Sunday, September 28, 2014

TAZAMA FILAMU YA YESU KWA LUGHA YA KINYAKYUSA.....!!!


 

Fanya siku yako kuwa nzuri kwa kutazama filamu ya Yesu kwa lugha ya kinyakyusa. Share na wenzio waione. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

POLISI MORO WAFICHUA SIRI YA KUINYAMAZISHA SIMBA SC


s13

Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
NAHODHA wa Polisi Morogoro Nicholas Kabipe amefichua siri ya kupata sare ya 1-1 dhidi ya Simba katika mchezo wa raundi ya pili ya ligi kuu soka Tanzania bara iliopigwa jana uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Simba walikuwa kwa kwanza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 32 kipindi cha kwanza kupitia kwa Emmanuel Okwi, lakini Danny David Mrwanda aliisawazishia Polisi katika dakika ya 50 kipindi cha pili.
Kabla ya mechi ya jana, Polisi walifungwa 3-1 na Azam fc katika mechi ya ufunguzi iliyochezwa wikiendi ya septamba 20 mwaka huu uwanja wa Azam Complex, Chamazi.
Baada ya mechi ya jana dhidi ya Simba, Kabipe alisema: “Kwa matokeo haya sisi tumefurahi kwasababu tulipoteza mchezo wa kwanza. Kuna makosa yalikuwa yanatugharimu na Azam wakatufunga magoli matatu.
“Tumerekebisha hayo makosa na tumeweza kupata sare. Wakati wa mapumziko tukiwa nyuma kwa goli moja kwa bila, mwalimu alituelekeza kuwa Simba wana kasi sana sehemu ya kiungo”.
“Kwahiyo akasema tunatakiwa tuwe wengi katikati ili tusiwape nafasi ya kucheza, tuwe tunaenda kukaba watu watatu na tulifanya hivyo, ikawezekana na tukaweza kupata sare hiyo”. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMAPILI SEPTEMBA 28, 2014 YA DINI, MICHEZO NA HARD NEWS


.

.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

ARSENAL YAPONEA CHUPUCHUPU EMIRATES….OXLADE-CHAMBERLAIN AOKOA JAHAZI

1411841753978_wps_25_Arsenals_English_striker_
Mshambuliaji wa Arsenal, Alex Oxlade-Chamberlain (kushoto) alifunga goli la kusawazisha dhidi ya Tottenham
MASHABIKI wa Emirates walishangilia kwa matarajio ya kushinda mechi ya watani wa jadi wa kaskazini mwa London baina ya Arsenal na Tottenham, lakini wametoka sare ya 1-1.
Arsenal walitawala mchezo na kushambuli zaidi, lakini hawakuweza kupata magoli.
Tottenham walikuwa wa kwanza kuandika bao la kuongoza katika dakika ya 56 kupitia kwa Nacer Chadli, lakini Alex Oxlade-Chamberlain aliisawazishia Arsenal mnamo dakika ya 74.
Arsenal's Alex Oxlade-Chamberlain celebrates scoring the equaliser against Tottenham at the Emirates
Alex Oxlade-Chamberlain akishangilia goli lake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAANDAMANO YA KUMPINGA KABILA YAFANYIKA

Rais Joseph Kabila
Maelfu ya watu wameandamana nchini Jamhuri ya kidemorasi ya Congo wakimpinga rais wa taifa hilo Joseph Kabila.
Wafuasi wa upinzani wanataka rais Kabila kuondoka madarakani wakati muhula wake wa pili wa uongozi utakapomilika mnamo mwaka 2016.
Kuna shaka kuwa huenda katiba ikabatilishwa ili kumruhusu kuwania muhula wa tatu.
Maandamano kwenye mji mkuu Kinshasa yaliripotiwa kuwa ya amani lakini polisi walitumia vitoa machozi kuwatawanya waandamanaji kwenye mji wa Goma ulio mashariki mwa nchi hiyo.
Rais Joseph Kabila alichukua mamlaka mwaka 2001 kufuatia kuuawa kwa babake Laurent Kabila. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

SALVA KIIR ATAKA KUSITISHWA KWA VITA

Rais Salva Kiir na Riek Machar wakibadilishana makubaliano ya kusitisha vita
Rais wa Sudan Kusini Salva Kiir amesema kuwa serikali yake imejitolea kumaliza vita nchini nchini humo.
Akiongea kwenye mkutano mkuu wa baraza la umoja wa mataifa mjini New York Kiir ameitaka jamii ya kimataifa kuwashinikiza waasi kuheshimu makubaliano ya kusitisha vita.
Vita vya kisiasa nchini Sudan Kusini kati ya rais Kiir na makamu wake wa zamani Riek Machar vimesababisha vifo vya maelfu ya watu na kuwalazimu mamalioni ya wengine kuhama makwao.
Mzozo ulianza mwezi Disemba mwaka uliopita na makubaliano ya kumaliza vita yameshindwa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

BAHATI MBAYA SIMBA, YANGA HAWAGUSI CHAMAZI…NGOMA INGEKUWA TAMU SANA

azam web_3
UWANJA wa Azam Complex unaomilikiwa na mabingwa watetezi wa ligi kuu soka Tanzania bara, Azam fc umezidi kuwa mgumu kwa timu za ligi kuu.
Timu pinzani zinapofika maeneo ya Chamazi zinaanza kupata harufu ya kipigo kutoka kwa wenyeji wao.
Chamazi si sehemu salama kwa timu za ligi kuu isipokuwa kwa Simba na Yanga ambao hawajawahi kucheza katika uwanja huo.
Azam fc wakiendelea kuutumia vyema uwanja wao wa nyumbani, jana walishinda mabao 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting ya Mkoani Pwani.
Kabla ya mechi hii, niliandika kupitia mtandao huu nikisema Azam fc wataifunga Ruvu Shooting kwasababu mazingira ya Chamazi ni rafiki kwao na wana kikosi kilichojaa. Nilisema sio rahisi kuifunga Azam katika uwanja wake, hata rekodi zinaonesha hivyo.
Azam walikwenda kupumzika wakiwa mbele kwa bao 1-0 liliofungwa na Mrundi, Didier Kavumnagu katika dakika ya 40. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

YANGA ‘WAKITAITIWA’ SAFU YA KIUNGO..JAJA ATAISHIA KUZUNGUKA TU!

Jaja akipambana

Jaja alishindwa kufunga dhidi ya Mtibwa na kwa bahati mbaya alikosa mkwaju wa penalti
Na Baraka Mpenja, Dar es salaam
0712461976
YANGA SC wakiwa na kumbukumbu mbaya ya kufungwa 2-0 katika mechi ya ufunguzi wa ligi kuu soka Tanzania bara, septemba 20 mwaka huu uwanja wa Jamhuri Morogoro dhidi ya Mtibwa Sugar, leo jioni wanaikaribisha Tanzania Prisons katika mtanange wa raundi ya pili uwanja wa Taifa, Dar es salaam.
Prisons wanaingia katika mechi hiyo wakiwa na kumbukumbu ya ushindi wa 2-0 dhidi ya Ruvu Shooting waliopata katika mechi ya ufunguzi iliyopigwa wikiendi ya septemba 20 mwaka huu uwanja wa Mabatini, Mlandizi, mkoani Pwani. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, September 27, 2014

UKAWA WASEMA JK, CCM HAWAELEWEKI



 
Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) umesema kuwa Rais Jakaya Kikwete na CCM hawaeleweki ukidai ni kutokana na kukiuka makubaliano yao kuhusu kuendelea kwa Bunge Maalumu la Katiba mjini Dodoma.

Umoja huo pia umedai kwamba Mahakama Kuu ya Tanzania imeshindwa kutoa uamuzi fasaha kuhusu tafsiri ya kisheria ya mamlaka ya Bunge hilo katika kurekebisha Rasimu ya Katiba kwa kuogopa lawama kutoka Ukawa na CCM.

Ukawa unaoundwa na vyama vya Chadema, CUF, DP, NLD na NCCR-Mageuzi ulieleza hayo jijini hapa jana ulipozungumzia Mchakato wa Katiba ulipofikia, hasa baada ya Bunge hilo kufanya marekebisho ya kanuni kwa wajumbe wake kuruhusiwa kupiga kura kwa njia ya mtandao.

Mwenyekiti mwenza wa Ukawa ambaye pia ni Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe alisema kuwa makubaliano ya kusitishwa kwa Bunge hilo kati yao na Rais Kikwete yameshindwa kutekelezwa, jambo ambalo wanashindwa kuelewa sababu zake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

JAJI WARIOBA AWAPANIA WAJUMBE WA KATIBA

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Mstaafu Joseph Warioba akizungumza wakati wa Maadhimisho ya Miaka 19 ya Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC), Dar es Salaam jana.

Aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba amesema Rasimu ya Katiba iliyopendekezwa na Kamati ya Uandishi ya Bunge Maalumu la Katiba imeondoa mambo manne muhimu yaliyokuwa kiini cha kupata Katiba ya mageuzi.
Akiyataja mambo hayo muhimu ambayo ni maadili ya viongozi wa umma,  madaraka ya wananchi, mgawanyo wa madaraka na muungano. “Tutakutana mtaani. Tume tutaendelea kutetea rasimu yetu na wao wawaeleze wananchi kwa nini wameondoa maoni yao yaliyokuwa katika Rasimu ya Pili ya Katiba,” aliongeza kwa ufafanuzi Jaji Warioba.
Akizungumza katika maadhimisho ya miaka 19 tangu kuanzishwa kwa Kituo cha Sheria na Haki za Binadamu (LHRC) Dar es Salaam jana, Jaji Warioba alisema rasimu hiyo inatofautiana kwa kiasi kikubwa na rasimu iliyotolewa na tume hiyo Desemba mwaka jana.
“Sina hakika kama tutapata Katiba Mpya labda Katiba iliyoboreshwa. Rasimu au Katiba itakayopendekezwa na Bunge Maalumu haitapigiwa kura hadi 2016. Sina hakika kama kura hiyo itapigwa kwa kuwa hakuna maridhiano hasa kuhusu muungano,  rasimu hiyo itaanza kupingwa tangu siku ya kutolewa kwake,” alisema. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...