambulio tisa yaliyolenga ngome kuu za kundi la wapiganaji wa Islamic State.
Wakereketwa wameiambia BBC kuwa Hospitali kuu ya Raqqa imesalia bila huduma kwani HAKUNA chakula na umeme. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

KLABU BINGWA BARANI ULAYA

 Timu ya Chelsea 
 
Usiku wa kuamkia leo kindumbwe ndumbwe cha michuano ya Klabu Bigwa barani Ulaya kiliendelea na kushuhudia Chelsea ikitoa kipigo cha mbwa mwizi mbele ya mashabiki wa Schalke 04 ya Ujuremani pale ilipoishindilia magoli 5 bila majibu.
Manchester City ya England nao wakawabamiza wababe wengine wa Ujerumani Bayern Munich kwa kwa kuwafunga magoli 3 - 2 na kufufua matumaini ya kusonga mbele katika michuano hiyo huku magoli yote matatu ya Man City yakitiwa kimiani Sergio Aguero.
Katika mechi nyingine Paris St. Germain ya Ufaransa waliwashikisha adabu Ajax ya Uholanzi kwa kuifunga magoli 3 - 1 huku Becelona kwa upande mwingine wakiisasambua Apoel Nicosia ya Syprus kwa kuishushia kichapo cha magoli 4 kwa yai.
CSKA Moscow ya Urusi na AC Roma zikatoka suluhu ya goli moja 1 - 1
Burudani hiyo itaendelea leo ambapo Liverpool ya England baada ya kufanya vibaya katika mechi zilizotangulia leo wanajaribu bahati yao wakiwa ugenini dhidi Ludogorets ya Bulgaria.
Arsenal nao watawakaribisha Borusia Dortmud ya Ujerumani huku vita vingine vikiwa ni kati ya FC Basel ya Uswis watakaopopepetana na Real Madrid. Malmo FF ya Sweden watakuwa wenyeji wa Juventus ya Italia. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Tuesday, November 25, 2014

MKONO ASIMULIA ALIVOLISHWA SUMU LONDON


Mbunge wa Musoma Vijijini, Nimrod Mkono akisisitiza jambo alipokuwa akizungumza kwenye mkutano na waandishi wa habari uliofanyika ofisini kwake jijini Dar es Salaam jana.

Mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono ambaye hivi karibuni alinusurika kifo akidaiwa kulishwa sumu akiwa London, Uingereza amesimulia jinsi tukio hilo lilivyomkuta.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Mkono alisema endapo uchunguzi wa suala hilo utakamilika na kuthibitisha kwamba alilishwa sumu, atapambana na wahusika kwa kuwa wamehatarisha maisha yake.
Mkono ambaye pia ni wakili maarufu nchini, alitoa kauli hizo jijini hapa jana, alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuelezea mwenendo wa afya yake.
Alidai kwamba, lengo la kumlisha sumu ni kuharibu figo zake ndani ya saa 72 wakati alipokuwa katika ziara ya nchini humo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ULINZI MKALI MDAHARO WA JAJI WARIOBA LEO




Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba. PICHA|MAKTABA 


Kamanda wa Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam, Kamishna Suleiman Kova amesema ulinzi utaimarishwa kabla, wakati na baada ya mdahalo maalumu wa Katiba ulioandaliwa na Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), kwenye Ukumbi wa Mlimani City, Dar es Salaam mzungumzaji mkuu akiwa Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.

Hatua ya Kova imekuja baada ya kuibuka kwa vurugu zilizosababisha kuvunjika mdahalo wa kwanza uliofanyika Novemba 2, kwenye Hoteli ya Blue Pearl Ubungo, Dar es Salaam. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE NOVEMBA 25, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

RAIS KIKWETE KUREJEA JUMAMOSI

Rais Jakaya Kikwete. PICHA|MAKTABA

Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kurejea nchini Jumamosi, Novemba 29 baada ya taratibu za matibabu yake nchini Marekani kukamilika.
Taarifa ya Kurugenzi ya Mawasiliano ya Rais, Ikulu ilisema jana kuwa taratibu hizo zilikamilika saa 12 asubuhi jana, baada ya madaktari bingwa katika Hospitali ya Johns Hopkins kumfanyia hatua ya mwisho ya tiba.
Hata hivyo, Rais Kikwete ataendelea kupumzika na kuangaliwa kwenye Hoteli Maalumu inayohusiana na Hospitali ya Johns Hopkins kwa siku mbili hadi tatu kabla ya kuanza safari ya kurejea nyumbani.
Rais Kikwete aliondoka nchini Alhamisi ya Novemba 6, 2014, kwenda kufanyiwa uchunguzi wa afya yake lakini madaktari katika Hospitali ya Johns Hopkins waliamua kumfanyia upasuaji wa tezi dume Jumamosi ya Novemba 8, 2014.
Taarifa hiyo ilisema Rais Kikwete anaendelea kuwashukuru Watanzania kwa sala na maombi yao ya kumtakia heri ya kupona haraka na kurejesha afya njema katika kipindi chote cha ugonjwa wake. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JENGO LAANGUKA, KUMI WAFA

 Vikosi vya uokoaji vikitafuta Watu walionasa kwenye kifusi cha Jengo
 
Watu kumi wamepoteza maisha baada ya jengo la ghorofa kuanguka mjini Cairo nchini Misri, maafisa wameeleza.
Watu saba wamejeruhiwa baada ya jengo la ghorofa nane kuanguka usiku.
Mkuu wa Idara ya dharula Jenerali Mamdouh Abdul Qader amesema vikosi vya uaokoaji vinawasaka Watu 15 wanaokisiwa kunasa kwenye kifusi.
Mara kadhaa majengo yameanguka nchini humo, sababu kubwa ikiwa ujenzi usiofuata kanuni na Sheria pia usimamizi mbovu wa taratibu za ujenzi.
Jenerali Qader ameliambia shirika la Habari la Ufaransa kuwa hawajui chanzo cha ajali hiyo,lakini walipatiwa taarifa kuwa ghorofa mbili za juu zilijengwa kinyume cha sheria.
Wakazi wa majengo ya karibu na lilipoanguka jengo hilo wameondoka katika makazi yao kwa nia ya kujihadhari.
Mwezi Januari Mwaka jana,Watu 28 walipoteza maisha baada ya jengo la ghorofa nane kuanguka mjini Alexandria. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

WAANDAMANAJI WAFANYA VURUGU ST. LUIS

Polisi wakirusha gesi za kutoa machozi dhidi ya Waandamanaji St Louis 
 
Mji wa St Louis limeshuhudia maandamano na vitendo vya uporaji baada ya jaji kupitisha uamuzi wa kumshtaki aliyemuua kijana mweusi Michael Brown.
Polisi mjini humo wamesema vurugu zimeleta madhara makubwa zaidi kuliko ya mwezi Agosti baada ya kuuawa kwa kijana huyo.
Kamanda wa Polisi wa St Louis, Jon Belmar amesema alisikia milio ya risasi takriban 150 kutoka kwenye makundi ya watu.
Brown alifyatuliwa risasi na Polisi tarehe 9 Mwezi Agosti, hali iliyoibua ghadhabu na maandamano.
Watu wengi wa jamii ya Afrika na Marekani walitoa wito wakitaka Afisa Polisi Darren Wilson ashtakiwe kwa mauaji.
Rais wa Marekani Barack Obama alitoa wito kwa wamarekani kuwa watulivu na kukubali maamuzi ya Jaji kuhusu kesi hiyo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, November 24, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATATU NOVEMBA 24, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS


.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MDAHALO WA JAJI WARIOBA KESHO DAR

Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.PICHA|MAKTABA 
Taasisi ya Mwalimu Nyerere (MNF), imeandaa mdahalo maalumu wa Katiba utakaofanyika kesho kwenye Ukumbi wa Mlimani City ambao mzungumzaji mkuu atakuwa Mwenyekiti wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba.
Mwenyekiti wa taasisi hiyo, Joseph Butiku alisema jana kwamba mdahalo huo wa amani ni kwa ajili ya Watanzania wenye mapenzi mema na utakuwa wa wazi, ikiwa ni sehemu ya kuziba pengo la mdahalo wa Katiba uliovunjika Novemba 2 ambao ulifanyika kwenye Hoteli ya Blue Pearl.
Ulivunjika baada ya kutokea vurugu zinazodaiwa kuanzishwa na kikundi cha watu kwa lengo la kuvuruga uwasilishwaji wa ujumbe wa Katiba, huku Katibu wa Uhamasishaji wa UVCCM, Paul Makonda akitajwa kinara wa vurugu hizo. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BUNDUKI BANDI YAMLETEA MAAFA

Kijana Tamir Rice alipigwa risasi mbili baada ya kupatikana na kilichobainika kuwa bunduki bandi. 
 
Wakili anayewakilisha familia ya kijana mweusi mwenye umri wa miaka kumi na mbili aliyepigwa risasi na polisi katika mji wa Cleveland nchini Marekani, amesema familia yake itafanya uchunguzi wake sambamba na ule unaofanywa na Polisi kubaini kilichotokea.
Kijana huyo kwa jina Tamir Rice mwenye umri wa miaka 12 alikuwa amebeba kile kilichoonekana kuwa bunduki bandia. Polisi wanadai kuwa kijana huyo alikataa kutii amri alipoambaiwa asalimu amri.
Kifaa walichokuwa nacho polisi ndicho kilibaini kuwa bunduki hiyo ilikuwa bandia.
Inaarifiwa kijana huyo alipigwa risasi mara mbili baada ya kuitoa bunduki yake kiunoni mwake lakini hakujaribu hata wakati mmoja kuielekeza kwa poliso wala kujribu kuifyatua.
Wakili wa familia hiyo amesema kuwa ikiwa watapata kuwa haki za kijana huyo zilikiukwa, familia yake itachukua hatua za kisheria dhidi ya polisi.
Mwanasiasa mmoja anapendekeza sheria ambayo itahakikisha kuwa bunduki bandia zinakuwa na rangi unayong'aa zaidi ili ziweze kutambulika haraka. Asante kwa kutembelea blog hii na endelea kuwa nasi siku zote, kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...