Tuesday, April 30, 2013

YALIOJILI KWENYE BIRTHDAY KICK YA MTU MZIMA CHIDY BENZ@NEW MAISHA CLUB


 Chidy akimlisha keki joketi

 Hapa akimlisha keki moja kati ya mafuns wake katika siku yake zakuzaliwa

 Totozzilikuwa zaukweli na zakumwaga

 Makiss na ma hug yalihusika sana siku hiyooooo

 Hii hapa keki ya king kong chidy beeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeeenz

BABA MZAZI WA CHRIS BROWN, AMEZUNGUMZA KUHUSU MAPENZI YA CHRIS NA RIHANNA

.
Gazeti la New York Daily News limefanya Exclusive interview na baba mzazi wa mwimbaji staa Chris Brown na kutoa maoni yake kuhusu mahusiano ya kimapenzi ya mwanae na Rihanna RiRi.
Clinton Brown amesema “sioni maisha marefu kwa Chris Brown kuwa na Rihanna, sijawahi kupendezwa na kurudiana kwao, unajua ni lazima kwenye uhusiano wa kimapenzi uwe na mtu sahihi ambae ni hitaji la kweli na linaloweza kuwa lako kwenye maisha, lakini sio kama hivi”
Clinton amesema hapendi kutumia mifano lakini anadhani watu wameona mahusiano ya mastaa kama Whitney Houston, Michael Jackson, Amy Winehouse na wengine”
Kuhusu mrembo ambae angependa kuona anaolewa na mwanae, Clinton amemtaja Jordin Sparks kwa kusema “nimempenda Jordin, ni msichana mdogo lakini mwenye upeo mkubwa… ana akili na heshima”
.

DOTNATA AFUNGUKA BAADA YA KUGUNDUA KAWEKEWA SUMU KWENYE JUICE

http://1.bp.blogspot.com/-Xf5pb-ynWck/UFeJceXxqJI/AAAAAAAAIqE/ajgKiv17IsI/s1600/DOTNATA2.jpgMuigizaji wa filamu nchini Dotnata Rubagumya anadai kuwekewa sumu kwenye juice na mtu asiyemfahamu ambayo imemsababishia matatizo makubwa ya kiafya.
Amesema alianza kuhisi kupandwa na pressure ambapo alilazwa kwenye hospitali ya IMTU na kuambiwa imepanda hadi kufikia 284 huku wakimweleza huenda ni kwakuwa amenenepa sana.Baadaye alifanyiwa uchunguzi wa moyo kwenye hospitali ya Lugalo kabla ya kupelekwa TMJ kwa vipimo zaidi.

Anasema tatizo hilo lilimsabisha ashindwe kuhema, sauti kukata na mara nyingi alikuwa akitapika.
“Nimezidiwa usiku wa kuamkia Jumatano nikakimbizwa tena TMJ ndo sasa ikabidi wanichunguze kwa makini kwanini nakuwa hivi ndo wakagundua nimelishwa sumu takriban mwezi wa nane sasa huyo mtu aliyenipa sumu aliipitisha kwa njia ya juice,” amesema Dotnata ambaye kwa sasa ameokoka.
Akizungumzia sababu za kuwekewa sumu, Dotnata amesema:
“Kila mwanadamu ana mawazo jinsi anavyowaza katika akili yake labda hakupendezewa na mimi niendelea kuishi hivi, labda alifikiria akiniua mimi yeye hatokufa. Lakini natamka wazi kwamba sitokufa nitaishi ili niyasimulie mema ya Mungu. Nimejifunza mtu anaweza kuwa rafiki yako kumbe ndio mbaya wako siwezi kujua ni kwasababu gani, namwachia Mungu.”
Msikilize zaidi hapa.
NA BONGO CLAN BLOG

Wabunge waliosimamishwa warejea kwa ari Bungeni

Dodoma. Baada ya kutumikia adhabu ya kutohudhuria vikao vitano vya Bunge, wabunge watano wa Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema), jana waliingia bungeni wakionekana kuwa na ari mpya.
Wabunge waliosimamishwa Aprili 17 ni Mnadhimu Mkuu wa Kambi ya Upinzani Bungeni ambaye pia ni Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mbunge wa Iringa Mjini, Mchungaji Peter Msigwa.
Wengine ni Highness Kiwia (Ilemela), Ezekiel Wenje (Nyamagana), Joseph Mbilinyi ‘Sugu’ (Mbeya Mjini) na Godbless Lema (Arusha Mjini).
Jana asubuhi Mchungaji Msigwa alikuwa miongoni mwa wabunge waliowahi kuingia mapema ndani ya Ukumbi wa Bunge na kufuatiwa na Lissu muda mfupi baada ya kikao kuanza.
Ndani ya Ukumbi wa Bunge, Msigwa alipata nafasi ya kuuliza swali namba 115 lililokuwa liulizwe na Joyce Mukya kuhusu Kampuni ya Kamwene Woodworks . Kwa upande wake, Lissu aliomba mwongozo wa Spika kuhusu kukwama kwa Bajeti ya Wizara ya Maji.
Wabunge wengine haikujulikana sababu za kutofika jana licha ya kuwa adhabu yao ilikwisha tangu April 25 huku taarifa zikieleza kuwa Mbunge wa Arusha Mjini Godbless Lema alikuwa apelekwe mahakamani kujibu staka la uchochezi.
Mwananchi

Mitambo ya analojia Mbeya kuzimwa leo saa 6:00 usiku.

Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), imesema mitambo ya Analojia mkoani Mbeya itazimwa rasmi leo saa 6:00 usiku.
                                      Innocent Mungi, alisema Mkoa wa Mbeya.
Akizungumza na waandishi habari jana, Meneja Mawasiliano wa Mamlaka ya Mawasiliano Tanzania (TCRA), Innocent Mungi, alisema Mkoa wa Mbeya umekuwa wa mwisho katika hatua za kuzima mitambo hiyo, katika awamu ya kwanza.

Mungi alisema uzimaji wa mitambo ya analojia na kuhamia katika mitambo ya Digitali katika awamu ya kwanza, ulihusisha Mikoa ya Dar es Salaam, Dodoma, Tanga, Mwanza, Moshi na Arusha.

Alisema wakazi wa Mbeya walikwishafahamishwa kuhusu kuzimwa kwa mitambo hiyo kwa kufanya maandalizi yaliayohitajika ili kuepuka usumbufu ambao ungejitokeza.
 

Aliwataka Watanzania kuacha kunung’unika wanapokabiliwa na changamoto mbalimbali na hasa yanayohusu matatizo ya ving’amuzi na badala yake, wachukue za kutafuta ufumbuzi
Alisema baadhi ya Watanzania wamekuwa wakitumia muda mrefu kunung’unika na kushindwa kuchukua hatua za kukabiliana na changamoto zinazowakabili.

Shambulio lafanyika mjini Rome wakati serikali mpya ikiapishwa.


Serikali mpya nchini Italia imeapishwa na kumaliza hali ya iliyodumu kwa miezi kadhaa ya wasiwasi wa kisiasa, kufuatia uchaguzi mkuu wa mwezi Februari mwaka huu, ambao ulishindwa kutoa mshindi wa moja kwa moja.
Hata hivyo hafla ya kuapishwa kwa viongozi hao ilifunikwa na tukio la ufyatuaji risasi nje ya ofisi ya waziri mkuu ambapo maafisa wawili wa polisi walishambuliwa.
Watu walioshuhudia tukio hilo wamesema walimuona mwanaume mwenye silaha akifyatua risasi nje ya ofisi ya waziri mkuu katikati ya mji wa Rome, wakati baraza jipya la mawaziri likiendelea kuapishwa, umbali wa kilomita moja kutoka hapo, katika ikulu ya rais.

HAWA NDIO WATUMIAJI 11 WA MADAWA YA KULEVYA WENYE AKILI ZAID DUNIANI NA OBAMA YUMO.........!!!

STEVE JOBS
Imeripotiwa kwamba mwanzilishi wa Apple alitumia madawa kweny muhula wa kwanza kule Reed College in Portland, Oregon mwaka 1972. Tangu aach shule, Jobs amekuwa moja ya watu wenye mafanikio zaidi nchini America na dunia nzima kwa ujumla. Mwaka 1984,medali ya Taifa ya Technology nchini Marekani kutoka kwa rais wa kipindi hicho Ronald Reagan. Mwaka 2007, Fortune Magazine walimtaja kama mtu mwenye nguvu zaidi kwenye biashara na kisha mwaka 2011 gavana wa California Arnold Schwarzeneggerallimuweka kwenye California Hall of Fame.pia walimtaja kama CEO wa muongo (CEO of the decade) mwaka 2009 huku Forbeswakimuweka  #57 kwenye list ya “World’s Most Powerful People” mwaka huo huo.

richardbranson
Sir Richard Branson
Huku ile ‘Sir’ikimuweka kwenye list ya watu wanaoheshimiwa zaidi, hiyo sio sababu ya yeye kuwa kwenye hii list. Kinachomfanywa awekwe ni kwa sababu yeye anashika namba 236 kwenye watu matajiri zaidi duniani, mwanzilishi wa Virgin empire, ambayo inashughulika na vitu vingi kuanzia ndege mpaka maduka ya rekodi tofauti, simu,na ametengeneza utajiri wake from scratch.Sio tu kwamba a, he gets high with his 21-year-old son. alishasema mbele ya umati kwamba haoni tatizo kuhusu kutumia marijuana,na amefanya mchakato kuhalalisha utumiaji wake,na pia amesema kama ikiruhusiwa, atauza.

DADA WA NDIKUMANA APALILIA NDOA YA KAKA YAKE

 
Uwoya akiwa na mumewe Ndikumana enzi hizo.
Dada wa mchezaji wa Timu ya Rayon Sport, Ndikumana Katauti, Fatuma amefunguka kuwa licha ya migongano ya ndoa ya kaka yake lakini bado wanapendana. 
Akizungumza na gazeti moja la nchini Rwanda, Fatuma alisema kwamba hata ilivyotoka habari kuwa wifi yake Irene Uwoya amenaswa na Diamond alishtuka sana kwani yeye bado anaamini ndoa ya kaka yake ina uhai wa asilimia mia moja.

“Nilishangaa sana kuona gazeti limeandika kuwa wifi yangu amenaswa na Diamond, mimi naamini ndoa ya kaka yangu bado ipo hai,” alisema Fatuma.

MAGAZETI YA LEO APRILI 30, 2013

.

.
.
.

MH. KOMBANI: WATUMISHI WA UMMA WATAKIWA KUKUZA UCHUMI

6
Mh. Celina Kombani 
 
Na Georgina Misama-Maelezo
WAZIRI wa Nchi, Ofisi ya Rais Manejimenti ya Utumishi wa Umma Celina Kombani amewataka watumishi wa Umma kutimiza wajibu wao ipasavyo ili kukuza uchumi wa nchi.
Waziri Kombani amesema hayo katika ufunguzi wa mkutano wa siku mbili unaohusu majukumu ya watumishi wa Umma katika kutekeleza Mpango wa Maendeleo wa miaka mitano.
Alisema ubora au udhaifu wa utendaji wa serikali yoyote unahusishwa na ubora wa watumishi wa Umma.
“Uchumi hauwezi kukua bila watumishi wa umma kufanya kazi vizuri, katika kukuza uchumi tunategemea,kukua kwa uchumi pia kunategemea watumishi wa umma,” alisema Waziri Kombani.
Waziri Kombani alisema kwa kipindi cha miaka 50 ya Uhuru wa Tanzania bara, Tanzania imepiga hatua kubwa katika maendeleo, ingawa inakabiliwa na changamoto mbali mbali.
Pamoja na changamoto hizo, Waziri Kombani amesema Serikali imekuwa ikifanya juhudi mbali mbali ikiwemo, kupitia na kutafakari jinsi ya kufikia malengo ya maendeleo yake kwa haraka zaidi
Alisema changomoto zilizopo katika utumishi huo ni kuwa huduma zinawafikia wananchi kwa polepole, zisizo na ubora mfano kumekuwa na ongezeko la idadi ya wanafunzi wanaondikishwa katika shule ya msingi na sekondari, lakini kuna tatizo la ubora wa elimu.
“Tunapo sema uchumi wa nchi inatakiwa kumwangalia mtu wa ngazi za chini. Hivyo mkutano huu utakuwa unajadili changamoto zilizopo na nini kifanyike,” alisema.

Aidha aliongeza kuwa wakati mwingine wananchi wanalalamikia kuwepo kwa vitendo vya rushwa.
Hata hivyo Waziri Kombani ametoa wito kwa viongozi kutafuta majibu ya changamoto zilizopo, ikiwemo ongozeko la idadi ya watu, matumizi ya rasilimali na matumizi bora ya Teknolojia ya Habari na Mawasiliano (TEHAMA).
Mkutano huo wa siku mbili, unawashirikisha manaibu makatibu wakuu kutoka wizara mbalimbali, makatibu tawala wa mikoa, wakurugenzi wa Halmashauri, wakuu wa taasisi za elimu ya juu , sekta binafsi na wadau wa maendeleo kutoka ndani na nje ya Tanzania.

Monday, April 29, 2013

ASKARI MWANAUME ABAKWA NA WANAWAKE WANNE BAADA YA KUTEKWA

Askari mmoja mwanaume anadaiwa kutekwa kisha kudhalilishwa kijinsia na wanawake wanne kwa karibu wiki moja kabla ya kupigwa mawe na kutupwa katikati ya milima.

Mateso ya muathirika huyo mwenye miaka 25 yalianza pale alipopata lifti ya gari kuelekea mji wa Mutare nchini Zimbabwe.
Wanawake wawili na mwanaume mmoja walikuwa kwenye gari, Mercedes Benz, na, baada ya kuendesha kwa takribani saa moja kuelekea mji huo, dereva wa gari hilo akabadili mwelekeo wa safari hiyo.
Ndipo muathirika huyo akalalamika, alitishiwa kwa kisu.
Msemaji wa polisi wa Manicaland, Inspekta Msaidizi Nuzondiwa Clean, alieleza: "Baada ya kubadilishwa mwelekeo huo, mlalamikaji alihoji wapi walikokuwa wakielekea na walimweleza walikuwa wakienda kupata chakula.
 
"Askari huyo alitaka kushushwa, lakini dereva huyo akatoa kisu na kumtishia nacho. Mmoja wa abiria wanawake akamfunga kwa kitambaa cheusi machoni mtuhumiwa huyo."
 Kwa mujibu wa Nuzondiwa,watesi  hao  walimpeleka mlalamikaji kwenye nyumba isiyojulikana ambako walimvua nguo zote na kumpora simu yake na Dola za marekani 35.
 Watuhumiwa walimwamuru mtu huyo kulala na mmoja wa wanawake hao katika matukio kadhaa na alishikiliwa kati ya Aprili 19-23.
 
 Kisha akafungwa tena kitambaa machoni na kushushwa kwenye Milima ya Dangamvura ambako, kwa mujibu wa polisi, alipigwa mawe katika mguu wake wa kushoto, na kumsababishia majeraha makubwa.
 Watuhumiwa hao kisha wakawasha gari lao na kutokomea kusikojulikana.Askari huyo alitoa taarifa Kituo cha Polisi cha Sakubva

Mbowe amtwisha mzigo mzito Zitto

Tabora. Mwenyekiti wa Chadema, Freeman Mbowe amemwagiza Naibu Katibu Mkuu, Zitto Kabwe kuhakikisha chama kinapata ushindi katika majimbo mengi kwenye uchaguzi mkuu ujao.
Mbowe alisema chama chake kitahakikisha kinachukua majimbo ya Samwel Sitta, (Urambo Mashariki), Ismail Aden Rage (Tabora mjini) na Jimbo la Kaliua la Profesa Juma Kapuya, katika uchaguzi mkuu ujao mwaka 2015.
Akizungumza katika mkutano wa hadhara, Mbowe alimwagiza mbunge huyo wa Kigoma Kaskazini kuhakikisha kwamba majimbo hayo yanachukuliwa na Chadema katika uchaguzi mkuu ujao.
Alimtaka kufanya kampeni za mtaa kwa mtaa, nyumba kwa
hadi nyumba na mtu kwa mtu ili kuhakikisha kwamba wabunge hao wa sasa katika majimbo hayo hawachaguliwi tena na wananchi katika uchaguzi huo.
Katika mkutano huo uliofanyika kwenye Uwanja wa Shule ya Msingi Town School mjini Tabora, pamoja na mambo mengine alisema anazindua kampeni hiyo kwa ajili ya mikoa ya Tabora, Kigoma na Katavi ambapo Zito Kbwe alikabidhiwa jukumu la kuisimamia  kanda hiyo.
Aliwageukia polisi na kuwataka kukiunga mkono chama hicho ili kikifanikiwa kuingia madarakani kiweze kuwaboreshea mishahara yao kuliko ilivyo sasa akidai wanalipwa mishahara kiduchu ikilinganishwa na ugumu wa kazi yao.
“Nyie makamanda nanyi mmepigika kama sisi, sasa ninachowaomba tuungeni mkono kupambana na hawa CCM ili tuwakomboe wanyonge,” alisema Mbowe.
Awali Naibu Katibu Mkuu wa chama hicho Zitto Kabwe alisema Kanda ya Magharibi ina historia katika nchi kwa Mkoa wa Tabora kuwa kitovu cha mapambano ya uhuru wa nchi na Kigoma kuwa kitovu cha mapambano ya mageuzi.
Mwananchi

SHILOLE ALONGA BAADA YA KUNASWA AKILA BATA COCO BEACH NA BARNABA

MSANII wa filamu na muziki Bongo, Zuwena Mohamed ‘Shilole’ amefunguka kuwa hakuna kinachoweza kumtenganisha na msanii wa muziki wa kizazi kipya, Elius Barnabas ‘Barnaba’ kwani walikotoka ni mbali.

Shilole na Barnaba hivi karibuni walinaswa maeneo ya Coco Beach wakila bata lakini baada ya kuwaona mapaparazi wakizunguka kutafuta matukio, Barnaba alitimua mbio na kumuacha Shilole ambaye bila hiyana alitiririka: 

“Jamani mimi na Barnaba hakuna cha kututenganisha japokuwa watu wanachonga sana hata kuandikwa kwenye magazeti lakini bado tunaendelea tu, hivyo najua hakuna mtu anayeweza kututenganisha.”

PADRI AFUMANIWA NA MKE WA MTU! STORY NA PICHA KAMILI HIZI HAPA

KANISA Katoliki Jimbo la Moshi limeingia katika kashfa nzito baada ya padri wake, Father Urbanus Ngowi wa moja ya parokia zake kudaiwa kufumaniwa na mwanamke anayesemekana ni mke wa mtu, Ijumaa Wikienda lina sakata zima.
MSHANGAO: Father Ngowi akiwa ameduwaa baada ya kufumaniwa akiwa na mke wa mtu aliyejulikana kwa jina la kijamii la Mama P.
Sakata la fumanizi hilo linadaiwa kutokea Jumatatu ya wiki iliyopita chumbani kwa padri huyo, Marangu Wilaya ya Moshi  Vijijini ambako Father Ngowi inasemekana alikutwa ‘laivu’ akiwa na mwanamke huyo aliyejulikana kwa jina la kijamii la Mama P.
Pamoja na kunaswa huko, vyanzo havijaeleza humo chumbani wawili hao walikuwa wakifanya nini!
Habari zinadai siku ya tukio, mwanamke huyo aliingia nyumbani kwa padri huyo ambapo baadhi ya ndugu wa mumewe walikuwa wakimfuatilia baada ya madai yaliyokuwepo kwamba ana ukaribu wenye maswali mengi na mtumishi huyo wa Mungu.
“Unajua siku nyingi ilivuma kwamba Mama P na Father Ngowi wana ukaribu wenye maswali mengi, mume wake alifuatilia na kubaini ni kweli lakini akashindwa kuutenganisha ukaribu wao,” kilidai chanzo.

MSAMAHA: Father Ngowi akijaribu kuomba samahani baada ya kufumaniwa.
Chanzo kikaendelea kudai kwamba baada ya kuona mkewe amejikita kwa mtumishi wa Mungu, mumewe (jina tunalo) alinyoosha mikono juu na kumwachia Mungu.
Chanzo: Sasa siku hiyo baada ya ndugu wa mume kumfuatilia mpaka anaingia kwa Father Ngowi, wakaona ni bora watafute mpigapicha ili kupata picha za tukio ambazo zitakuwa ushahidi siku za mbele.
“Walipompata wakazama ndani, sekeseke likaanzia hapo. Walimkuta mwanamke huyo na mtumishi wa Mungu wapo kitandani."

MAGAZETI LEO JUMATATU APRIL 29, KURASA ZA MWANZO NA MWISHO ZA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.

MIAKA 13 YA LADY JAY DEE KWENYE MUZIKI KUDONDOSHA BONGE LA PARTY

TAARIFA KWA VYOMBO VYA HABARI
Katika mwaka huu 2013, Inatimia miaka13 tangu nianze kazi ya muziki.
Nashukuru MUNGU tukopamojanapia, nashukuru umma wa Tanzania kwa kuendelea ku support muziki wa Tanzania nakunipa nguvu mimi kama msanii.
Nashukuru vyombo vyotevya habari vinavyoshiriki kikamilifu kukuza na kulinda sanaa ya Tanzania bila kujali maslahi binafsi.
Tumeandaa sherehe kubwa na nzuri ya miaka 13 ya LADY JAYDEE, katika muziki. Na mdhamini mkuu kwa upande wa media ni East Africa TV. Shereheyamiaka 13 ya Lady Jay Dee katika muziki itaambatana na uzinduzi wa album yangu ya sita inayokwenda kwa jina la NOTHING BUT THE TRUT ambayo ina jumla ya nyimbo 10.

Katika sherehe hizo pia kutakuwa na show ya nyimbo zote bora za Jay Dee nikishirikiana na baadhi ya wasanii wenzangu hapa nchini.
Sherehe zitafanyika Ijumaa tarehe 31 May 2013.

Nawakaribisha wote tufurahi pamoja
Na Mungu awabariki

AY Kuachia "JIPE SHAVU" Jumatano Hii ..


!!! YEEESAYAAH !!! 
Mwanamuziki kutoka Tanzania, Ambwene Yessayah a.k.a AY au pia unawweza kumuita "Zee La Commercial" anataraji kuachia ngoma yake nyingine hivi karibuni ...
AY ambae bado machoni mwako anafanya vizuri na video SPEAK WITH YA BODY, PARTY ZONE na MONEY zinazopigwa katika televisheni kubwa duniani kama Channel O na TRACE TV ya Ufaransa soon anaachia JIWE hilo litakalofahamika kama JIPE SHAVU ...
JIPE SHAVU is the next single from AY akiwa amemshirikisha mshkaji wake wa karibu akijulikana Fid Q [that Illest Hip-Hop dude from MWANZA City] ...
Hapa "Zee La Commercial" na hapa pembeni ni "Zee La Hardcore" ... JIPE SHAVU ...
Dundo hilo according to AY, limefanywa na Producer Q ikiwa ni katika studio za MPO AFRICA zilizopo maeneo ya mikocheni ...
AY anasema ngoma hiyo itaachiwa rasmi jumatano hii katika sehemu tofauti ... As to fans wakae tayari kupokea kazi nyingine bora kabisa kutoka kwake ...
AY na rapper Fid Q waliwahi kufanya ngoma mbali mbali nzuri za pamoja ikiwemo USIJARIBU yenye video yake pia ...
Let's wait for JIPE SHAVU afu tuone ...

"UREMBO SIYO KIPAJI NA SI KILA MWANAMKE MZURI ANAWEZA KUIGIZA"...JACKLINE WOLPER

Muigizaji Jacqueline “Jackie” Wolper amewashangaa wanaodhani kuwa urembo wa mwanamke ni mbadala wa kipaji hasa katika sanaa ya maigizo.

Alisema urembo ni moja ya sifa ya mwanamke lakini kamwe hauwezi kumfanya asiye na kipaji kuwa nacho.
 
“Ukiwa mrembo ni bora zaidi,kwa kuwa itamfanya avutie kwenye movie,lakini pamoja na hayo ni lazima awe na uwezo wa kuigiza kulingana na kipande husika”alisema Wolper.
 
Wolper aliendelea kulalama kuwa kila mtu akijona ana sura ya kuvutia na umbo zuri basi anajua anaweza kuigiza ndio maana matokeo yake wanafanya vitu sivyo na mwisho wake wanaacha fani kabisa.
 
Alifafanuwa kuwa kuigiza ni zaidi ya urembo hivyo yeyote ambaye anafikiri anaweza kufanya kazi hii kwa uzuri wa sura na umbo ajaribu kama hakuchemka.

Source: Mwananchi

Sunday, April 28, 2013

GARI JIPYALA MILIONI 35 ALILONUNUA NEY WA MITEGO PAMOJA NA BASTOLA HAPA

Mwaka 2013 ni mzuri kwa rapper Nay wa Mitego. Licha ya kuwa na hit single hewani, Muziki Gani aliyomshirikisha Diamond, rapper huyo amenunua ndinga mpya aina ya Mark X yenye thamani ya shilingi milioni 35. Kama hiyo haitoshi, hitmaker wa Nasema Nao, amejihami pia kwa kununua bastola.
29ddba2cae6b11e2aeda22000a1f973b_7


Nay akiwa na bastola yake
Nay akiwa na bastola yake
Nay ameshare picha hizo kwenye Instagram na Facebook ambapo miongini mwa picha za gari lake ameandika, ‘My new car. Mark X, Zic z wat I nid.” Mwaka huu Nay ametumiwa kwenye show nyingi za Airtel na Vodacom ambazo huenda zimemwingizia mkwanja wa kutosha.
23a19536ae6e11e2942122000aaa0535_7

82d44f72ae6d11e2a2ce22000a1fa411_7

a2364980ae6b11e2b9ed22000a1f8cd8_7

d07e1cfaae6b11e2b09522000a1f9363_7

dc3c1784ae6d11e28c1022000a9e08e0_7


MBUNGE LEMA AZUILIWA KUPIGA MSWAKI WALA KUNYWA CHAI AKIWA MAHABUSU...... !!

TUKIO la kukamatwa na kuwekwa mahabusu kwa Mbunge wa Arusha Mjini, Godbless Lema (CHADEMA), kwa madai ya uchochezi, limeibua sura mpya baada ya Chama Cha Mapinduzi (CCM) kutajwa kuwa nyuma ya mkakati huo,
 
Lema ambaye bado anaendelea kusota rumande siku ya tatu baada ya kunyimwa dhamana, ameanza kufanyiwa vituko na Jeshi la Polisi baada ya jana asubuhi mkewe kuzuiliwa asimpe mswaki wala chai.
 
Mbunge huyo alikamatwa kutokana na amri ya Mkuu wa Mkoa wa Arusha, Magesa Mulongo, aliyedai kuwa aliwachochea wanafunzi wa Chuo cha Uhasibu Arusha kumzomea kiongozi huyo na kupopoa gari lake kwa mawe.
 
Hata hivyo, siku moja kabla ya kukamatwa Lema aliwaonesha waandishi wa habari ujumbe mfupi wa simu ya kiganjani aliyotumiwa na Mulongo akimtishia kuwa atamfungulia kesi yoyote anayoitaka.
 
“Umeruka kihunzi cha kwanza, nitakuonesha kuwa mimi ni serikali, ulikojificha nitakupata na nitakupa kesi ninayotaka mimi,’’ ulisomeka ujumbe huo uliotumwa kupitia simu namba 0752 960276 ambayo Lema alidai ni ya Mulungo.

MSANII SIZE NANE ALILIA BIKRA YAKE HADHARANI...!!

Mwanamuziki  aliyeitikisa vilivyo Kenya kabla ya kuokoka na kuachana na muziki wa kidunia, mwanadada Size 8 sasa ameanza kufunguka katika interview kwenye vituo mbali mbali vya redio na Tv kuhusiana na maisha mapya ya kidini.

Kati ya  mambo yote ambayo Size 8 amekuwa akiyaongelea, ni moja tu ambalo amekuwa akilitilia mkazo kwa kumaanisha kuwa linamsikitisha zaidi .....Jambo hilo ni lile la kupoteza BIKRA YAKE.....
Size 8 ameziambia media kuwa  "Najutia sana kupoteza bikra yangu. Ninaamini kuwa kijana anatakiwa kujilinda na kujizuia kufanya ngono katika ujana wake wote mpaka atakapo pata kibali toka kwa Mungu."

KIONGOZI WA KANISA AZIKWA AKIWA HAI

26 46e3f
Msaidizi wa zamani wa Padri (Katekisita) katika Kigango cha Kanisa Katoliki Kijiji cha Mkwajuni, Florian Mwamosi (70) amekufa baada ya kuzikwa akiwa hai katika kaburi moja na mtu anayedaiwa kumuua kwa njia ya kishirikina.
Tukio hilo limetokea katika Kitongoji cha Maweni kijijini hapo wilayani Chunya mkoani Mbeya.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Mbeya Diwani Athumani alikiri kutokea kwa tukio hilo akieleza kuwa lilitokea saa 9:00 mchana katika kijiji hicho cha Maweni Mkwajuni wilayani Chunya.

"Marehemu aliuawa na wananchi wenye hasira kali kwa kupigwa na mawe kwa tuhuma za kuhusika na uchawi na kusababisha kifo cha Peter Robert," alisema.
Kamanda Athumani alisema kuwa uchunguzi kuhusiana na tukio hilo unaendelea na kwamba wahusika wote wa tukio hilo wamekimbia na kuzihama nyumba zao, hivyo polisi wanaendelea na msako wa kuwatia mbaroni watuhumiwa na kwamba tayari kaburi hilo limefukuliwa jana kutenganisha maiti hizo.

WEMA AFUNGUKA INSTAGRAM BAADA YA KUSOMA MOJA YA GAZETI KWAMBA ANA BEEF NA LULU

BEYONCE AWAPIGA MKWARA WAPIGA PICHA, HIKI NDO ALICHOKISEMA

Baada ya kukerwa na picha alizopigwa wakati wa tamasha la SuperBowl ambazo anaona zilimdhalilisha, mwanamuziki Beyonce amefikia maamuzi magumu ya kuwakataa wapiga picha

Kwa mujibu wa barua pepe iliyotumwa kwenye ukurasa wa facebook wa Umoja wa Wapiga picha za Muziki imeeleza kuwa mwanamuziki huyo haitaji tena wapiga picha katika shoo za ziara yake ya sasa ya Ulaya

Badala yake amekuwa akitoa picha rasmi zilizopigwa kutoka katika shoo na wapiga picha maalum aliowakodisha.

MAGAZETI YA LEO APRIL 28 2013 KURASA ZA MWANZO NA MWISHO

.

.
.
.

Mawaziri, wabunge CCM warushiana 'makombora'



Wabunge wa Chama cha Mapinduzi (CCM), jana walishambuliana huku waliokuwa mstari wa mbele kuikosoa serikali katika vikao vya bajeti vinavyoendelea mjini Dodoma wakituhumiwa kukiua chama na kukipa nguvu Chama cha Demokrasia na Maendeleo (Chadema).

Kikao hicho ambacho kilikuwa chini ya Mwenyekiti wake, Waziri Mkuu, Mizengo Pinda, kilifanyika katika ukumbi wa Bunge wa Pius Msekwa mjini Dodoma.

Pinda alianza kwa kuweka hoja mezani akitaka wabunge wa CCM kuchangia Sh.100,000 kila mmoja kwa ajili ya kuwezesha ushindi katika uchaguzi mdogo wa madiwani unaotarajiwa kufanyika katika kata 26 nchini.

Hoja hiyo iliungwa mkono na wabunge hao, lakini alisimama Mbunge wa Mwibara, Alphaxard Khangi Lugola, akihoji kulikoni wanaosaidiwa na chama wakawa madiwani ili hali wabunge walio na kesi mahakamani wakiachwa kugharamia kila kitu wenyewe.
“Si unajua nyoka wa shaba (Lugola), ana kesi mahakamani, sasa ndiyo maana akaamua kuhoji, iweje yeye hasaidiwi na chama wakati huo huo anaambiwa akisaidie chama,” alisema mmoja wa wabunge aliyekuwa ndani ya kikao hicho.

Saturday, April 27, 2013

MGANGA AELEZEA ISHU YA DIAMOND KUNG'ANG'ANIA MAITI YA BI.KIDUDE KWA NIA YA KUIBA NYOTA YAKE

Baada ya msiba wa Bi Kidude kumalizika, hivi karibuni ziliibuka taarifa kuwa mwanamuziki Nasibu Abdul ‘Diamond’ alibaki peke yake na mwili wa marehemu chumbani kwa ajili ya kuchota nyota ya Bi. Kidude.
Leo tunaye Dr Salum Mkumba ambaye ataeleza kwa kirefu tafsiri ya kitendo alichokifanya Diamond.
Funguka: Dr Mkumba asalam aleikum, karibu ndani ya nyumba kubwa ya magazeti Pendwa Tanzania, Global Publishers Ltd.
Dr Mkumba: Waaleikum salaam, ahsanteni nashukuru. Mimi leo nina jambo ninataka niliweke sawa.
Funguka: Liweke sawa, sisi pamoja na wasomaji wetu wa Risasi Jumamosi tunakusikiliza.
Dr Mkumba: Nataka kuweka sawa juu ya suala la nyota, mtu akifariki huwa anakwenda na nyota yake sasa nimeshangaa kusikia Diamond alikwenda kuchukua nyota ya marehemu.
Funguka: Sasa Diamond alipobaki peke yake chumbani na mwili wa marehemu ilikuwa ina maana gani?
Dr Mkumba: Pale alikuwa anajaribu kujisafisha tu katika jamii, hakuna cha ziada.
Funguka: Unaposema anajisafisha, kwani amechafuka?
Dr Mkumba: Eee! Kwani hujui? Amenaswa na mke wa mtu hotelini, skendo za wanawake tofauti zimekuwa zikimtafuna kila kukicha.
Funguka: Unaposema alikuwa anajisafisha una kitu gani cha kushika mkononi?
Dr Mkumba: Surat Nnajimi Sura ya 39 imezungumza kwa kirefu ila tafsiri yake ipo hivi; hakuna anachokichuma mwanadamu kwa marehemu ila marehemu anategemea kuombewa dua na mtu mzima.
Funguka: Kwa hiyo ina maana vile alivyofanya Diamond ni kazi bure?
Dr Mkumba: Nakwambia hakuna cha maana zaidi ya kujisafisha.
Funguka: Sasa una mshauri nini Diamond?
Dr Mkumba: Amrudie mwenyezi Mungu kwa kufanya ibada ya kweli.
Funguka: Vipi kuhusu suala la kujenga msikiti ambalo Diamond alitangaza kuwa ana mpango huo?
Dr Mkumba: Hapo ndiyo kabisa, ajenge tu lakini haisaidii kitu sababu ukijenga nyumba ya ibada inatakiwa utumie fedha ambazo umezipata kihalali katika njia safi.
Funguka: Kwani fedha zake hajazichuma kwa njia safi?
Dr Mkumba: Kiimani yetu ya Kiislam muziki siyo halali hivyo fedha anayoipata kwenye muziki haiwezi kuwa halali.
Funguka: Tunashukuru, karibu tena siku nyingine.
Dr Mkumba: Haya Ishallah!

FATAKI LANASWA LIVE NA MWANAFUNZI GESTI WAKIWA UCHI WA MNYAMA WAKILA URODA..!!



MfanyabiAshara ‘alwatani’ Bongo, mkazi wa jijini Dar, Allain Tajiri amekumbwa na skendo nzito baada ya kufumaniwa na mwanafunzi wa sekondari wa kidato cha pili mwenye umri wa miaka 16.
Tukio hilo la kusikitisha lilitokea Jumatano ya Aprili 24, mwaka huu katika chumba namba 107 kwenye gesti iitwayo Jamboz iliyopo Kinondoni jijini Dar.

Habari za uhakika zilieleza kuwa tukio hilo lilikuwa ni mtego baada ya walezi wa denti huyo kunasa mawasiliano ya mfanyabiashara huyo akimrubuni binti yao.


Katika mawasiliano hayo, Tajiri alimtaka denti huyo wa sekondari moja iliyopo Kibamba, Dar (jina linahifadhiwa kwa sababu maalum za weledi wa uandishi wa habari), wakutane kwenye gesti hiyo kwa ajili ya kuimomonyoa amri ya sita.

Baada ya walezi hao kuufuma ujumbe kwenye simu ya binti yao, walimuwekea doria bila mwenyewe kujijua na ulipokaribia muda waliokubaliana kukutana gesti, denti huyo aliaga anakwenda ‘tuisheni’.

AIBU ! KIJANA ANASWA AKIMNAJISI NA KUMLAWITI MBUZI HADHARANI....!!

Katika  hali  ya  kushangaza, jamaa  mmoja  nchini  Nigeria  amenaswa  live  akivunja  amri  ya  sita  na  Mbuzi ....
Baada  ya  kufamaniwa  na  wanachi, mwanaume  huyo  alipewa  kichapo  kikali  na  kufangashwa  na  mbuzi  huyo  hadi kituo  cha  polisi.... 
Maswali  yenye  utata  kuhusu  tukio  hilo:
1. Kuna  faida  gani  au  starehe  gani  ya  kufanya  mapenzi  na  mnnyama....
2..Viungo  vya  mwanaume  ni  vikubwa  sana  ukilinganisha  na  vile  vya  mbuzi...huyu  jamaa  aliwezaje....Bora  angechukua  punda  kuliko   kumuonea  mbuzi  wa  watu..!!! 
Niimani  yetu  kwamba sheria  itamfundisha  adabu

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...