Thursday, January 30, 2014

MKUU WA WILAYA AFUNGA KIWANDA CHA SUKARI

miwa e4424
Mkuu wa Wilaya ya Mvomero, Antony Mtaka amekifungia kwa muda usiojulika shughuli za uzalishaji, Kiwanada cha Sukari cha Mtibwa mpaka kiwanda hicho kitakapolipa madeni ya wafanyakazi na wakulima wa miwa.
Akitoa msimamo wa Serikali ya wilaya hiyo juu ya kukifungia kiwanda hicho mbele ya wafanyakzi na wakulima hao katika mkutano wa hadhara uliofanyika katika ofisi za mtendaji wa kata ya Mtibwa wilayani hapa, Mtaka alisema, wamechukua uamuzi huo baada ya mabishano ya muda mrefu baina ya pande mbili kutofikia muafaka.
Mkuu huyo wa wilaya katika mabishano hayo ya muda mrefu juu ya madai ya wakulima na wafanyakazi alisema wanakidai Kiwanda cha Mtibwa zaidi ya Sh1.9 bilioni ambazo ni za mauzo ya miwa na mishahara ya wafanyakazi.
Mtaka alisema shughuli nyingine kiwandani hapo zitaendelea kama huduma ya afya, ulinzi na idara ya fedha ili kuwezesha makundi hayo kupata mafao yao mwishoni mwa wiki hii kama ilivyoahidiwa na uongozi wa kiwanda hicho.
Meneja mkuu Hamad Juma alisema, kiwanda hicho kilikwama kulipa madeni hayo kutokana na uingizwaji mwingi wa sukari nchini uliosababisha wao kukosa soko ingawa waliahidi kuanza kulipa mwezi huu. Chanzo: mwananchi

MAN UNITED YAKATAA MABILIONI KWA JANUZAJ

JANU eb4eb
HATUTAKI, na tena hatutaki hata kusikia. Na ikiwezekana msirudi tena. Ndivyo ambavyo mapovu yamewatoka mdomoni watu wa Manchester United baada ya PSG kurudi mezani juzi Jumapili na ofa ya kumtaka kinda wao mahiri, Adnan Januzaj.
PSG wamekuwa wakitokwa udenda kwa kinda huyo mwenye asili ya Albania aliyezaliwa Ubelgiji miaka 18 iliyopita na hawajali kama aliingia mkataba mpya wa kuichezea Man United mwishoni mwa msimu uliopita.
Hata hivyo, kocha David Moyes amekataa ofa hiyo ya PSG inayodhaniwa kuanzia Pauni 25 milioni na kuendelea huku wakisisitiza kwamba hawana mpango hata wa kukaa chini na kuzungumza na matajiri hao wa mafuta kutoka Paris.
Man United imempatia mkataba mrefu wa miaka mitano Januzaj Oktoba mwaka jana baada ya kugundulika kuwa huenda mchezaji huyo angekuwa huru na kuondoka Mei mwaka huu mara baada ya msimu kumalizika.

RAIS KIKWETE AMPIGA KIJEMBE RAGE

rage1 1d2f4
RAIS Jakaya Kikwete amemshangaa Mwenyekiti wa Simba SC ya jijini Dar es Salaam, Ismail Aden Rage kwa kuitisha mkutano wenye ajenda moja kwa ajili ya wanachama wa klabu hiyo. Wiki iliyopita, Mwenyekiti wa Simba Rage, alitangaza kuwepo kwa mkutano wa klabu hiyo Machi 23 na kueleza wazi kuwa kutakuwa na ajenda moja ya kujadili mapungufu ya Katiba.
Akizungumza mbele ya umati wa watu waliohudhuria mazishi ya Mbunge wa Chalinze, Saidi Bwanamdogo mwishoni mwa wiki iliyopita, Rais Kikwete ambaye alifika katika eneo la makaburi, alimuuliza Mwenyekiti huyo wa Simba kuhusiana na maandalizi ya mkutano huo.
"Ndugu yangu Rage mimi Mwenyekiti mwenzio, lakini sijawahi kuona mkutano wenye ajenda moja ndio kwanza huo wa kwako, yaani wewe kiboko, pamoja na makelele yote lakini umeweza kutuliza hali ya mambo mpaka leo umedumu kuwa mwenyekiti," alisikika Rais Kikwete akisema huku mamia ya waombolezaji wakicheka.
Akizungumzia kauli hiyo ya Rais Kikwete, Rage alisema ili kuwa kiongozi imara ndani ya klabu za Simba na Yanga, inakupasa kuwa na roho ngumu, kwani bila ya kufanya hivyo wanachama watakuwa wakikuchezea kila kukicha.
"Mheshimiwa Rais kuwa kiongozi ndani ya klabu hizi mbili kunahitaji umakini sana, kwani bila ya kufanya hivyo wewe utakuwa ni kiongozi wa kupelekwa kila siku na hatimaye unamaliza muda hakuna ulichokifanya ndani ya uongozi wako," alisema Rage. Chanzo: mtanzania

IKULU YAVUNJA UKIMYA KUHUSU "MAWAZIRI MIZIGO" ...!!!


kawambwa_2846f.jpg
SHUKURU KAWAMBWA
Dar es Salaam. Ikulu imetaka kufungwa kwa mjadala wa kuhusu kurudishwa kwa mawaziri wanaodaiwa kuwa ni mizigo kwenye Baraza la Mawaziri na badala imetaka waachwe wafanye kazi.
Mkurugenzi wa Mawasiliano Ikulu, Salva Rweyemamu alisema kuendeleza mjadala huo ni kupoteza muda, kwani Rais Jakaya Kikwete alishamaliza kazi yake.

Rweyemamu alisema Rais ndiye mwenye mamlaka ya kuteua mawaziri ambao wana wajibu wa kumsaidia katika utekelezaji wa majukumu yake, hivyo si sahihi wateule hao kuitwa 'mizigo' kwani yeye (Rais) ameona wanafaa.
"Rais anapoteua watu anaangalia wanaofaa kumsaidia na si vinginevyo. Kwani lengo lake ni kuona nchi ina 'move forward' (inasonga mbele) kimaendeleo," alisema Rweyemamu. Alisema watu wanapaswa kukumbuka kuwa mtu anapoteuliwa kwenye uwaziri kuna suala la uwajibikaji: "Anatakiwa kutekeleza uwajibikaji wa pamoja. Sasa kumshambulia mtu binafsi na kumwita mzigo siyo sahihi."

Rweyemamu alisema mjadala huo kwa sasa umepitwa na wakati na kuwataka wananchi na wachambuzi kuwaacha mawaziri hao kuchapa kazi.
"Ni vizuri wananchi wakawapa nafasi mawaziri hawa ya kufanya kazi na baadaye kuwapima na kuwachambua kutokana na utendaji wao," alisema.
Chimbuko la majadala
Mjadala kuhusu suala hilo unatokana na Rais Kikwete kuwarejesha katika Baraza la Mawaziri baadhi ya mawaziri ambao walidaiwa kuwa ni mizigo kutokana na udhaifu katika utendaji wao.

NEC "DAFTARI LA WAPIGA KURA LITABORESHWA"

 
Mwenyekiti wa Nec, Jaji Damian Lubuva.PICHA|MAKTABA 
**********
Pamoja na kushindwa kutaja tarehe rasmi ya kuanza kuboresha daftari la kudumu la wapigakura, Tume ya Taifa ya Uchaguzi (Nec) imesema daftari hilo litaboreshwa kabla ya kuanza kwa upigaji wa kura ya maoni kwa ajili ya kupata Katiba Mpya. Upigaji wa kura hiyo utafanyika ndani ya siku 70 baada ya kumalizika kwa Bunge Maalumu la Katiba linalotarajiwa kuanza katikati ya mwezi ujao mjini Dodoma. Litafanyika kwa kati ya siku 70 na 90.

Nec imetoa ufafanuzi huo baada ya kuwepo kwa malalamiko kutoka kwa vyama vya siasa na wananchi kwamba tangu uchaguzi mkuu wa mwaka 2010, daftari hilo halijawahi kuboreshwa, jambo ambalo litasababisha upigaji wa kura kwa ajili ya kupata Katiba Mpya kutawaliwa na vurugu. Malalamiko hayo yanatokana na kuwepo kwa idadi kubwa ya watu waliotimiza umri wa kupiga kura lakini hawamo katika daftari hilo.
Pia waliopoteza vitambulisho vya kupigia kura na wenye kasoro mbalimbali zinazowafanya wapoteze sifa.

HAYA HAPA MATOKEO YA MECHI ZA LIGI KUU YA UINGEREZA, USIKU WA JUMATANO

MAGAZETI YA LEO JANUARI 30, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Tuesday, January 28, 2014

"MBWA MWITU" SASA TISHIO KWA WANANCHI WA TABATA DAR


Dar es Salaam. Wakazi wa Tabata na viunga vyake, sasa wanaishi kwa wasiwasi mkubwa kutokana na kuibuka kwa kundi la vijana, wanaojiita Mbwa Mwitu wakitumia silaha za jadi, kujeruhi watu na kupora mali nyakati za usiku.
Mmoja wa wananchi wa Tabata Matumbi alisema wiki mbili zilizopita, vijana hao walimuua mwanamume mmoja kwenye Daraja la Reli la Matumbi. Kwa mujibu wa mtoa habari huyo ambaye hata hivyo hakutaka jina lake litajwe, mtu huyo alichinjwa na kichwa chake kutenganishwa na kiwiliwili.
“Watu walipeleka kiwiliwili kituo cha polisi, maana kichwa hakikupatikana na haikufahamika kama alitambuliwa au vipi. Yaani sasa hivi ikifika saa tatu watu inabidi tubaki ndani,” alisema.
 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

M4C OPERESHENI PAMOJA DAIMA NDANI YA IRINGA


Katibu Mkuu wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), Dk. Willibrod Slaa akiwahutubia maelfu ya wakazi wa Manispaa ya Iringa, katika mkutano wa hadhara wa Operesehni M4C Pamoja Daima, uliofanyika kwenye Uwanja wa Mwembe Togwa jana.
Mbunge wa Kawe, Halima Mdee akihutubia katika mkutano wa hadhara wa Operesheni M4C ya Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), uliofanyika kwenye Uwanja wa Mwembe Togwa mjini Iringa jana.
Maelefu ya wakazi wa Manispaa ya Iringa na vitongoji vyake wakiwa katika mkutano wa hadhara wa Operesheni ya M4C Pamoja Daima wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), uliofanyika kwenye Uwanja wa Mwembe Togwa jana. (PICHA NA CHADEMA)

 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

KINANA KUPIGA KAMBI Z’BAR KUIMARISHA CCM

kinana_98cb1.jpg
Na Mwinyi Sadallah, Mwananchi
Zanzibar. Katibu Mkuu wa CCM Abdulrahman Kinana amesema ameamua kuweka kambi Zanzibar, lengo likiwa ni kuimarisha chama hicho na kuhakikisha CCM inarejesha majimbo yake yaliyopotea tangu kuanzishwa kwa mfumo wa vyama vingi mwaka 1995.
Kinana aliweka msimamo huo kwenye mkutano wa hadhara wa uzinduzi wa miaka 37 ya kuzaliwa CCM, uliofanyika uwanja wa Soka Kiembesamaki mjini hapa juzi.
Alisema kambi hiyo itaanza kabla ya Aprili mwaka huu, kwa kufanya ziara kuanzia ngazi ya wadi, jimbo, wilaya hadi mikoa kukagua hali ya kisiasa na kuweka mikakati mipya ya chama hicho kisiwani Zanzibar.
"Nitaanza ziara maalumu kabla ya sherehe za Muungano, mengi nitayazungumza wakati huo ukifika, lengo kubwa ni kuangalia uhai wa chama chetu na kuweka mikakati ya kisiasa kabla ya mwaka," alisema Kinana.
Alisema kazi kubwa ya CCM ni kutekekeza sera na ilani yake ya uchaguzi tofauti na vyama vya upinzani, ambavyo ni mahiri na hodari wa kusema bila ya kuonyesha vitendo.
Katibu Mkuu huyo aliviponda vya upinzani nchini na kwamba, CCM imewaachia kazi ya kusema, yenyewe imekijikita kuwatumia wananchi na kutekeleza majukumu yake ya kisera, mipango na mwongozo.
Kuhusu Mapinduzi ya Zanzibar ya mwaka 1964, Kinana alisema watu waliobeza Mapinduzi hayo hivi sasa wamefedheheka kwa kushuhudia yakitimiza miaka 50 huku taifa likiwana hali ya amani, umoja na mshikamano.

 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MTWARA WASHUSHIWA BEI YA KUINGIZA UMEME HADI TSH. 27,000/=

mhongo 67365
Serikali imetangaza neema kwa vijiji vinavyopitiwa na bomba la gesi ambavyo vipo mkoani Mtwara na Lindi, sasa wataunganishiwa kwa Sh27,000. (HM)
Hatua hiyo ilitangazwa na Waziri wa Nishati na Madini, Profesa Sospeter Muhongo mbele ya Waziri Mkuu, Mizengo Pinda kwenye uzinduzi mradi wa umeme wilayani Nanyumbu na Masasi.
Profesa Muhongo alisema gharama za kuunganisha umeme kwa sasa ni Sh177,000.
Alisema zaidi ya vijiji 50 vimepewa upendeleo huo ili kuwawezesha wananchi kuwa na maisha bora.
Lengo la Serikali ni kufikia asilimia 30 ya wasasatu waliounganishwa na umeme na kwamba, hivi sasa ni asilimia 23 pekee wanaopata umeme nchini wakati Mtwara ni asilimia nne.
 Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

CHADEMA WAANZA KAMPENI ZA URAIS...!!!

Willibrod-Slaa 9cd30
Viongozi mbalimbali wa Chadema wameanza kupiga kampeni za urais mwaka 2015 kupitia Operesheni Pamoja Daima. (HM)
Akihutubia mamia ya wakazi wa Mkoa wa Njombe huku mvua kubwa ikinyesha jana, Katibu Mkuu wa chama hicho, Dk Willibrod Slaa aliwatahadharisha vigogo wa Serikali wanaoiba fedha za umma kuwa, atawashtaki na kuwafilisi iwapo chama hicho kitashinda uchaguzi mwaka 2015.
Alisema chama hicho kikishinda dola, kitaboresha masilahi kwa watumishi waadilifu lakini mafisadi wanaotafuna fedha za Serikali watapata wakati mgumu.
"Tutakuwa wakali kwa walarushwa," alisema Dk Slaa.
Dk Slaa alisema watendaji walarushwa na wezi watashtakiwa ili mali walizowaibia Watanzania zirejeshwa Serikalini.
"Ninawapa miezi 15 kabla ya uchaguzi mkuu, vigogo hao kurudisha mali walizoiba vinginevyo watajuta kwa sababu tutawashtaki tutakapoingia madarakani." alisema.
Naye Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo alisema chama hicho kitatumia kila aina ya 'silaha' kilichonayo kuhakikisha majimbo yote ya Mkoa Kilimanjaro yananyakuliwa na chama hicho 2015.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

NYOKA MKUBWA AINA YA COBRA AILAZIMISHA NDEGE KUTUA BILA KUFIKA MWISHO WA SAFARI

NewsImages/6694982.jpgMoja ya ndege zinazo milikiwa na shirika na ndege la Misri.
NYOKA aina ya Cobra amesababisha kizaza kwenye ndege na kuilazimisha kukatisha safari yake na kutua kwa dharura katika uwanja wa ndege wa Hurghada nchini Misri, auliwa baada ya kumjeruhi abiria .
Nyoka huyo alizua mtafaruku huo baada ya kutoka katika mfuko alipokuwa amehifadhiwa na kumjeruhi abiria mmoja raia wa Jordan aliekuwa amekaa karibu na mfuko uliokuwa amehifadhiwa nyoka huyo.
Abiria walianza kumshambulia wakijaribu kumuua kwa kumpiga na viatu na hatimae kufanikiwa kumuua, abiria aliejeruhiwa alipatiwa huduma ya kwanza, na kuhamishiwa hospitalini kwa matibabu zaidi na kuwekwa chini ya uangalizi kwa masaa 24, hali iliopekea kukatisha safari yake.

Uchunguzi wa awali uliofanywa umebaini kwamba, mmoja wa abiria alimficha nyoka huyo kwenye mkoba na alifanikiwa kupita katika vizuizi na kuingia na nyoka huyo kwenye ndege.

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya 
Jambo Tz

MWANAMKE ANASWA NA NGOZI YA CHUI...!!!

Mwanamke anaswa na ngozi za chui
JESHI la Polisi Kanda Maalumu ya Dar es Salaam linamshikilia Mwajuma Hamisi, mkazi wa Yombo Vituka kwa kosa la kukutwa na ngozi mbili za chui kinyume cha sheria, zenye thamani ya sh milioni 11.
Akizungumza na waandishi wa habari jijini Dar es Salaam jana, Kamishna wa Polisi wa kanda hiyo, Suleiman Kova, alisema mwanamke huyo alinaswa Januari 18, mwaka huu katika eneo la Yombo Vituka, Wilaya ya Temeke.
Kova alisema mwanamke huyo alinaswa baada ya Ofisa Mhifadhi Wanyamapori mkazi wa Ukonga, kutoa taarifa kituoni hapo kwamba kuna mwananchi anauza ngozi za chui.
Alisema askari walifika eneo la tukio na kumkamata mtuhumiwa na walipompekua chumbani kwake, walimkuta na nyara hizo za serikali.

Wakati huo huo, jeshi hilo limesema limemuua jambazi sugu la uhalifu wa kutumia silaha katika majibizano ya risasi na polisi.
Alisema awali polisi waliweka mtego ili kuyanasa majambazi hayo Januari 22 baada ya kufanya tukio la uporaji wa sh milioni 29 kwa mfanyabiashara wa Mtaa wa Kariakoo, anayejulikana kwa jina la  Shanys Abdalla, mkazi wa Mbezi.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE TAREHE 28.01.2013 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Tuesday, January 21, 2014

OBAMA AISIFIA BANGI NA KUIPONDA POMBE...!!

Obama 1 
Rais Barack Obama wa Marekani amesema kuvuta bangi ni salama zaidi kuliko kunywa pombe lakini akawasisitizia mabinti zake kwamba hilo sio wazo zuri pia ambapo kwa mujibu wa gazeti la The Mirror,  amesema anaamini uvutaji bangi hauna madhara au athari za hatari kwa mtumiaji binafsi.
Obama ambae aliwahi kuvuta kwenye enzi za ujana wake anasema “uvutaji sio kitu ambacho nachochea kifanyike, tambua ni upotezaji muda na inaathiri afya, bangi imehalalishwa kwenye miji ya Colorado na Washington kwa kura ya maoni na ilikuwa ni muhimu kwa ajili ya mataifa kumaliza uhalifu wa vijana wadogo wanaotoka kwenye familia zenye asili ya umasikini”
“tabaka la watoto wa kati hawafungwi kwa uvutaji bangi bali wanaofungwa ni wale watoto wa maskini, watoto wenye asili ya African -American na wa Kilatino wengi wao hawana uwezo wa kuwa rasilimali au misaada kuweza kuepuka vifungo vikali, hatupaswi kufunga watoto wetu au watumiaji binafsi vifungo virefu vya jela wakati baadhi ya hawa watunga sheria nao wamefanya uhalifu huo huo”
Bangi imebaki kuwa chini ya usimamizi wa sheria licha ya kwamba imehalalishwa kwenye miji ya Colorado na Washington huku serikali ikiwa haina nia ya kubadili msimamo wake.
Dawa hii ya kulevya iliingia sokoni Colorado na kusababisha foleni ndefu kwenye vituo mbalimbali vya uuzaji kuanzia Januari 1 huku na mji wa Washington ukitarajiwa kufuata.
Sentensi nyingine kutoka kwa Obama >>>  “ni muhimu kusonga mbele kwa sababu ni muhimu kwa jamii kutokuwa na hali ambayo sehemu kubwa ya watu kwa wakati mmoja au mwingine wamevunja sheria na ni wachache wanaoadhibiwa, wale ambao wanasema kuhalalisha bangi ni tiba na inatatua matatizo kijamii pengine (overstating) wanainua/wanakuza kesi.

SOMA MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 21, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.


.

Monday, January 20, 2014

AJALI YATOKEA MBALIZI MBEYA, MAGARI ZAIDI YA MATANO YAGONGWA

 Magari yakiwa yamegongwa Mbalizi Mbeya

MWANAJESHI FEKI AKAMATWA TANGA AKIMTAPELI DC

'Koplo' feki wa JWTZ akiwa ofisini kwa mkuu wa wilya.


 'Koplo' feki akijiandaa kupanda  kwenye gari kupelekwa kituo cha polisi kwa mahojiano zaidi

SOMA SABABU YA MAWAZIRI MIZIGO KUACHWA KWENYE BARAZA LA MAWAZIRI...!!!


RAIS JAKAYA KIKWETE.

SERIKALI imetoa kauli kuhusu tuhuma zilizokuwa zikiwakabili baadhi ya mawaziri, waliobatizwa jina la ‘Mawaziri Mizigo’, na hatua ambazo zimekuwa zikichukuliwa kukabiliana na kero zilizosababisha wapewe jina hilo.

Akizungumza na waandishi wa habari jana Ikulu Dar es Salaam, Katibu Mkuu Kiongozi, Balozi Ombeni Safue, alisema mawaziri hao walituhumiwa kutokana na changamoto zilizopo katika wizara zao; na si upungufu wao binafsi kama viongozi.

Mawaziri hao saba walitajwa katika ziara ya mikoani ya Katibu Mkuu wa CCM, Abdulrahman Kinana na baadae walihojiwa katika kikao cha Kamati Kuu cha chama hicho.

Baada ya kuhojiwa, Katibu wa Halmashauri Kuu ya CCM (NEC), Itikadi na Uenezi, Nape Nnauye, alisema Kamati Kuu ilimuachia Rais Kikwete jukumu la kuamua kuwafukuza kazi, kuwahamisha au kuwataka kutekeleza majukumu yao kikamilifu.

Miongoni mwa mawaziri waliohojiwa ni aliyekuwa Naibu Waziri wa Fedha, Saada Mkuya, ambaye sasa ameteuliwa kuwa Waziri wa Fedha.

HII NDIO THAMANI YA JINO MOJA LA NDOVU NA JINSI BIASHARA INAVYOFANYWA

  2013-04-28-TimphotobyCarlSafina.JPG
Yafuatayo ni kuhusu biashara ya meno ya tembo

Kwanza: Matumizi yake; meno ya tembo hutumika kutengeneza vitu vya urembo kama vile hereni , mikufu, mapambo kama vile sanamu na hata keys za keyboards za vinanda.
Vifaa vilivyotengenezwa kwa meno ya tembo hutumika nchini China kama sehemu ya kuonyesha ufahari, kwa mujibu wa Wikipedia.


Pili: Bei ya meno ya tembo

Bei inategemea na soko , hata hivyo kwa mujibu wa answers.com , jino moja la tembo huweza kuuzwa kwa dola za kimarekani mia saba (700).

Tuesday, January 14, 2014

MHUDUMU WA MOCHWARI 'AMCHIMBA MKWARA' WAZIRI...!!!


Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid. PICHA|MAKTABA 
*******
Mfanyakazi wa Kitengo cha Kuhifadhi Maiti cha Hospitali ya Rufaa ya Mbeya, Eugene Vurugu amemtisha Naibu Waziri wa Afya na Ustawi wa Jamii, Dk Seif Rashid kuwa ikitokea amefariki dunia akiwa mkoani Mbeya, basi maiti yake italazwa kwenye sakafu hospitalini hapo.
Akizungumza kwenye mkutano wa wafanyakazi na naibu waziri huyo mwishoni mwa wiki iliyopita, Vurugu alisema kitengo hicho kimezidiwa na wingi wa maiti zinazopelekwa hospitalini hapo.
Alisema kitengo hicho cha kina majokofu sita tu na hulazimika kuhifadhi miili kwa zamu ili angalau maiti zisiharibike.
“Hata wewe Waziri ukifa leo, hakuna pa kukuweka.
Utawekwa sakafuni kusubiri maiti nyingine zipoe halafu utaingizwa ndani kwa kuingizwa maiti mbili kwenye eneo la mtu mmoja,’’ alisema Vurugu.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

JAMBO TZ BLOG INAWATAKIA WAISLAM WOTE DUNIANI KHERI YA SIKUKUU YA MAULID

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMANNE JANUARI 14, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC03476

DSC03460
DSC03463
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

CHRISTIANO RONALDO ATWAA TUZO YA FIFA BALLON D'OR 2013

MSHAMBULIAJI wa Real Madrid, Cristiano Ronaldo, ameuvunja utawala wa miaka minne wa Lionel Messi wa Argentina anayechezea klabu pinzani ya Barcelona baada ya kunyakua tuzo ya Mwanasoka Bora wa Dunia wa Fifa usiku wa kuamkia leo.
Ronaldo amemshinda pia Franck Rivery, Mfaransa anayechezea Bayern Munich.
Sherehe za tuzo hizo zilifanyika Zurich, Uswisi.
Nadine Angerer
Kwa upande wa wanawake, kipa wa timu ya taifa ya Ujerumani, Nadine Angerer ameibuka kinara mbele ya Marta (Brazil) na Abby Wambach (Marekani). Mdada huyo aliisaidia Ujerumani kutwaa taji ya Euro 2013 kwa wanawake akiokoa penati katika mechi yao ya fainali dhidi ya Norway waliyoshinda 1-0.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Monday, January 13, 2014

HODI TENA...!!! OPERESHENI TOKOMEZA YA PILI KUANZA KARIBUNI

Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu.
WAKATI hatua zaidi zikisubiriwa kuchukuliwa kwa watendaji waliohusika na ukiukwaji wa haki za binadamu wakati wa Operesheni Tokomeza, Rais Jakaya Kikwete anatarajiwa kutangaza kuanza kwa awamu ya pili ya Operesheni hiyo wakati wowote kuanzia sasa.
Akizungumza na waandishi wa habari jana, Naibu Waziri wa Maliasili na Utalii, Lazaro Nyalandu, alisema wakati wowote Rais Kikwete atatangaza kuanza kwa Awamu ya Pili ya Operesheni Tokomeza na itazingatia haki zote ikiwemo haki za binadamu.
Nyalandu alisema ingawa awamu ya kwanza kulikuwa na kasoro zilizojitokeza, awamu hii ya pili kasoro hizo zitafanyiwa kazi ili kuhakikisha rasilimali za Taifa zinalindwa.
Kusitishwa kwa operesheni hiyo kulikosababisha uteuzi wa mawaziri watatu kutenguliwa na waziri mmoja, kujiuzulu kwa mujibu wa Nyalandu, kulisababisha pia tembo 60 kuuliwa.
Mawaziri ambao uteuzi wao ulitenguliwa na Rais Kikwete mwishoni mwa mwaka jana ni Dk Emmanuel Nchimbi (Mambo ya Ndani ya Nchi), Shamsi Vuai Nahodha (Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa) na Dk David Mathayo (Maendeleo ya Mifugo) huku Balozi Khamis Kagasheki (Maliasili na Utalii), akijiuzulu.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

TAARIFA YA CHADEMA KWA UMMA KUHUSU TUHUMA DHIDI YA M/KITI, FREEMAN MBOWE

TAARIFA KWA UMMA

KUHUSU TUHUMA DHIDI YA MWENYEKITI WA TAIFA, FREEMAN MBOWE
Kama mojawapo ya mikakati ya baadhi ya watu wanaotaka kuhamisha mjadala wa makosa yanayowaandama ya utovu wa maadili na usaliti dhidi ya chama, hivi karibuni, Mwenyekiti wa Chama Taifa, Freeman Mbowe amezushiwa tuhuma zisizokuwa na ukweli wowote zikilenga kumchafua kwa nafasi yake ya uongozi na kuipaka matope taasisi anayoiongoza;

Tuhuma hizo ni pamoja na;

1.     Kwamba Mwenyekiti wa CHADEMA Taifa mwaka 2005 eti alichukua fedha kutoka kwa Mbunge wa Musoma Vijijini (CCM), Nimrod Mkono kiasi cha sh.Milioni 40 ili Mwenyekiti Mbowe asifanye kampeni katika jimbo hilo.

2.     Mwaka 2008, eti Mbunge Mkono alimpatia Mwenyekiti wa Chama Taifa, sh. Milioni 20 kwa ajili ya uchaguzi mdogo wa
Tarime, kisha akazitoa kwenye chama kama mkopo na akalipwa.

3.    Mwaka 2010, wakati wa uchaguzi mkuu Mbunge Mkono eti alimpatia Mwenyekiti wa Chama Taifa sh. Milioni 200 kwa ajili ya kampeni za mgombea urais.

4.     Mwaka huo huo wakati wa uchaguzi mkuu, eti Mwenyekiti wa Chama Taifa, alipokea sh. Milioni 100 kutoka kwa Rostam Aziz kwa ajili ya kampeni.

Idara ya Habari ya CHADEMA, inapenda kusema yafuatayo;

1.    Hakuna ukweli hata mmoja katika tuhuma hizo. Ni uongo na uzushi uliopangiliwa kama moja ya mikakati ya watu wenye malengo ya kutaka kuilaghai jamii kwamba viongozi wa CHADEMA hawana tofauti na wale wa CCM na kwamba chama hiki kikuu cha upinzani kinachobeba matumaini ya Watanzania katika kupigania haki zao na kupinga kila aina ya ufisadi, kionekane hakina tofauti na chama kilichoko madarakani, ambacho kimepoteza ushawishi kwa wananchi.

2.     Matokeo ya uongo huo ni kutaka kuisaidia CCM na kugeuza mjadala.

3.    Idara ya Habari ya CHADEMA inapenda kuuambia umma wa Watanzania wote, hususan wanachama, wapenzi, mashabiki wa CHADEMA na wapenda mabadiliko nchini kwamba,Mwenyekiti wa Chama Taifa, ameshawasiliana na mawakili walifanyie kazi suala hili kwa ajili ya kuchukua hatua za kisheria.

4.     Kwa uhakika tunapenda kuiambia jamii ya Watanzania wote, hususan wanachama, wapenzi, mashabiki wa CHADEMA na wapenda mabadiliko wote nchini, kwamba; Chama wala Mwenyekiti wa Chama Taifa, mahali popote na wakati wowote, hajawahi kupokea msaada wa fedha hizo kutoka kwa waliotajwa kwa malengo yaliyosemwa.

5.     Tungependa kuwaambia waliozusha tuhuma hizo, ni vyema kama wanapenda kutunza heshima kidogo waliyobakiza katika jamii kutokana na kuelemewa na mzigo wa tuhuma za utovu wa maadili na usaliti dhidi ya CHADEMA, badala ya kugeuka kuwa mabingwa wa kupika uongo, wajibu masuala ya msingi yanayowaandamana kuhusu mikakati yao ya kuhujumu CHADEMA na viongozi wake, ambayo iwapo chama kisingeibaini na kuchukua hatua za kinidhamu, ingesababisha kuua ndoto na matumaini ya Watanzania kufanya mabadiliko ya kimfumo na kiutawala, kwa kuiondoa CCM madarakani.

6.     Taarifa kuhusu baadhi ya tuhuma katika mkakati huo ambazo zimemlenga Mwenyekiti wa Chama Taifa, kwa kuhusisha shughuli zake binafsi za uwekezaji, zitajibiwa kupitia taasisi husika.

Imetolewa leo Dar es Salaam na;
Tumaini Makene
Ofisa Mwandamizi wa Habari- CHADEMA

MALINZI AZINDUA KAMPENI YA ISHI HURU

Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi akizungumza kwenye uzinduzi wa programu ya Ishi Huru jijini Dar es Salaam.
Rais wa Shirikisho la Mpira wa Miguu Tanzania (TFF), Jamal Malinzi amezindua programu ya kutoa elimu ya kupambana na matumizi ya dawa za kulevya kwa vijana iitwayo Ishi Huru.
Programu hiyo iliyozimduliwa tarehe 10 Januari mwaka huu jijini Dar es Salaam iko chini ya taasisi ya Africa Inside Out inayoongozwa na Rebecca Young wakati washirika (partners) ni TFF na kampuni ya Rhino Resources ya Marekani.
Rais Malinzi amesema matumizi ya dawa za kulevya nchini yamekuwa yakiongezeka, hivyo kuwa kikwazo kwa maendeleo ya vijana ambapo ameipongeza Africa Inside Out kwa programu hiyo kwa vile itazuia vijana wengi kujiingiza katika matumizi ya dawa hizo.
"Moja athari kubwa za matumizi ya dawa za kulevya ni kupata maambukizi ya virusi vya Ukimwi kutokana na kuchangia sindano za kujidunga dawa hizo.
"TFF tutatoa ushirikiano wa kutosha katika programu hii. Lakini pia tutaingiza Ishi Huru katika programu zetu za mpira wa miguu kwa vijana. Tutahamasisha jamii katika kupambana na dawa za kulevya," amesema.
Katika uzinduzi huo, pia Rais Malinzi alizundua semina ya waelimishaji na kuwaeleza kuwa wamepata fursa hiyo kwa vile ni vijana wanaojituma, hivyo watafikisha vizuri ujumbe wa Ishi Huru katika shule na vituo vya vijana nchini.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MBUNGE WA CHADEMA MH. NDESAMBURO AMKINGIA KIFUA LOWASSA ASEMA ASISAKAMWE

Philemon Ndesamburo na Edward Lowassa 
WAKATI Chama Cha Mapinduzi (CCM) kikionekana kutikiswa na ushawishi wa Waziri Mkuu aliyejiuzulu, Edward Lowassa, wa kutaka kutimiza safari yake ya kuwapatia Watanzania elimu bure, Mbunge wa Moshi Mjini, Philemon Ndesamburo (CHADEMA), amejitokeza kumkingia kifua na kutaka asisakamwe.

Kauli ya Ndesamburo inakuja siku chache wakati kukiwa na harakati za wazi wazi kuwapinga wanaotajwa kutaka kuwania urais, zikishika kasi ndani ya CCM na kuonekana kuzigonganisha vichwa jumuiya zake.  
Akitoa salamu zake za mwaka mpya jana, pamoja na kuzungumzia hali ya kisiasa nchini kuelekea uchaguzi wa Serikali za Mitaa na Uchaguzi Mkuu mwakani, Ndesamburo alisema Lowassa hapaswi kushambuliwa kwa kigezo cha kutangaza safari yake.  
“Wanaotangaza nia mbona wako wengi sana huko CCM na wala siyo Lowassa peke yake? Kwenye urais na hata huku chini kwenye ubunge na hata udiwani wako wengi tu wanafanya hivyo. Ina maana hao wanaomnyooshea kidole Lowassa hawa wengine hawawaoni?
“Hata huku kwenye vyama vyetu CHADEMA, CUF, NCCR-Mageuzi wapo wanaotuvuruga, lakini sasa hivi habari ya mjini ni Lowassa, Lowassa… kama kweli hatupendezwi na hali hiyo tuwanyooshee wote basi, kama hatuwezi wamwache aendeleze ndoto yake. The best way to predict the future is to invent it,” aliongeza Ndesamburo.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

CHELSEA YATOA PAUNI MILIONI 25 KUMSAJILI NEMANJA

Kiungo wa Benfica, Nemanja Matic (kulia) anahusishwa na kurejea Chelsea kwa Pauni Milioni 25
Toughness: Jose Mourinho sees Matic as the man to fill Chelsea's need in the holding role
Jose Mourinho anaona Matic ndiye anayefaa katika nafasi ya kiungo mkabaji Chelsea
KLABU ya Chelsea imetoa ofa ya Pauni Milioni 25 kumsajili kiungo wa Benfica ya Ureno, Nemanja Matic arejee Stamford Bridge.
Kiungo huyo hodari alijiunga na Chelsea mwaka 2009, lakini akacheza mechi mbili tu kabla ya kutimkia Ureno mwaka kama sehemu ya dili ya David Luiz kutua Stamford Bridge.
Pamoja nayo, kocha Jose Mourinho sasa anaona Matic kama mtu anayefaa katika nafasi ya kiungo mkabaji wa timu yake.
Chanzo:BIN ZUBEIRY

Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

ISRAEL KUMUAGA ARIEL SHARON, ALIKUWA MAHUTUTI KWA MIAKA 8....!!!

Maelfu ya watu nchini Israel wamekuwa wakitoa heshima zao za mwisho kwa hayati Ariel Sharon kabla ya mazishi yake hii leo.
Jeneza la Sharon liliwekwa nje ya majengo ya bunge mjini Jerusalem jana Jumapili huku waombolezaji wakimiminika kumtolea heshima za mwisho kabla ya maziko. Sharon alifariki akiwa na umri wa miaka 85 baada ya kuwa hali mahututi kwa miaka 8, akitumia mashine kupumua. Atafanyiwa ibada maalum ya kitaifa leo kabla ya kuzikwa karibu na shamba lake eneo la Sderot.
Waisreli pamoja na viongozi wa dunia, wametoa heshima zao za mwisho , lakini wale ambao wanaweza kusema hawajaguswa sana na kifo cha Sharon ni wapalestina. Mwili wa Sharon ulifikishwa katika bunge la taifa Jumapili ambapo watu waliruhusiwa kuutizama siku nzima. Maombi yalifanywa huku bendera zikipepea nusu mlingoti. Watu waliendelea kumiminika nje ya jengo hilo wengine wakiwasha mishumaa katika hatua ya kumuenzi Sharon.

Wageni mashuhuri wanatarajiwa kuhudhuria ibada maalum ya Ariel katika bunge la taifa wakiwemo makamu wa Rais wa Marekani Joe Biden, waziri wa mambo ya nje wa Urusi Sergei Lavrov, mjumbe maalum wa Mashariki ya kati Tony Blair, na waziri wa mambo ya nje wa Ujerumani Frank-Walter Steinmeier.
Sharon anakumbukwa na wengi kwa siasa zake na harakati zake dhidi ya wapalestina wakati akiwa mwanajeshi. Aliidhinisha ujenzi wa makazi ya walowezi katika eneo la Palestina na pia baadaye tume ya uchunguzi ilimpata na hatia ya kukosa kuzuia mauaji ya wapalestina yaliyofanywa na wakristo wa Phalangist baada ya Iisrael kuvamia Lebanon.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

MBOWE KUMBURUZA ZITTO MAHAKAMANI

Freeman Mbowe na Zitto Kabwe MWENYEKITI wa Taifa wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (CHADEMA), anakusudia kumburuza mahakamani, Mbunge wa Kigoma Kaskazini, Zitto Kabwe, kwa madai ya kumkashifu na kumchafulia jina.  
Kwa mujibu wa taarifa toka Kurugenzi ya  Habari na Uenezi ya CHADEMA, Mbowe amezushiwa tuhuma zisizokuwa na ukweli wowote zikilenga kumchafua kwa nafasi yake ya uongozi na kuipaka matope taasisi anayoiongoza. Tayari Mbowe kwa mujibu wa taarifa hiyo, ameshawasiliana na wanasheria wake kwa ajili ya kuchukua hatua za kisheria dhidi ya aliyezusha uongo huo. Ingawa taarifa hiyo haikutaja jina la Zitto, lakini hivi karibuni mbunge huyo katika ukurasa wake wa facebook, aliibua tuhuma nzito dhidi ya Mbowe. 
 
  Zitto, Samson Mwigamba na Dk. Kitila Mkumbo, walivuliwa nyadhifa zao na Kamati Kuu (CC) ya CHADEMA. Baadaye CC iliwatimua uanachama Mwigamba na Kitila kwa tuhuma za kukisaliti na kukihujumu chama, huku Zitto akikimbilia mahakamani kuzuia asijadiliwe. Akiwa na kesi mahakamani, Zitto aliingia mtegoni kwa kushambulia viongozi wake mitandaoni kwa kutoa tuhuma nzito dhidi ya Mbowe. 
  Katika tuhuma hizo, Zitto alidai Mbowe alipokea michango ya pesa kutoka kwa makada wa CCM, Nimrod Mkono na Rostam Azizi, kusaidia kampeni za CHADEMA mwaka 2005 na 2010.
Pia Zitto alidai kuwa Mbowe alipokea sh milioni 40 mwaka 2005 kutoka kwa Mkono ili asifanye kampeni katika Jimbo la Musoma Vijijini; na kwamba mwaka 2008 alimpatia sh milioni 20 kusaidia CHADEMA ishinde uchaguzi mdogo wa Tarime.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-like page ya facebook ya Jambo Tz

Sunday, January 12, 2014

RAIS KIKWETE ATANGAZA JUMATATU JANUARI 13, 2014 KUWA NI SIKU YA MAPUMZIKO

THE UNITED REPUBLIC OF TANZANIA
DIRECTORATE OF PRESIDENTIAL COMMUNICATIONS

Telephone: 255-22-2114512, 2116898
E-mail:  ikulumawasiliano@yahoo.com press@ikulu.go.tz              

Fax: 255-22-2113425

PRESIDENT’S OFFICE,
      THE STATE HOUSE,
       P.O. BOX 9120,  
DAR ES SALAAM.
Tanzania.
 
                                         
TAARIFA KWA  UMMA.
Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza kuwa kesho, Jumatatu, Januari 13, 2014, itakuwa ni Siku ya Mapumziko (Public Holiday) kwa Watanzania wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Rais Kikwete ameutangaza uamuzi huo mjini Zanzibar ambako leo ameungana na Watanzania na Wazanzibari wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, mwaka 1964.

Mapinduzi hayo yaliyoongozwa na mwasisi wa Zanzibar na Taifa la Tanzania, Hayati Abeid Amaan Karume yalifanikiwa kuung’oa madarakani utawala dhalimu wa Sultan na kuwawezesha kwa mara ya kwanza katika historia Waafrika walio wengine kujitawala ndani ya nchi yao wenyewe.

Yalikuwa ni Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofungua njia ya kuzaliwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar – miezi mitatu baada ya Mapinduzi hayo – Aprili 26, 1964.               
Naye Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein ametangaza kuwa kesho itakuwa Siku ya Mapumziko Tanzania Visiwani kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar. Rais Shein alitangaza mapumziko hayo wakati alipohutubia wananchi kwenye Uwanja wa Michezo wa Amaan mjini Zanzibar katika kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi.

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ametangaza kuwa kesho, Jumatatu, Januari 13, 2014, itakuwa ni Siku ya Mapumziko (Public Holiday) kwa Watanzania wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar.

Rais Kikwete ameutangaza uamuzi huo mjini Zanzibar ambako leo ameungana na Watanzania na Wazanzibari wote kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi Matukufu ya Zanzibar ya Januari 12, mwaka 1964.

Mapinduzi hayo yaliyoongozwa na mwasisi wa Zanzibar na Taifa la Tanzania, Hayati Abeid Amaan Karume yalifanikiwa kuung’oa madarakani utawala dhalimu wa Sultan na kuwawezesha kwa mara ya kwanza katika historia Waafrika walio wengine kujitawala ndani ya nchi yao wenyewe.

Yalikuwa ni Mapinduzi ya Zanzibar yaliyofungua njia ya kuzaliwa kwa Muungano wa Tanganyika na Zanzibar – miezi mitatu baada ya Mapinduzi hayo – Aprili 26, 1964.               
Naye Rais wa Zanzibar na Mwenyekiti wa Baraza la Mapinduzi Mheshimiwa Ali Mohamed Shein ametangaza kuwa kesho itakuwa Siku ya Mapumziko Tanzania Visiwani kusheherekea miaka 50 ya Mapinduzi ya Zanzibar.

Rais Shein alitangaza mapumziko hayo wakati alipohutubia wananchi kwenye Uwanja wa Michezo wa Amaan mjini Zanzibar katika kusherehekea miaka 50 ya Mapinduzi.

Mwisho.

Imetolewa na;
KURUGENZI YA MAWASILIANO YA RAIS
Ikulu,
es Salaam.
12 January, 2014

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...