Tuesday, July 04, 2017

MAGUFULI AZITAKA NGO'S ZINAZOTETEA WANAFUNZI WENYE MIMBA WAFUNGUE SHULE ZAO

Rais John Magufuli amezitaka Asasi za Kiraia (NGO’s) kufungua shule kwa wanafunzi wanaopata mimba shuleni kama kweli zinawapenda wanafunzi hao.

Rais ameyasema hayo leo (Jumanne, Julai 4) alipokuwa akihutubia wakati wa uzinduzi wa mradi wa maji Sengerema.

“Si kwamba nawachukia wenye mimba, hata kwa bahati mbaya akapata mimba, kama hizo NGO zinawatetea sana, zifungue shule za wenye mimba, kwa sababu zinawapenda wenye mimba, wafungue shule zao,”amesema Rais leo.

Amesema hata hao wanaofanya makongamano ya kuhamasisha watu wapate mimba wafungue shule zao kwa ajili ya wanafunzi hao.

“ Haiwezekani fedha za walipa kodi, Sh 17 bilioni kila mwaka za kusomesha watoto wetu, kwenda kusomesha wakinamama, wazunguke, waimbe, waseme nini mimi ndiyo Rais, huo ndio ukweli,” amesema.

Amesema tatizo si wanaopata mimba, kwani wapo waliopata matatizo, kama kuugua kwa muda mrefu wakashindwa kwenda shule lakini ulianzishwa mpango maalum wa kuwasomesha katika mfumo usio rasmi.

KINGA YA UKIMWI YAANZA KUONESHA MAFANIKIO

Utafiti wa kinga ya kuzuia maambukizi ya virusi vya  Ukimwi, ulioanza kufanywa nchini miaka kadhaa iliyopita umeana kuonyesha mafanikio.

Lakini watafiti wamesema Watanzania watahitaji kuwa uvumilivu wa miaka michache ijayo kusubiri hatua za mwisho za ukamilishaji utafiti wa kinga hiyo kabla haijaanza kutimika rasmi.

Taarifa hizo zinakuja ikiwa wiki moja baada ya Kenya kuwa nchi ya kwanza barani Afrika kuanza kutumia dawa ya ugonjwa wa Ukimwi ambayo inaweza kuboresha afya na kurefusha maisha ya maelfu ya watu ambao wanasumbuliwa na magonjwa nyemelezi na ambayo hayakubali tiba nyingine.

Kwa miaka kadhaa  Chuo Kikuu cha Afya na Tiba Muhimbili (MUHAS) imekuwa ikiendesha utafiti kuhusiana na chanjo ya maambukizi ya virusi vya Ukimwi na katika hatua ya awali utafiti huo uliwahusisha baadhi ya watu wanaishi na virusi hivyo.

TIMU YA SINGIDA UNITED YAONESHA JEURI YA PESA, YANUNUA BASI LA MILLION 350/-

Baada ya kupata udhamini mnono kutoka katika kampuni ya michezo ya kubashiri ya SportPesa hatimaye klabu ya Singida United inazidi kutanua misuli yake katika ligi kuu ya Tanzania Bara kwa kutambulisha usafiri wao utakao tumika katika kusafirishia wachezaji.
 Akizungumza na waandishi wa habari jana katibu Mwenezi wa klabu hiyo Festo Sanga amethibitisha Singida United kununua Basi jipya lenye gharama ya shilling milioni 350.

Sunday, July 02, 2017

MTANGAZAJI WA AZAM TV ALIEPOTEA APATIKANA

Mtangazaji wa Kituo cha Televisheni cha Azam, Fatna Ramole amepatikana ikiwa ni saa 48 baada ya kudaiwa kutoweka.

Ndugu yake, Lulu Ramole amezungumza na mwandishi wa habari hii jana (Julai mosi) na kueleza kuwa kwa sasa yeye na Fatna wapo kituo cha Polisi, Kinondoni.

Lulu aliandika katika ukurasa wake wa twitter leo saa nane mchana akiwashukuru Watanzania kwa ushirikiano waliompa hadi dada yake kupatikana.

“Msamaria alitupigia simu amepatikana Makongo, nipo naye lakini siwezi kueleza kwa undani alivyopatikana, uchunguzi unaendelea,” amejibu kwa kifupi Lulu.

Kamanda wa Polisi Mkoa wa Kinondoni, Suzan Kaganda amethibitisha kupatikana kwa Fatna, lakini kwa maelezo na ufafanuzi zaidi alishauri familia ya mwanahabari huyo iulizwe.

“Lakini tutawaita hapa kwa mahojiano zaidi,” amesema

WABUNGE UJERUMANI WAIDHINISHA NDOA YA JINSIA MOJA

Wabunge nchini Ujerumani wameidhinishwa, kwa wingi wa kura, sheria ya kuhalalisha ndoa za wapenzi wa jinsia moja.

Wamefanya hivyos iku chache baada ya Kansela Angela Merkel kuondoa upinzani wake dhidi ya mpango huo.

Chini ya mabadiliko hayo sasa, wapenzi wanaotaka kuoana ambao awali walikubaliwa tu kuwa na ushirika, hadhi ya ndoa kamili na wana haki ya kuasili watoto.

TRUMP: TUMECHOKA KUIVUMILIA KOREA KASKAZINI

Rais wa Marekani, Donald Trump amesisitiza kwamba muda wa kimkakati wa uvumilivu kwa Korea Kaskazini umekwisha.

Katika hotuba ya pamoja juzi, akiwa na mwenzake wa Korea Kusini, Moon Jae katika bustani ya Rose kwenye Ikulu ya White house, Trump aliahidi ‘kuchukua hatua madhubuti’ dhidi ya programu ya nyuklia na makombora ya Korea Kusini akisema vitisho vyake vinafaa kupatiwa majibu ya kijasiri.

“Hizi si zama za kuvuta subira juu ya Serikali ya Korea Kusini ambayo imeshindwa kutekeleza wajibu wake,” alisema Trump.

Tuesday, June 27, 2017

'MARUFUKU CHAKULA KUSAFIRISHWA NJE YA NCHI' MAJALIWA

Waziri Mkuu, Kassim Majaliwa amepiga marufuku usafirishaji wa chakula nje ya nchi bila kibali na kuwataka wafanyabiashara kuuza chakula kwenye maeneo yenye uhaba nchini.

Majaliwa ametoa agizo hilo jana, Jumatatu wakati akihutubia Baraza la Eid katika Msikiti wa Masjid Riadha mjini Moshi mkoani Kilimanjaro.

Waziri Mkuu huyo amesema kuwa kuna maeneo ambayo wananchi hawakupata chakula vizuri kutokana na uhaba wa mvua hivyo wafanyabiashara wapeleke chakula kwenye maeneo hayo.

“Serikali bado haijatoa kibali cha kutoa chakula nje ya nchi, kama unaona kuna umuhimu kaombe kibali, lakini utapewa kibali cha kusaga upeleke unga na siyo mahindi,”amesisitiza  Majaliwa.

Majaliwa ameonya kuwa kwa wale watakao kamatwa wakisafirisha mahindi nje ya nchi kinyume na utaratibu, mahindi hayo yatataifishwa na kupelekwa kwenye ghala la Taifa na magari yatapelekwa polisi.

Amesema kuwa Serikali imepokea barua za maombi ya kupeleka chakula nchi jirani, lakini bado haijatoa ruhusa.

Monday, June 26, 2017

JAMBO TZ INAWATAKIA EID MUBARAK WAISLAMU WOTE DUNIANI

Uongozi na wafanyakazi wote wa Jambo Tz Blog wanawatakia watanzania wote kwa ujumla Eid Mubarak na mapumziko mema katika sikukuu ya Eid El Fitr.

Sunday, June 18, 2017

OLE SENDEKA AWAKUBALI WAPINZANI MSIBANI KWA MAMA YAKE

Mkuu wa Mkoa wa Njombe, Christopher Ole Sendeka amesema tofauti za itikadi za kisiasa zisitumike kuwagawa Watanzania, bali ziwe chachu ya kufanikisha maendeleo.

Ole Sendeka aliyasema hayo jana, wakati wa kuaga mwili wa mama yake Raheli Sendeka kwenye ibada iliyofanyika katika Kanisa la Kiinjili la Kilutheri Tanzania (KKKT), Usharika wa Engarenarok jijini Arusha.

Alisema baada ya kutokea kwa msiba huo, viongozi wa kwanza kufika nyumbani kwake kumpa pole walikuwa mbunge na diwani wa Chadema, hivyo amepata somo kuwa tofauti za kisiasa hazipaswi kuondoa umoja na upendo wa Watanzania. Alisema mbunge wa kwanza kufika nyumbani kwake Ngarenaro jijini hapa ni wa Siha mkoani Kilimanjaro (Chadema), Dk Godson Mollel na diwani wa Ngarenaro (Chadema), Issaya Doita.

MAJERUHI WA LUCKY VINCENT KUREJEA NCHINI MWEZI WA NANE

Watoto watatu walionusurika katika ajali iliyoua wanafunzi 32, walimu wawili na dereva wa Shule ya Lucky Vincent ya mjini Arusha, huenda wakaruhusiwa kurejea nchini baada ya miezi miwili.

Taarifa hiyo imetolewa na Mbunge wa Singida Kaskazini, Lazaro Nyalandu katika mtandao wake wa kijamii wa Facebook.

Pia, Nyalandu ameandika katika mtandao huo kuwa watoto hao; Doreen Mshanga, Saidia Ismael na Wilson Tarimo wanategemewa kutembea tena.

Hata hivyo, kwa sasa Doreen, atahamishiwa katika kituo maalumu kwa ajili ya matibabu ya uti wa mgongo cha Madonna katika mji wa Lincoln, Nebraska.

“Katika watoto wote hao watatu, Doreen ni muujiza mkubwa zaidi,” amesema Nyalandu.

UTHAMINI MOYO WAKO, KAA MBALI NA MAUMIVU

HAKUNA ubishi kuwa mapenzi yanachukua nafasi kubwa sana katika maisha ya binadamu, ipo dhahiri kwamba mapenzi yanaweza kuleta furaha maishani mwako lakini wakati huohuo  maumivu, mateso na karaha.

Watu wengi bado wanalizwa na mapenzi na hii ni kwa sababu hawafuati kanuni sahihi za mapenzi. Ndiyo… mapenzi yana kanuni zake.

Kwa bahati mbaya kabisa, kwa sasa mapenzi yamegeuzwa na kuwa kama kitu cha kujaribu au kufanyia biashara ndiyo maana yanawatesa wengi.

Lakini ni kwa nini mapenzi yaendelee kututesa?  Au ni kwa sababu hatujui maana halisi ya mapenzi? Hebu tuyaangalie mapenzi kwa jicho la tatu, kisha tuchukue hatua.

MAPENZI NI NINI?
Katika hali ya kawaida, mapenzi hayaelezeki kuwa ni nini. Ni vigumu sana mtu kukueleza maana ya mapenzi ndiyo maana kila mtu ana uelewa tofauti juu ya suala hilo.

Saturday, June 17, 2017

MANGULA AWATAKA WAPINZANI KUACHA KUDANDIA TRENI KWA MBELE SAKATA LA MCHANGA WA MADINI

Makamu Mwenyekiti wa CCM, Tanzania Bara, Philip Mangula amesema kitendo alichokifanya Rais John Magufuli cha kuwafichua wanaotorosha mchanga wa madini kipo kwenye ilani ya chama hicho hivyo wapinzani waache kudandia treni kwa mbele.

Mangula amesema hayo leo (Jumamosi) wakati akizungumza na wanachama wa CCM kwenye kongamano la kuunga mkono juhudi za Rais na kumpongeza kwa kuwafichua mafisadi lililoandaliwa na wanachama hao.

"Alichokifanya Rais kipo ndani ya ilani ya chama, wapo wanaotaka kudandia treni kwa mbele wakidai wao ndiyo walikuwa na mawazo hayo, nataka niwaambie Rais anatekeleza ilani hiyo ni mipanngo ya CCM, "amesema.

Pia, Mangula amewaonya watu wanaoibuka na kutaka kukwamisha kazi anayofanya Magufuli kuwa hawataweza na nchi haitashtakiwa kama wanavyodai.

“Niwatoe hofu wananchi na wanachama wote kuwa nchi iko salama zaidi tumuunge mkono Rais wetu kuwafichua wezi wa mali za nchi, "amesema

MTANZANIA ATUPWA JELA UINGEREZA KWA KOSA LA KUPOST PICHA ZA MAREHEMU FACEBOOK

Mwanaume mmoja anayedaiwa kuwa ni Mtanzania amehukumiwa kifungo cha miezi mitatu jela nchini Uingereza kwa kosa la kurusha katika ukurasa wake wa Facebook, picha za mtu aliyefariki dunia kutokana na moto uliounguza jengo la ghorofa la Mnara wa Grenfell lililopo nchini humo.

Pia, mtu huyo ametakiwa kulipa faini ya Sh579,880 kwa mwathirika wa tukio hilo.

Mtanzania huyo, Omega Mwaikambo (43) alituma video na picha za mwili wa marehemu uliokuwa kwenye begi  na baadaye picha nyingine tano zikionyesha uso wa  marehemu huyo.

Friday, June 16, 2017

HII NDIO NDEGE BINAFSI ALIYOKUJA NAYO MWENYEKITI WA KAMPUNI YA BARRICK GOLD CORPORATION KWAAJILI YA KUJA KUFANYA MAZUNGUMZO NA RAIS MAGUFULI

Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania Dkt. John Pombe Magufuli katika picha ya pamoja na  Mwenyekiti wa Kampuni ya Barrick Gold Corporation ambayo ni mmiliki mkubwa wa kampuni ya Acacia Mining Limited Prof. John L. Thornton pamoja na Balozi wa Canada hapa nchini Mhe. Ian Myles na Waziri wa Sheria na Katiba Mhe. Prof. Palamagamba Kabudi.

WANAFUNZI 56 WALIOCHAGULIWA KUJIUNGA NA KIDATO CHA TANO 207 WABADILISHIWA SHULE

Taarifa kutoka ofisi ya Rais-TAMISEMI imeonyesha mabadiliko ya kuwapangia shule wanafunzi 56 waliochaguliwa kujiunga na Kidato cha Tano katika Shule ya Sekondari Madibira Tahasusi ya PCB na kuwapeleka katika shule zingine zenye tahasusi (Combination) hiyo ndani ya Mkoa wa Mbeya na Mikoa ya jirani. Mabadiliko haya ni kwa sababu maalum.

Aidha, wanafunzi wapya 56 wamechaguliwa kujiunga na kidato cha Tano katika shule ya Sekondari Madibira Tahasusi ya CBG kama inavyoonekana kwenye tovuti. Wanafunzi hawa wanapaswa kuripoti katika shule walizopangiwa tarehe 17 Julai, 2017. 
TAARIFA KWA UMMA (15-06-2017)

 Tafadhali bofya chini Kujua Orodha ya Wanafunzi waliochaguliwa na Waliobadilishwa kidato cha 5 kwa sababu maalum.

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...