Saturday, April 26, 2014

MIAKA 50 YA MUUNGANO WA TANGANYIKA NA ZANZIBAR

IMG-20140426-WA0034_af1cd.jpg
IMG-20140426-WA0035_686a4.jpg
Umati wa watu waliohudhuria maadhimisho ya miaka 50 ya Muungano wa Tanganyika na Zanzibar yanayoendelea hivi sasa katika uwanja wa Uhuru jijini Dar es Salaam, maonyesho haya yanajumuisha shughuli mbalimbali zikiwemo maonyesho. Maadhimisho haya yamehudhuriwa na viongozi mbalimbali kutoaka mataifa mbalimbali (Picha na Awadhi Ibrahim)

G7 YAZIDI KUIBANA URUSI...!!!

Askari wa Ukraine
Viongozi wa nchi Saba tajiri kwa viwanda duniani G7 wamekubaliana kuongeza vikwazo zaidi kwa Urusi ambapo wamesema imezidi kuifanya Ukraine isitawalike.
Ikulu ya White House ya Marekani imesema wataanza kuweka vikwazo hivyo haraka iwezekanavyo kuanzia siku ya jumatatu na wanatarajia kulenga biashara za binafsi na ambazo zina uhusiano na Rais Vladimir Putin wa Urusi.
Viongozi hao wa G7 wameelezea kuguswa kwa na jinsi Urusi ilivyoshindwa kuacha kuwasaidia wanaoipinga serikali.
Wametoa wito kwa Urusi kuacha mipango yake kijeshi ya siri kwenye mpaka na Ukraine.
Kwa upande mwingine viongozi hao wa nchi saba tajiri duniani wameisifu Ukraine kwa jinsi walivyojizuia kwa kupanda na wapiganaji waasi.
Serikali ya Ukraine imesema inahofia kuwa Urusi ina mipango ya kuivamia. Hata hivyo Urusi imesema nchi za magharibi zina mipango ya kuteka kuitawala nchi yao.

HAKUNA KATIBA BILA UKAWA...!!!

kingunge c2ea5
Na Hudugu Ng'amilo
MWANASIASA mkongwe na Mjumbe wa Bunge Maalumu la Katiba, Kingunge Ngombale – Mwiru, amesema makada wenzake wanaomshambulia aliyekuwa Mwenyekiti wa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, Jaji Joseph Warioba, wanakitukana Chama Cha Mapinduzi (CCM).
Alisema kumtukana au kumshambulia Jaji Warioba, au wajumbe wengine wa tume hiyo ni sawa na kukitukana Chama Cha Mapinduzi (CCM) kinachoongoza serikali.
Kingunge alitoa kauli hiyo jana bungeni alipokuwa akichangia sura ya kwanza na ya sita ya rasimu ya Katiba, ambapo alisema wanaomshambulia Jaji Warioba wanaonyesha utovu wa adabu, kwa kuwa chama kina maadili na adabu katika kushughulikia masuala mbalimbali.
"Mimi sitakubali hata kidogo wajumbe watumie msimamo wa chama kumshambulia Warioba au wajumbe wengine wa iliyokuwa Tume ya Mabadiliko ya Katiba, si halali kumshambulia Warioba au mjumbe yeyote yule binafsi.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI APRIL 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.

.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...