Saturday, October 07, 2017

MAREKANI YAIONDOLEA VIKWAZO SUDAN

Marekani imeiondolea vikwazo Sudan ikisema taifa hilo la Afrika lilikuwa limeanza kuangazia maswala kuhusu kukabiliana na ugaidi pamoja na ukiukeaji wa haki za kibinaadamu dhidi ya raia wanaoishi katika jimbo la Darfur.

Uamuzi wa kuiondolea vikwazo na kusitisha vikwazo vya kiuchumi wa taifa hilo unajiri baada ya utawala wa Trump mwezi uliopita kuliondoa taifa hilo katika mataifa ambayo raia wake wamewekwa vikwazo vya kusafiri.

Sudan ndio taifa la pekee ambalo liliondolewa katika orodha hiyo. Lakini uamuzi huo unaviacha vikwazo vingine kuendelea kwa sasa ikiwemo vile dhidi ya watu binafsi walio na agizo la kukamtwa kufuatia unyanyasaji uliofanyika katika eneo la Darfur.

Friday, September 29, 2017

OFISI YA BUNGE YAKANUSHA MBOWE KUNYANG'ANYWA GARI

Ofisi ya Bunge imekanusha kumnyang’anya gari mbunge Freeman Mbowe na kuwa linatafutiwa kibali kutoka kwa Katibu Mkuu Kiongozi ili Mbowe akalitumie Nairobi.

GAZETI LA MWANANCHI LATAKIWA KUOMBA RADHI

Serikali ya mapinduzi Zanzibar imewaagiza Wahariri wa Gazeti la Mwananchi kuomba radhi Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati (ZURA) ndani ya saa 24 kuanzia saa 9:00 Alasiri ya jana Septemba 28, 2017.

Kwa mujibu wa taarifa hiyo iliyotolewa naNaibu Mkurugenzi Idara ya Habari (MAELEZO) Zanzibar, Dk. Juma Mohammed Salum ambapo amesema iwapo wahusika hawatafanya hivyo hatua kali za kisheria zitachukuliwa dhidi ya gazeti hilo la Mwananchi.

Hatua hiyo imekuja baada ya Serikali kudai gazeti hilo la Mwananchi linalochapishwa na kampuni ya Mwananchi Communications Limited Septemba 27, 2017 kuchapisha makala katika Ukurasa wake wa 16 yenye kichwa cha habari kisemacho “Siri ya nini Zabuni ya Mafuta Zanzibar”?

Salum amefafanua kuwa makala hiyo licha ya kujenga picha kwamba hakuna uwazi katika Zabuni ya uletaji Mafuta Zanzibar,msingi na maudhuhi ya Makala yenyewe kwa ujumla ni upotoshaji wa makusudi kwa nia ya kuipaka matope Serikali ya Mapinduzi Zanzibar.

Taarifa hiyo pia licha ya kuwataka wahariri wa gazeti hilo kuomba radhi pia imefafanua ukweli wa mambo yalivyo kwa sasa ambapo Serikali, kupitia Mamlaka ya Udhibiti wa Huduma za Maji na Nishati Zanzibar (ZURA) tayari imeanzisha mfumo mpya wa uletaji Mafuta Zanzibar tangu Septemba Mosi, 2017.

Saturday, September 09, 2017

WATOTO WALIOPO TUMBONI WAKUTWA NA MATATIZO YA MOYO

Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto wa Taasisi ya Moyo ya Jakaya Kikwete (JKCI), Naiz Majani.
 
JUMLA ya wajawazito 35 wamefamyiwa  uchunguzi wa kipimo cha magonjwa ya moyo kwa watoto wachanga waliopo tumboni mwa mama zao (FETAL ECHOCARDIOGRAPHY) ili kujuwa kama wanamatatizo ya moyo au la.

Majibu ya kipimo hicho yalionyesha kuwa kati ya hao watoto watano walikutwa na matatizo ya moyo jambo ambalo litawawezesha   kupata matibabu mapema pindi watakapozaliwa.

Hayo yamesemwa na Daktari bingwa wa magonjwa ya moyo kwa watoto kutoka Taasisi ya Moyo Jakaya Kikwete (JKCI) Naiz Majani wakati akiongea na waandishi wa habari hivi karibuni.

Dkt. Naiz alisema kipimo hicho hakina madhara yoyote kwa mama na mtoto na kina  uwezo wa kugundua endapo mtoto ameathirika na ugonjwa wa moyo na hivyo kumuandaa mama mjamzito kwaajili ya uzazi salama.

“Mojawapo ya dalili za mama mjamzito ambazo zinaweza pelekea kupata mtoto mwenye  tatizo la ugonjwa wa moyo ni pamoja na ugonjwa wa kisukari,shinikizo la damu,matumizi ya dawa za muda mrefu,mimba ya mapacha, kuwepo na mtu mwenye tatizo la moyo katika familia na mimba pandikizi”.

“Ninawaomba kina mama wajawazito wenye moja ya dalili nilizozitaja waje tuwafanyie kipimo hiki  kipindi  ambacho mimba zao zitakuwa na umri wa kati ya miezi minne hadi saba hii itawasaidia  kugundua afya za watoto wao na kuepuka na  vifo vya mara  baada ya kuzaliwa vinavyotokea kipindi cha mwezi mmoja hadi  mwaka”, alisema Dkt. Naiz.

Alizitaja changamoto wanazokabiliana nazo kuwa ni pamoja na uelewa mdogo wa kinamama wajawazito juu ya kipimo hicho kwa kufikiria kuwa kinamadhara  jambo ambalo siyo kweli kwani kipimo hicho hakina  madhara yoyote kiafya.

Taasisi ya Moyo  Jakaya Kikwete (JKCI) ilianza kutoa huduma hiyo tangu mwezi wa tatu mwaka huu ili kupunguza  vifo vya watoto vinavyotokana na  magonjwa ya moyo mara baada ya mtoto kuzaliwa.
Na Sweetbert Hudson.

Wednesday, September 06, 2017

WANAFUNZI 917,072 KUFANYA MTIHANI WA DARASA LA SABA LEO

Baraza la Taifa la Mitihani nchini (NECTA) limesema maandalizi ya kuanza mtihani wa Taifa wa darasa la saba utakaofanyika leo jumatano Septemba 6 na kesho alhamisi ya Septemba 7 yamekamilika.

Akizungumza na wanahabari kuhusu maandalizi hayo, Katibu Mtendaji wa NECTA, Dk. Charles Msonde. Tayari mitihani imesafirishwa katika maeneo yote nchini na kinachosubiriwa kwa sasa ni kuanza kwa mtihani.

“Leo na kesho katika shule zetu 16,583 za msingi nchini kutakuwa ana mtihani wa kumaliza elimu ya msingi, watahiniwa ni 917,072 wataufanya wavulana wakiwa 432,744 sawa na asilimia 47.19%, wasichana ni 484,328 sawa na asilimia 52.81%, mwaka jana watahiniwa walikuwa 795,761.

EMIRATES TANZANIA YAPATA BOSI MPYA

Uongozi wa shirika la ndege la kimataifa la Emirates umemteua Bwana Rashed Alfajeer kuwa meneja mkuu mpya wa shirika hilo nchini Tanzania.

Kwa mujibu wa taarifa ya msemaji wa shirika hilo nchini Tanzania inasema, Bwana Alfajeer, kutoka katika nchi za Falme za Kiarabu, atakuwa na jukumu la kusimamia shughuli zote za Emirates za kibiashara, wateja na mizigo kwenye soko.

"Nina furaha kwa kuchaguliwa kuwa meneja mpya wa Emirates nchini Tanzania na ninatarajia kufanya kazi na timu ya ndani, pamoja na washirika wetu wa biashara katika kuendeleza biashara zaidi ya Emirates kwenye soko," alisema Alfajeer.

"Mtazamo wangu utakuwa kuendelea kuwapa wateja wetu wa Tanzania huduma bora kulingana na thamani ya pesa, tunapowaunganisha kwenye maeneo zaidi ya 150 ulimwenguni kote," aliongeza.

Bwana Alfajeer alijiunga na Emirates mwaka 2013 kama sehemu ya mpango wa Emirates kama msimamizi wa Taifa wa Uendeshaji wa Biashara. Tangu wakati huo, amefanya kazi za biashara nchini Sri Lanka kabla ya kuchukua nafasi ya Meneja wa Wilaya huko Dammam, Saudi Arabia mwaka 2015.

Emirates hufanya safiri mara moja kwa siku kati ya Dar es Salaam na Dubai na ndege kubwa aina ya Boeing 777.

HASHIM RUNGWE ASHIKILIWA NA POLISI

Aliyekuwa mgombea Urais katika Uchaguzi Mkuu wa mwaka 2015, Hashim Rungwe anashikiliwa na polisi kwa siku nne sasa.

Rungwe ambaye ni Mwenyekiti wa Chama cha Chaumma anashikiliwa katika Kituo Kikuu cha Polisi cha Kanda Maalumu ya Dar es Salaam. Mwanasiasa huyo anashikiliwa akituhumiwa kughushi nyaraka.

Kamanda wa Polisi wa kanda hiyo, Lazaro Mambosasa amesema jana Septemba 5 kuwa, Rungwe anashikiliwa kituoni hapo kwa siku nne.

Hata hivyo, Kamanda Mambosasa hakutaka kuingia kwa undani kuhusu suala hilo akisema hana taarifa za kutosha.

JAJI MARAGA AMJIBU UHURU KENYATTA

JAJI Mkuu David Maraga amejibu shutuma kutoka kwa Rais Uhuru Kenyatta na viongozi wengine wa Chama cha Jubilee, kufuatia uamuzi wa  Mahakama ya Juu kufuta matokeo ya uchaguzi wa urais.

Viongozi wa Jubilee wamemkosoa Maraga wakidai anatumiwa na upinzani kutoa maamuzi yanayoupendelea muungano wa NASA, na wameapa  kuupitia uamuzi huo wa mahakama wakati uchaguzi utakapomalizika.

“Mimi si mwanasiasa na ninafanya kazi kwa kuzingatia misingi ya kiapo cha utii nilichoapa kuwatumikia Wakenya. Siungi mkono Jubilee wala NASA au  mtu yeyote,” alisema Jaji Maraga katika taarifa yake fupi jana.

Rais Kenyatta mwishoni mwa wiki iliyopita alimkosoa Maraga akimwita ‘mkora’, kwamba ‘alipindua’ matakwa ya mamilioni ya Wakenya waliomchagua.

Kufuatia vitisho hivyo, ambavyo vimelaaniwa vikali na wanaharakati na katika mitandao ya jamii, Maraga ambaye ni mzee wa Kanisa la Sabato (SDA),  alisisitiza kuwa anamwogopa Mungu pekee.

“Ninafuata katiba yetu. Nendeni mkaendeshe uchaguzi na iwapo mtu anapinga, lete shauri ukiwa na ushahidi mzuri na nitalifanyia kazi ipasavyo.  Kumbuka namhofia Mungu pekee,” alisema Maraga ambaye anaongoza mfumo wa mahakama

Friday, August 18, 2017

MAPACHA WALIOSHIKANA WAFARIKI MUHIMBILI

Pacha walioshikana ambao walikuwa wamelazwa katika hospitali ya taifa ya Muhimbili mjini Dar es Salaam wamefariki kwa mujibu wa msemaji wa hospitali hiyo.

Pacha hao waliokuwa wakifanyiwa vipimo ili kuwaanda kwa upasuaji walifariki siku ya Jumanne kulingana na bi Neema Mwangomo. Watoto hao walizaliwa wilayani Kilosa katika eneo la Morogoro. Familia yao ilitoka katika kijiji cha Chaumbele.

Akizungumza na mwandishi wa habari hii, Bi Mwangomo alisema kuwa wataalam watatoa maelezo katika wakati ufaao.

Pacha hao walioshikana chini ya kifua na tumboni walikuwa wakitumia ini moja na mishipa ya moyo lakini kila mmoja alikuwa na tumbo lake.

Awali daktari wa watoto Dkt Zaituni Bokhary alitumai kwamba pacha hao wanaweza kutenganishwa watakapofikisha umri wa miaka sita.

MUGABE: 'WALIOWAUA WAZUNGU HAWATASHITAKIWA'

Rais Robert Mugabe, ameuambia umati wakati wa sherehe za siku ya mashujaa jijini Harare Jumatatu wiki hii kuwa watu waliowaua wakulima wa kizungu wakati wa mabadiliko ya sheria ya ardhi nchini Zimbabwe hawatashtakiwa.

“Ndiyo, tuna wale waliouawa wakati wakipinga ukoloni. Hatuwezi kuwashtaki wale waliowaua wazungu. Je, tutawashtaki vipi?” alisema Mugabe.

Wakati wa ukoloni, ardhi nzuri ilitengwa kwa wazungu, lakini mwaka 2000, Mugabe aliongoza kutwaliwa kwa ardhi hiyo kutoka kwa wakulima 4,000 wa kizungu.

Rais Mugabe awali alikiri kuwa mifumo ya ardhi ya nchi hiyo ilishindwa na mwaka 2015 alisema: “Nafikiri mashamba tuliyowapa watu wetu ni makubwa, hawawezi kuyasimamia.”

Kutwaliwa ghafla mashamba kutoka kwa wakulima wazungu, inaonekana kuwa sababu kuu ya kuporomoka kwa uchumi wa Zimbabwe tangu mwaka 2000.

DANGOTE: 'NIKIINUNUA ARSENAL NITAMFUKUZA WENGER'

Mfanyabiashara tajiri raia wa Nigeria Aliko Dangote, ambaye anaorodheshwa kuwa mtu tajiri zaidi Afrika, amesema kuwa atamfuta kazi meneja wa Arsenal, Arsene Wenger, ikiwa atafaulu kuinunua klabu hiyo ya Uingereza, kwa mujibu wa shirika la Bloomberg.

Wakati wa mahojiano na shirika hilo, Dangote alisema kuwa atajaribu kuinunua klabu hiyo, wakati ujenzi wa kiwanda chake cha kusafisha mafuta cha gharama ya dola bilioni 11 mjini Lagos utakapokamilika.

Bw. Dangote anasema amekuwa shabiki wa Arsenal tangu mwaka 1980.

Wenger ni mmoja wa mameneja wa kandanda wanaosifika sana barani Ulaya na hivi majuzi, alisaini mkataba wa miaka miwili na kuendelea kuwa na klabu hiyo kwa zaidi ya miongo miwili.

Kuna maoni tofauti kutoka kwa wafuasi wake, wengine wakisema kuwa klabu hiyo inahitaji meneja mpya ili kiweze kurejea hadhi yake.

Friday, August 11, 2017

NI UHURU KENYATTA TENA KENYA

Mwenyekiti wa Tume ya Uchaguzi (IEBC), Wafula Chebukati amemtangaza Rais Uhuru Kenyatta kuwa mshindi wa uchaguzi wa urais.

Chebukati amemtangaza Kenyatta chama Jubilee kwa kupata kura 8,203,290 sawa na asilimia 54.27 ya kura zote zilizopigwa huku mpinzani wake, Raila Odinga aliyekuwa anawakilisha Muungano wa vyama vya upinzani (NASA), akipata kura 6,762,224 sawa na asilimia 44.74 ya kura zote zilizopigwa.

Aidha, watu waliojitokeza kupiga kura walikuwa 15,073,662 sawa na asilimia 78.91 kati ya milioni 19 waliojiandikisha kupiga kura huku kura zilizoharibika zikiwa 399, 935.



Licha ya mchuano mkali ambao ulionyesha tangu awali Kenyatta akiongoza lakini Raila na wafuasi wake waliamini ameshinda uchaguzi huo huku akitaka tume imtangaze kuwa mshindi wa urais.



SERIKALIYAZIMBAMBWEYAKATAAWAFUNGWA KUPIGA KURA


Serikali ya Zimbabwe imekataa ombi la chama cha MDC-T la kuwaruhusu wafungwa kupiga kura katika Uchaguzi Mkuu wa nchi hiyo ambao utafanyika mwakani 2018.

Taarifa ambayo imetolewa na Katibu Mkuu wa Wizara ya Sheria ya Zimbabwe, Virginia Mabiza imeeleza kuwa hawawezi kuwaruhusu wafungwa kupiga kura kwani sheria za nchi hiyo haziruhusu.

Aisha Mabiza amekishauri chama hicho cha MDC-T kuwa kama inataka wafungwa waruhusiwe kupige kura basi watume maombi katika Bunge la nchi hiyo ili lifanye marekebisho ya kisheria ambayo yatawapa ruhusa wafungwa kupiga kura.

“Ninashauriwa na washauri watu na uamuzi ambao ninauchukua ni ambao unaruhusiwa na sheria ya nchi, na kama ni jambo ambalo linakiuka katiba jambo pekee ambalo linahitajika ni kwenda Bungeni kuomba kubadilisha sheria,” alisema Mabiza.

Thursday, July 20, 2017

RAIS MAGUFULI ATOA SIKU 14 VITUO VYA MAFUTA KUFUNGA MASHINE ZA KIELEKRONIKI


Wamiliki wa vituo vyote vya mafuta nchini Tanzania wamepewa siku 14 kufunga na kuanza kutumia mashine za kielektroniki za kutolea risiti la sivyo wafutiwe leseni.

Rais Magufuli, ambaye ametoa agizo hilo, ameiagiza Wizara ya Fedha na Mipango na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kuhakikisha vituo vyote vya mafuta nchini vinatumia mashine hizo ambazo kwa Kiingereza zinafahamika kama Electronic Fiscal Petrol Printer na kusisitiza kuwa wamiliki watakaokiuka agizo hilo vituo vyao vifungwe na kufutiwa leseni.

"Na kwa hili natoa siku 14, wale wenye vituo vya mafuta wote, uwe upo Chato, uwe Biharamulo, uwe Kagera, uwe Dar es Salaam hakikisha una hiyo mashine, ndani ya siku 14," amesema Dkt Magufuli.

Mwishoni mwa wiki Mamlaka ya mapato Tanzania (TRA) ilivifungia vituo vya mafuta kutokana kutotimiza vigezo baada ya kutofunga mashine za kielektroniki kwenye pampu za mafuta.

WAZIRI MKUU AONYA MATAMSHI YA UCHOCHEZI


Waziri Mkuu Kassim Majaliwa, amesema Serikali itawashughulikia watu wote wanaotoa matamshi ya kichochezi nchini bila ya kujali nyadhifa zao.

Amesema ni vema watu wakawa makini na kijiepusha kutoa matamshi ambayo yataathiri mfumo wa maisha kwa wananchi wengine.

Waziri Mkuu ametoa kauli hiyo jana, Julai 19, wakati wa ibada ya mazishi ya mke wa Waziri wa Habari, Utamaduni, Sanaa na Michezo, Dkt. Harrison Mwakyembe, Linnah Mwakyembe iliyofanyika wilayani Kyela.

Amesema Serikali haitavumilia kuona baadhi ya watu wakitoa matamshi ambayo hayana tija kwa jamii na badala yake yanalenga kuwavuruga wananchi na kuchochea migogoro.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...