Wednesday, December 17, 2014

MAGAZETI YA LEO JUMATANO DESEMBA 17, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

.
.
.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UCHAGUZI SERIKALI ZA MITAA WAMWAGA DAMU

Kamanda wa Polisi mkoani Tabora, Suzan Kaganda. PICHA|MAKTABA 

Wakati tukio la Bukombe likihusisha mtu kuchinjwa katika sherehe za ushindi wa mkewe kuwa mwenyekiti wa mtaa, huko Nzega kijana moja alipigwa risasi na polisi wakati wa kusubiri matokeo ya uchaguzi huo.
Bukombe
Mume wa mshindi wa kiti cha mwenyekiti wa Serikali ya Mtaa wa Kapela, wilayani Bukombe ameuawa baada ya kuchinjwa katika hafla ya ushindi wa mkewe.
Mtu huyo, Bundara James (56), aliuawa usiku wa kuamkia juzi katika Mtaa wa Kapela ulioko kwenye Kata ya Igulwa wilayani Bukombe muda mfupi baada ya kumalizika kwa hafla ya kusherehekea ushindi huo.
Mke wa marehemu ambaye sasa ni mwenyekiti wa mtaa huo, Lusia Samwel alisema mumewe ambaye ni mtumishi wa Halmashauri ya Wilaya ya Mbogwe, alikutwa amechinjwa na watu wasiojulikana ambao walitoweka baada ya tukio hilo wakiacha panga walilofanyia uhalifu kwenye eneo la tukio.

Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

NAPE: KAKOSA YA CCM YAMEINUFAISHA UKAWA

 
Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye. PICHA|MAKTABA 

Chama Cha Mapinduzi (CCM) kimesema kilifanya makosa katika baadhi ya maeneo ambayo yamekigharimu na kusababisha wananchi kupiga kura za hasira kukiadhibu katika Uchaguzi wa Serikali za Mitaa.

Katibu wa Itikadi na Uenezi wa CCM, Nape Nnauye alisema hayo jana alipokuwa akizungumza na waandishi wa habari kuhusu matokeo ya uchaguzi huo ambao umeonyesha kuvinufaisha vyama vya upinzani kupitia umoja wao wa Katiba ya Wananchi (Ukawa).

Nape alisisitiza kwamba makosa hayo ndiyo yaliyosababisha wapinzani kujinyakulia mitaa kadhaa kwa wepesi. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

PAKISTAN YAOMBOLEZA MAUAJI YA WAATOTO

Raia wa Pakistan wakiwaombea watoto 140 waliouawa katika shambulizi la kigaidi katika shule moja nchini humo. 
Raia nchini Pakistan wanaadhimisha siku tatu za maombolezo kuwakumbuka zaidi ya watu 140 waliouwawa,karibia wote wakiwa watoto katika shambulio lililotekelezwa na kundi la Taliban.
Waziri mkuu Nawaz Shariff ameitisha mkutano wa vyama vyote vya kisiasa nchini humo kujadili vile watakavyoweza kujibu shambulizi hilo la Peshawar.
Ameelezea shambulizi hilo kuwa janga la kitaifa lililotekelezwa na wakatili.
Mkuu wa jeshi Jenarali Raheel Shariff ameahidi kulipiza kisasi kwa kila tone la damu linalomwagika.
Nchini India ,shule zimenyamaza kwa dakika mbili ili kutoa heshima kwa wale waliouawa.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year. 

HAITI WAANDAMANA KUMNG'OA RAIS WAO

Rais wa Hait mICHAEL Martelly
Mamia ya raia wa nchini Haiti wameandamana katika mitaa ya Port-au-Prince wakishinikiza Rais Michel Martelly kuondoka madarakani.
Hata hivyo maandamano hayo yamegeuka vurugu baada polisi kutumia mabomu ya mchozi kuwatawanya waandamanaji hao. polisi wamepambana na waaandamanaji hao ambao wamekuwa wakirusha mawe na kuchoma moto matairi mitaani.
Madai ya raia hao ni kumtaka Rais Martelly kuitisha uchaguzi na kuunda serikali,ambapo uchaguzi ulitakiwa kuitishwa miaka mitatu iliyopita.
Waziri mkuu wa Haiti Laurent Lamothe, siku ya jumapili aliamua kuachia ngazi baada ya shinikizo la siku mbili.Maoni kutoka vyama vya upinzani ni kwamba wanamtaka rais Martelly kujiuzulu. Awali Waziri wa mambo ya nje wa Marekani John Kerry ameitaka Hait kuitisha uchaguzi mara moja.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.  

Na BBC

PLUIJM ATUA YANGA, MAXIMO ATIMULIWA MAZOEZINI

Kocha Hans van Pluijm akiwasili kwenye Uwanja wa Ndege wa Kimataifa wa Julius Nyerere Dar es Salaam juzi, kuchukua mikoba ya Marcio Maximo aliyetupiwa virago Yanga. (Na Mpigapicha Wetu).

Kocha Hans van Pluijm akiwasili kwenye uwanja wa ndege wa kimatafa wa Julius Nyerere Dar es Salaam juzi.

UONGOZI wa Klabu ya soka ya Yanga jana asubuhi ulilazimika kumwondoa mazoezini Kocha Mkuu, Marcio Maximo na kumrudisha klabuni ili kumalizana naye kabla ya kuanza safari ya kurudi kwao Brazil, huku akiiacha timu hiyo ikifundishwa na kocha anayetarajiwa kuchukua nafasi yake, Hans van Pluijm.

Maximo aliondolewa mazoezini na kupakiwa kwenye basi dogo la timu hiyo aina ya Toyota Hiace lililokuwa likiendeshwa na meneja wa timu hiyo, Hafidh Salehe.
Aliambana na msaidizi wake, Leonard Neiva na kiungo Emerson de Oliveira Roque aliyesajiliwa hivi karibuni akitokea nchini Brazil.
Kitendo hicho kilitokana na uongozi huo kufikia makubaliano ya kumtimua kazi kocha huyo pamoja na msaidizi wake Neiva, kutokana na kushindwa kuipa mafanikio tangu alipoanza kuifundisha timu hiyo katika kipindi cha miezi minne.

Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MLIBERIA APATAITC, MUSHEED ASUBIRI SIMBA

Kpah Sherman

Kpah Sherman
MSHAMBULIAJI mpya wa Yanga, Kpah Sherman sasa ni ruksa kucheza katika Ligi Kuu baada ya Shirikisho la Soka Tanzania (TFF), kuthibitisha kwamba hati yake ya uhamisho kumruhusu kucheza soka nchini tayari imeshafika.

Aidha, wakati Sherman akiwa na uhakika wa kuitumikia klabu hiyo, TFF imethibitisha kuchelewa kwa hati ya uhamisho ya kiungo mpya wa Yanga, Emerson de Oliviera Roque ambaye aliombewa ITC ili kuitumikia timu hiyo.
Licha ya kuwepo kwa taarifa za kukatwa kwa mchezaji huyo na nafasi yake kupewa aliyekuwa mchezaji wa Simba, Amisi Tambwe, Mkurugenzi wa Mashindano wa TFF, Boniface Wambura alisema jana kuwa ITC hiyo haijafika.

Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

KLABU BINGWA DUNIA MADRID YATINGA FAINALI

Raha ya goli ni shamra shamra, wanapongezana.
Wakicheza katika dimba la Stade de Marrakech. Mjini Marrakech Nchini Morocco, Mabingwa wa Ulaya Real Madrid wamepata ushindi mnono wa goli 4-0 dhidi ya Cruz Azul na kutinga Fainali ya Mashindano ya FIFA ya Kombe la Dunia kwa Klabu.
Real Madrid walianza kupata magoli yake dakika ya kumi na 15 kupitia kwa beki Sergio Ramos mshambuliaji Karim Benzema akaongeza la pili dakika ya 36,
Kipindi cha Pili, Gareth Bale, alifunga bao la 3 na Isco, kuhitimisha kwa goli la 4 na kuipelea Madrid fainali.
Azul walikosa penati dakika ya 40 iliyopigwa na Gerardo Torrado, na kuokolewa na kipa Iker Casillas.
Real wanasubiri mshindi wa mchezo wa leo kati ya San Lorenzo ya Argentina na Auckland City ya New Zealand.
 Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

CHELSEA NUSU FAINALI CAPITAL CUP

Chelsea wakipasha
Chelsea, wakicheza katika uwanja wa iPro Stadium waliwachabanga timu ya Derby County, Bao 3-1 kwenye Kombe la Ligi maarufu kama Capital One Cup, na kutinga Nusu Fainali.
Eden Hazard, ndie alianza kuipatia Chelsea, goli la kwanza dakika ya 33 kabla ya Filipe Luis, kufunga goli la pili dakika ya 56 huku Andre Schurrle, akihitimisha ushindi kwa goli la dakika ya 82.
Bao la kufutia machozi kwa Derby lilifungwa na Craig Bryson, Dakika ya 71.
Kwenye Mechi nyingine ya Robo Fainali Sheffield United, waliwashangaza Southampton kwa kuwabanjua Bao 1-0.
Bao la ushindi la Sheffield lilifungwa na McNulty, Dakika ya 63. Southampton walibaki 10 baada ya Gardos kupewa Kadi Nyekundu.
Leo Usiku zitachezwa Robo Fainali nyingine mbili ambapo Liverpool, watakuwa Wageni wa Bournemouth.
Huku katika uwanja wa white Hart Lane Tottenham Hotspur watawakaribisha Newcastle United. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

Tuesday, December 16, 2014

UKAWA MBELE KWA MBELE

Wafuasi wa CHADEMA mjini Nansio Wilaya ya Ukerewe, Mwanza wakishangilia ushindi katika uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika juzi. 

Matokeo ya Uchaguzi wa Serikali za Mitaa uliofanyika juzi, yanaonyesha kuimarika kwa upinzani nchini baada ya kupata viti vingi vya uenyekiti wa mitaa na vijiji, pamoja na mamia ya wajumbe wa Serikali husika.
Hayo yanaonyesha kuwa vyama hivyo vimeanza kuimarika katika ngazi za chini, tofauti na ilivyokuwa mwaka 2009, katika uchaguzi ambao CCM kilipata ushindi wa kishindo wa asilimia 91.72, huku wapinzani wakigawana asilimia 8.28 zilizobaki.
Licha ya uchaguzi wa juzi kugubikwa na kasoro lukuki, upinzani umeonekana kuchomoza huku katika baadhi ya mikoa ukipata ushindi maradufu hasa katika ile ambayo una nguvu kubwa wakati katika maeneo ambayo ulikuwa na viti vichache au kutokuwa navyo kabisa, umeibuka na kuipokonya CCM baadhi ya mitaa na vijiji.

Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year

MARCIO MAXIMO ATUPIWA VIRAGO YANGA NI BAADA YA KICHAPO CHA 2-0 KUTOKA SIMBA

YANGA SC imeirejea historia yake ya kuwatimia makocha wake muda mfupi tu baada ya kula kichapo kutoka kwa watani zao Simba ambapo tayari uongozi wa Yanga umelivunja benchi la ufundi la timu hiyo lililokuwa likiongozwa na makocha Wabrazil, Marcio Maximo na Msaidizi wake, Leonardo Neiva na kuwarejesha Mholanzi, Hans Van der Pluijm na  Charles Boniface Mkwasa 'Master'.

Maximo anaondolewa baada ya kipigo cha mabao 2-0 kutoka kwa mahasimu Simba SC Jumamosi katika mchezo wa Nani Mtani Jembe, wakati Pluijm anawasili usiku huu na kesho atasaini Mkataba na kuanza kazi. Mkwasa tayari alisaini Mkataba wiki kadhaa zilizopita na ameridhika kufanya kazi chini ya Pluijm tena.
Maximo na Leonardo walitua Yanga SC Julai mwaka huu kurithi mikoba ya Pluijm na Mkwasa ambao walipata kazi Uarabuni. Hata hivyo baada ya muda usiozidi mwezi mmoja, Pluijm na Mkwasa waliacha kazi Uarabuni, wakidai kukerwa na kuingiliwa na viongozi wa klabu yao katika masuala ya kiufundi.
  Pluijm alirudi Ghana wakati Mkwasa alirejea nyumbani Tanzania kabla ya kuajiriwa Shirikisho la Soka Tanzania (TFF) kama Mkufunzi Mkuu. Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

UTITIRI WA WACHEZAJI WA KIGENI KUTAICHIMBIA KABURI SOKA YA TANZANIA NA KUUWA TIMU YA TAIFA KAMA ILIVYO UINGEREZA

Simon Sserunkuma 
Mshambuliaji huyo raia wa Uganda alikuja nchini na timu ya Express ya nchini humo na kucheza mechi mbili za kirafiki dhidi ya Simba na Yanga na ndipo viongozi hao wa Yanga walipomwona na kumleta nchini ili kufanya naye mazungumzo lakini mambo yakawa tofauti kwani alitoroshwa kimya kimya na kupelekwa Zanzibar ambako Simba iliweka kambi kujiandaa na mechi ya Nani Mtani Jembe iliyochezwa juzi Jumamosi.
ACHANA na Yanga kufungwa mabao 2-0 na Simba katika mechi ya Nani Mtani Jembe, imebainika kuwa Simba iliifanyia Yanga umafia kwa mchezaji Simon Ssrenkuma baada ya kumtorosha kutoka mikononi mwa viongozi wa klabu hiyo na kwenda kumficha kwenye kambi ya timu hiyo visiwani Zanzibar wiki iliyopita.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

MAGAZETI YA LEO JUMANNE DESEMBA 16, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC07117
DSC07114
DSC07116
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutangaza matangazo mbalimbali na pia kutoa maoni yako kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year

THIERRY HENRY ATANGAZA RASMI KUSTAAFU SOKA

Theirry-Henry-in-action-o-007 
Katika ulimwengu wa soka leo kuna habari kubwa ambayo imeenea duniani kutokana na staa mkubwa na mkongwe Thierry Henry kutangaza kustaafu soka na kujiunga na shughuli nyingine. Nyota huyo  ambaye ameng’aa kwenye mchezo huo kwa muda mrefu sana akichezea vilabu mbalimbali ikiwemo Arsenal na Barcelona.
download
Henry ametangaza rasmi kustaafu soka dakika chache zilizopita na kusema kuwa kuanzia mwakani ataanza kujishughulisha kama Balozi wa Sky Sports huku akisema kuwa anajisikia furaha kuchezea vilabu vikubwa na pia anaamini anajiunga na kituo kikubwa cha Television na matarajio yake ni kuwa mchambuzi bora wa michezo kwenye kituo hicho.
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year.

HAYA NDIYO MAAMUZI MAGUMU YA YANGA KUHUSU MBRAZIL EMERSON

Moja ya vichwa vya habari vilivyokuwa vimepambwa na habari kumhusu Emerson.

Taarifa za usajili na kuachwa wachezaji zinazidi kuingia na safari hii inasemekana kuwa kiungo Mbrazil Emerson amekuwa mhanga wa kwanza wa kuondoka kwa kocha Mbrazil Marcio Maximo baada ya mchezaji huyo kuachwa na Yanga.
Mbrazil huyo anaondoka Yanga baada ya kucheza mechi moja pekee dhidi ya Simba ambako Yanga ilifungwa 2-0.
Emerson alishindwa kuwaridhisha mashabiki wa Yanga ambao wengi walionyesha kukerwa na uwezo mdogo wa kiungo huyo katika dakika 45 alizocheza kwenye mechi dhidi ya Simba.
Emerson alikuja nchini siku chache zilizopita ambapo alipaswa kuziba nafasi iliyoachwa wazi na mshambuliaji Genilson Santos Santana Jaja ambaye hakurudi baada ya kuondoka nchini kufuatia kusimama kwa ligi. 
Asante kwa kutembelea blog hii ya Jambo Tz, ili kuboresha blog yetu tunatoa fulsa ya kutoa maoni kupitia namba ya simu (WhatsApp & SMS) 0715 221198, E-mail jambotz8@gmail.com. Merry Chistmass & Happy New Year

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...