Tuesday, July 29, 2014

ISRAEL: TUTAJILINDA NA HAMAS

Waziri mkuu wa Israel Benjamin Netanyahu amesema Israel inatakiwa kujiandaa kwa ajili ya mpango wa muda mrefu katika Gaza.
Hata hivyo ameelezea msimamo wake dhidi ya kundi la wapiganaji wa Hamas. Netanyahu amesema Hamas wanapaswa kusambaratishwa na hilo ndilo lengo la Israel.
‘Tulijua kuwa tungekuwa na siku ngumu, hii ni siku ngumu na ya maumivu kutokana na mashambulizi haya, nguvu na malengo vinatakiwa ili kuendeleza mapambano dhidi ya kundi hilo, anasisitiza Netanyahu.
Wizara ya afya ya Gaza imesema kuwa raia 10 wa palestina wameuawa katika shambulio la makombora yaliyolenga uwanja wa mpira yakitekelezwa na Israel..

Kati ya waliouawa katika shambulio hilo ni watoto saba waliokuwa wakicheza uwanjani hapo ambapo walipigwa na kufa papo hapo.
Hamas imeilaumu Israel kwa shambulio hilo,huku msemaji wa Israel akidai kuwa shambulio hilo lilitekelezwa kwa bahati mbaya.
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Monday, July 28, 2014

KATIBA MPYA: WASSIRA, LIPUMBA, LISSU 'WANYUKANA'


http://jambotz8.blogspot.com/
Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais (Uratibu na Uhusiano), Stephen Wassira akizungumza kwenye mdahalo uliofanyika jijini Dar es Salaam jana. Kulia ni Mbunge wa Singida Mashariki(Chadema) Tundu Lissu na katikati ni Mwenyekiti wa CUF,  Profesa Ibrahim Lipumba.

Waziri wa Nchi Ofisi ya Rais, Uhusiano na Uratibu, Stephen Wassira akiwakilisha CCM, Mbunge wa Singida Mashariki, Tundu Lissu na Mwenyekiti wa CUF, Profesa Ibrahim Lipumba, jana walitoana jasho katika mdahalo wa Katiba ulioandaliwa na East African Business and Media Institute.
Mdahalo huo uliohudhuriwa na watazamaji wapatao 500, ulikuwa na mada inayosema: ‘Nani anakwamisha Upatikanaji wa Katiba Mpya.’ Kila upande ulitumia fursa hiyo kutupa shutuma kwa mwingine huku jazba na kelele vikitawala miongoni mwa waliohudhuria.
Hata hivyo, suala la muundano wa serikali ndiyo uliochukua nafasi kubwa katika mdahalo huo huku Umoja wa Katiba ya Wananchi (Ukawa) ukiishutumu Serikali ya CCM kuwa ndiyo kikwazo cha upatikanaji wa Katiba Mpya nayo ikitupa mpira huo kwa Ukawa kwa kitendo chake cha kutoka katika Bunge Maalumu la Katiba. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MAGAZETI YA LEO JUMATATU JULAI 28, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01214
DSC01216
DSC01217 
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

PAPA AOMBA VITA VIMALIZWE

Pope Francis
Papa Francis ameomba amani kwa dhati katika hotuba ya kila juma katika medani ya St Peter's mjini Rome.
Aliacha kusoma hotuba aliyoandika kuomba vita vimalizwe na hisia ikisikika kwenye sauti:
"makaka na madada, hapana vita, hapana vita, nawafikiria hasa watoto ambao wananyimwa matumaini ya maisha ya maana, ya siku za mbele, watoto waliokufa, walioumia, watoto walioachwa na vilema, waliokuwa yatima, watoto ambao wanacheza na mabaki ya vita, watoto wasiojua kucheka.
Acheni kupigana. Nakuombeni kwa moyo wangu wote. Tafadhali, acheni sasa hivi!" Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

UKRAIN KUJIBU MAPIGO

wanajeshi wa Ukrain
Jeshi la Ukrain limeanza kujihami mashariki mwa nchi hiyo dhidi ya mashambulizi ya waasi wa Urusi kufuatia kutunguliwa kwa ndege ya Malaysia katika eneo hilo.
Msemaji wa serikali ya Ukrain Andriy Lysenko amesema jeshi la nchi hiyo lilidhamiria kulifunga eneo hilo ili kupisha uchunguzi wa watalaamu kuhusiana na chanzo cha kuanguka kwa ndege hiyo.
Ndege ya Malaysia iliyokuwa imebeba watu 300 iliangushwa katika eneo hilo lililo chini ya udhibiti wa waasi.
Waangalizi wa kimataifa wanasema mapigano hayo yataadhiri uchunguzi wa ajali hiyo ya ndege, mapigano makali yameripotiwa katika amaeneo yanayozunguka mji wa Horlivka na Shakhtarsk. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

MBEYA CITY, NDANDA FC, STAND UNITED: 'ONYESHENI BINSLUM HAKUKOSEA KUWADHAMINI'


Ibrahim Bakari 

Ninataka kumpongeza Mkurugenzi wa Kampuni ya Bin Slum, Nassor Bin Slum nikiwa na sababu moja kubwa, BinSlum hakutaka biashara za timu kubwa, alichoangalia ni kuzisaidia timu ndogo zilizopanda Ligi Kuu.

Katika siku za karibuni, klabu za Mbeya City ya Mbeya, Ndanda FC ya Mtwara na Stand United ya Shinyanga, zimepata udhamini wa mamilioni na Nassor BinSlum kupitia kampuni yake ya BinSlum.
BinSlum alianza kwa kuidhamini Coastal Union ya Tanga ambayo alisema ameondoka kwenye timu hiyo kutokana na majungu.
Sitaki kuzama kwa hayo yaliyotokea Coastal Union, lakini naipongeza kampuni hiyo inayojishughulisha na uuzaji wa betri na matairi ya magari.
Ninataka kumpongeza Mkurugenzi wa Kampuni ya Bin Slum, Nassor Bin Slum nikiwa na sababu moja kubwa, BinSlum hakutaka biashara za timu kubwa, alichoangalia ni kuzisaidia timu ndogo zilizopanda Ligi Kuu. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Saturday, July 26, 2014

BASI LA HOOD LAPATA AJALI ASUBUHI YA LEO LIKITOKEA MBEYA


Muda mchache baada ajali kutokea. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
 Askari wa usalama wa barabarani wakiwa wamefika eneo la tukio  na baadhi ya Mashuhuda wakishuhudia ajali hiyo

SUDAN KUSINI YAKABILIWA NA BAA LA NJAA

Baa la njaa nchini Sudan Kusini

Baraza la usalama la Umoja wa Mataifa limeelezea uhaba wa chakula nchini Sudan Kusini kama mbaya zaidi kuwahi kuonekana duniani na kuyataka mataifa ambayo yaliahidi kutoa msaada wa zaidi ya dola millioni mia sita kutoa fedha hizo.
Limeonya kuwa vita vinavyoendelea kati ya vikosi vya serikali na waasi huenda vikasababisha baa la njaa nchini humo.
Shirika la chakula duniani WFP limesema kuwa iwapo hatua za haraka hazitachukuliwa watoto elfu hamsini huenda wakapoteza maisha yao kutokana na utapia mlo mwaka huu huku thuluthi moja ya raia wakikabiliwa na na viwango hatari vya njaa. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

REINA ATHIBITISHA KUPENDA KUENDELEA KUICHEZEA LIVERPOOL

438662_heroa
MLINDA mlango wa Liverpool, Pepe Reina amejitia kitanzi mwenyewe katika klabu hiyo, licha ya kudai anapenda kustaafu soka la kimataifa nchini Hispania.
 Akicheza kwa mkopo Seria A katika klabu ya Napoli msimu uliopita-Reina alianza kuhusishwa kujiunga na bosi wake  wa zamani wa Anfield Rafael Benitez-na kuzua maswali juu ya hatima yake Liverpool.
 Reina amesisitiza kuwa anaheshimu mkataba wake Anfield-ambao utamalizka mwaka 2016 kabla ya kwenda nchini Hispania.
 “Nina mkataba ambao nahitaji kuuheshimu Liverpool,” Reina aliiambia radio ya Hispania ya Cadena Ser. “Ninafanya mazoezi vizuri na nipo sawa na wachezaji wenzangu”.
 “Nipo hapa kwa ajili ya kukaa”.
 “Sijazungumza na Brendan Rodgers, ni siku nne tu tangu nifike hapa, naangalia kufanya mazoezi vizuri ili kurudi katika kiwango changu”.
 Reina mwenye miaka 31 alianza maisha yake ya soka katika klabu ya Barcelona, kabla ya kwenda Villarreal na kuelekea ligi kuu nchini England, na sasa amekiri kuwa kurudi La Liga itakuwa nafasi nzuri kwake. Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz
 “Nimekuwa nikiwaza hili kwa muda mrefu kuwa ni vizuri kurudi ulipotoka,” Reina aliongeza.
 “Wakati Rafa Benitez ananisajili Liverpool mwaka 2005, nilikubali na nilisema nitarudi Hispania baadaye”.

MAGAZETI YA LEO JUMAMOSI JULAI 26, 2014 YA UDAKU, MICHEZO NA HARD NEWS

DSC01150
DSC01151
DSC01152
Kuwa wa kwanza kupata habari zetu kwa ku-Like page yetu ya facebook kwa ku-click/ bofya neno Jambo Tz

Pro

PropellerAds

LinkWithin

Soma na Hizi Pia Plugin for WordPress, Blogger...